28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

turejee salama. Vile vile pia na kwa wasafiri wote ambao wanasafiri kwa vyombo mbalimbali<br />

Mwenyezi Mungu aweze kuwajalia safari njema. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, mimi nina kero moja kubwa sana inayohusiana na kodi. Nina mambo<br />

mengi ya kuzungumza lakini ninaomba nianzie kwanza na hili. Tunalotaka kulizungumza hasa ni<br />

kuhusiana na ukwepaji wa kodi. Kama kuna maeneo tunaibiwa kodi za ndani ni katika hili eneo la<br />

utoaji wa risiti pungufu au kutokutoa risiti kabisa. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, tunaibiwa sana na wafanyabiashara wado<strong>go</strong> na wakubwa. Hili ni<br />

eneo ambalo inabidi Serikali liangalie kwa umakini sana sana. Lakini kibaya zaidi ni kwamba<br />

utakuta Dar es Salaam ndio eneo kubwa sana ambalo tunalitegemea, lakini Dar es Salaam ndipo<br />

mahali ambapo pamekuwa kichochoro kikubwa sana kwa kutokutoa risiti.<br />

Mheshimiwa Spika, wafanyabiashara wengi Mikoani takribani asilimia 80 hivi wanapata<br />

bidhaa zao kutoka Dar es Salaam. Lakini cha kushangaza ukijaribu kwenda Kibaha pale kwenye<br />

mizani utakuta kwamba takribani asilimia 70 ya risiti zile zinazotolewa za kusindikiza mzi<strong>go</strong> ziko<br />

under valued. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, huu ni wizi mkubwa sana lakini tatizo siyo kwa hawa wanaonunua zile<br />

bidhaa tatizo ni kwa wale wauzaji kule Dar es Saalam. Kwa sababu wengi wanapokuwa<br />

wakinunua zile bidhaa wanataka wapewe risiti kulingana na risiti na kulingana thamani ya bidhaa<br />

zao lakini wale wauzaji (wafanyabiashara) kule Dar es Salaam wanakataa na wanawatishia<br />

wanasema kwamba mkikataa wengine watakuja na watanunua bidhaa hizi. Kwa hiyo, inabidi<br />

wanunue tu hivyo.<br />

Lakini tatizo linakuja pale mfanyabiashara yule anapofika kule Mkoani anapotaka sasa<br />

kuthaminisha bidhaa yake inakuwa ni ngumu haiwezekani kuiweka katika mahesabu thamani<br />

halisi ya biashara ile haipatikani. Huu ndio mwanzo sasa wa ukwepaji wa kodi kwa sababu itabidi<br />

na hata yeye kule Mkoani atumie njia hii hii ya ukwepaji wa kutoa risiti au kutoa risiti yenye thamani<br />

pungufu. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kwa kweli dhamana ambayo tumeipa TRA ni kubwa na wanajitahidi<br />

sana. Lakini kama wananchi hatutashiriki katika kudhibiti huu ukwepaji wa kodi kwa kweli kazi<br />

itawawia ngumu kwa sababu wao ni wachache, wafanyabiashara hapa nchini ni wengi na<br />

watumiaji wa bidhaa nchini ni wengi kwa hiyo, ni vema Watanzania wote tukashiriki katika hili<br />

suala.<br />

Mheshimiwa Spika, TRA, wamekuwa na mikakati mbalimbali ya kusaidia kuboresha<br />

makusanyo, kuboresha ukusanyaji wa kodi. Mfano mmojawapo tunaona kwa sasa hivi<br />

wameanzisha kutumia electronic physical devise kwa ajili ya kuhakikisha kwamba risiti zinatolewa.<br />

Lakini hata hivyo wafanyabiashara waweze kuweka kumbukumbu zao vizuri na hii device<br />

imeunganishwa na mtandao wa TRA.<br />

Lakini cha kushangaza ni kwamba pamoja na hizi device utakuta wafanyabiashara wengi<br />

wanadai kwamba ni mbovu mara nyingine, lakini hata wateja wenyewe mara nyingi huwa<br />

hawana tabia ya kuomba risiti. Kwa hiyo, unakuta hazifanyi kazi iliyokusudiwa. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, mimi ningependa nitoe mifano michache ambayo ni ushuhuda wangu<br />

mimi mwenyewe niliokutana nao kwa kuzingatia hili suala la ukwepaji wa kodi ni maeneo mengi<br />

sana ambayo nimekuwa nikikutana nayo. Lakini hii ni michache tu ambayo nitaitolea mifano.<br />

Eneo la kwanza ni katika Vituo vya Mafuta. Mara nyingi ninapokuwa nikijaza mafuta katika<br />

vituo vya mafuta ni lazima niombe risiti ndio nipewe, ni vituo vichache sana vya mafuta ambavyo<br />

huwa vinatoa risiti. Ninapokuwa nikiomba risiti huwa natumia lugha moja ni kwa nini huwa hamtoi<br />

risiti Sasa majibu mara nyingi huwa ni matatu si Dar es Salaam, si Dodoma si wapi majibu yake la<br />

kwanza wanasema wengi huwa hawapendi kuchukua risiti.<br />

20

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!