Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
turejee salama. Vile vile pia na kwa wasafiri wote ambao wanasafiri kwa vyombo mbalimbali<br />
Mwenyezi Mungu aweze kuwajalia safari njema. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, mimi nina kero moja kubwa sana inayohusiana na kodi. Nina mambo<br />
mengi ya kuzungumza lakini ninaomba nianzie kwanza na hili. Tunalotaka kulizungumza hasa ni<br />
kuhusiana na ukwepaji wa kodi. Kama kuna maeneo tunaibiwa kodi za ndani ni katika hili eneo la<br />
utoaji wa risiti pungufu au kutokutoa risiti kabisa. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, tunaibiwa sana na wafanyabiashara wado<strong>go</strong> na wakubwa. Hili ni<br />
eneo ambalo inabidi Serikali liangalie kwa umakini sana sana. Lakini kibaya zaidi ni kwamba<br />
utakuta Dar es Salaam ndio eneo kubwa sana ambalo tunalitegemea, lakini Dar es Salaam ndipo<br />
mahali ambapo pamekuwa kichochoro kikubwa sana kwa kutokutoa risiti.<br />
Mheshimiwa Spika, wafanyabiashara wengi Mikoani takribani asilimia 80 hivi wanapata<br />
bidhaa zao kutoka Dar es Salaam. Lakini cha kushangaza ukijaribu kwenda Kibaha pale kwenye<br />
mizani utakuta kwamba takribani asilimia 70 ya risiti zile zinazotolewa za kusindikiza mzi<strong>go</strong> ziko<br />
under valued. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, huu ni wizi mkubwa sana lakini tatizo siyo kwa hawa wanaonunua zile<br />
bidhaa tatizo ni kwa wale wauzaji kule Dar es Saalam. Kwa sababu wengi wanapokuwa<br />
wakinunua zile bidhaa wanataka wapewe risiti kulingana na risiti na kulingana thamani ya bidhaa<br />
zao lakini wale wauzaji (wafanyabiashara) kule Dar es Salaam wanakataa na wanawatishia<br />
wanasema kwamba mkikataa wengine watakuja na watanunua bidhaa hizi. Kwa hiyo, inabidi<br />
wanunue tu hivyo.<br />
Lakini tatizo linakuja pale mfanyabiashara yule anapofika kule Mkoani anapotaka sasa<br />
kuthaminisha bidhaa yake inakuwa ni ngumu haiwezekani kuiweka katika mahesabu thamani<br />
halisi ya biashara ile haipatikani. Huu ndio mwanzo sasa wa ukwepaji wa kodi kwa sababu itabidi<br />
na hata yeye kule Mkoani atumie njia hii hii ya ukwepaji wa kutoa risiti au kutoa risiti yenye thamani<br />
pungufu. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kwa kweli dhamana ambayo tumeipa TRA ni kubwa na wanajitahidi<br />
sana. Lakini kama wananchi hatutashiriki katika kudhibiti huu ukwepaji wa kodi kwa kweli kazi<br />
itawawia ngumu kwa sababu wao ni wachache, wafanyabiashara hapa nchini ni wengi na<br />
watumiaji wa bidhaa nchini ni wengi kwa hiyo, ni vema Watanzania wote tukashiriki katika hili<br />
suala.<br />
Mheshimiwa Spika, TRA, wamekuwa na mikakati mbalimbali ya kusaidia kuboresha<br />
makusanyo, kuboresha ukusanyaji wa kodi. Mfano mmojawapo tunaona kwa sasa hivi<br />
wameanzisha kutumia electronic physical devise kwa ajili ya kuhakikisha kwamba risiti zinatolewa.<br />
Lakini hata hivyo wafanyabiashara waweze kuweka kumbukumbu zao vizuri na hii device<br />
imeunganishwa na mtandao wa TRA.<br />
Lakini cha kushangaza ni kwamba pamoja na hizi device utakuta wafanyabiashara wengi<br />
wanadai kwamba ni mbovu mara nyingine, lakini hata wateja wenyewe mara nyingi huwa<br />
hawana tabia ya kuomba risiti. Kwa hiyo, unakuta hazifanyi kazi iliyokusudiwa. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, mimi ningependa nitoe mifano michache ambayo ni ushuhuda wangu<br />
mimi mwenyewe niliokutana nao kwa kuzingatia hili suala la ukwepaji wa kodi ni maeneo mengi<br />
sana ambayo nimekuwa nikikutana nayo. Lakini hii ni michache tu ambayo nitaitolea mifano.<br />
Eneo la kwanza ni katika Vituo vya Mafuta. Mara nyingi ninapokuwa nikijaza mafuta katika<br />
vituo vya mafuta ni lazima niombe risiti ndio nipewe, ni vituo vichache sana vya mafuta ambavyo<br />
huwa vinatoa risiti. Ninapokuwa nikiomba risiti huwa natumia lugha moja ni kwa nini huwa hamtoi<br />
risiti Sasa majibu mara nyingi huwa ni matatu si Dar es Salaam, si Dodoma si wapi majibu yake la<br />
kwanza wanasema wengi huwa hawapendi kuchukua risiti.<br />
20