28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Mheshimiwa Spika, Bunge la Tisa lilipitisha sheria inayohusiana na nchi yetu kwa kupitia<br />

mabenki kuwe na mikopo ya muda mrefu katika sekta ya ujenzi wa nyumba mortgage. Nchi yetu<br />

ujenzi wa nyumba inabidi wananchi wachukue muda refu katika ujenzi wa nyumba zao. Je,<br />

Wizara katika kuwafanya Watanzania waweze kujenga nyumba kwa mikopo ya muda mrefu<br />

imejipanga vipi Ninavyoamini na ndivyo ilivyo sekta ya nyumba inaweza ikaleta fedha nyingi<br />

katika uchumi wa nchi yetu.<br />

Mheshimiwa Spika, ni utaratibu wa kawaida kila mwaka Serikali kuongeza mshahara<br />

wakati wa bajeti kwa wafanyakazi wa Serikali. Ingawa ongezeko hilo la mshahara huwa do<strong>go</strong>, ni<br />

jambo zuri. Jambo la kusikitisha watumishi waliokwishastaafu, huu ni mwaka wa tatu<br />

hawajaongezewa pensheni zao. Nadhani umefika wakati wastaafu hao waongezewe pensheni<br />

zao.<br />

Mheshimiwa Spika, Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) pamoja na majukumu mengine pia<br />

ina dirisha la kilimo. Hivi sasa kuna kauli mbiu ya “Kilimo Kwanza”. Mikopo ya kilimo inategemewa<br />

itolewe na TIB wakati uwezekano wa kuendeleza kilimo kwa mikopo TIB ni mdo<strong>go</strong>. Je, Wizara iko<br />

tayari kuchukua hatua za dharura kwa kupata mtaji kwa TIB.<br />

MHE. AMINA ABDALLAH AMOUR: Mheshimiwa Spika, ukusanyaji wa mapato na misamaha<br />

ya kodi holela, inapunguza mapato ya Serikali. Utafiti unaonesha kuwa, misamaha ya kodi<br />

inapoteza wastani wa asilimia sita ya Pato la Taifa.<br />

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali itafute vyanzo vingine vya mapato na pia hii<br />

misamaha ya kodi kwa wawekezaji angalau ifikie asilimia mbili ya mapato ya Taifa. Pamoja na<br />

hilo, Halmashauri zetu zinakusanya mapato kido<strong>go</strong> sana, washauriwe watafute vyanzo vingine vya<br />

kuongeza mapato ili tuweze kuondokana na umaskini.<br />

Mheshimiwa Spika, kuna Makampuni mengi tu ambayo hayalipi kodi, mengine<br />

Wafanyakazi wa TRA hawayajui na mengine wanayajua lakini wanachukua rushwa na kuyaachia<br />

yale Makampuni yaendelee kufanya kazi bila kulipa kodi. Naishauri Serikali ifuatilie na<br />

wanaobainika kufanya hivyo, wachukuliwe hatua mara moja.<br />

Mheshimiwa Spika, Tume ya Mipan<strong>go</strong> katika Ofisi ya Rais imepitia Dira ya Taifa na kutafsiri<br />

katika Mpan<strong>go</strong> wa Muda Mrefu wa utekelezaji ikianzia na Mpan<strong>go</strong> wa Kwanza wa Miaka Mitano.<br />

Hata hivyo, Serikali haijaeleza kinagaubaga, mgawanywo wa madaraka na mamlaka kati ya<br />

Tume ya Mipan<strong>go</strong> na Wizara ya Fedha na Uchumi. Tume ya Mipan<strong>go</strong> ina mamlaka gani<br />

Mheshimiwa Spika, mabilioni ya fedha yanapotea kuwalipa wafanyakazi hewa na uliahidi<br />

litafanyika zoezi la kuwatambua wafanyakazi hewa wote na mpaka hii leo zoezi hilo halijafanyika.<br />

Sijui Mheshimiwa Waziri anaelewa kuwa kukawia kwa zoezi hili kunasababisha mabilioni ya fedha<br />

yazidi kupotea Namwomba Waziri katika majumuisho aniambie ni lini zoezi hili litafanyika<br />

Mheshimiwa Spika, napongeza sana kukamilishwa kwa Sera, Sheria na Kanuni za Ubia kati<br />

ya Serikali na Sekta Binafsi (PPP). Muhimu tuelewe Miradi IPTL, Richmond/Dowans ni sehemu ya<br />

PPP na Taifa limepata hasara kubwa. Pia ni muhimu tuwe na Watendaji waadilifu na makini ili<br />

kunufaika na PPP.<br />

Mheshimiwa Spika, huduma za TRA zina usumbufu mkubwa sana. Pamoja na kuwa system<br />

au mtandao, lakini usumbufu umezidi kuliko pale mwanzo walipokuwa wanatumia manual. Leo hii<br />

kila wakati unaambiwa system iko down; haieleweki kwa nini kila siku system inakuwa down.<br />

Mheshimiwa Spika, baada ya kulipa ushuru, kuna usumbufu mwingine wa kupata<br />

Released Order. Ukifika kwenye huduma hii, huyo Afisa wa TRA, kumtoa ofisini kwenda kukagua<br />

mzi<strong>go</strong> wako inabidi umwombe na huchukua siku mbili ndiyo anakwenda kukagua ule mzi<strong>go</strong> wako<br />

na akirudi kukagua huchukua siku mbili kupata Released Order nyingine kwa kisingizio mtandao<br />

unasumbua.<br />

50

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!