Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
kuanzisha Mji mdo<strong>go</strong> wa Madaba. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri je, ni hatua gani sasa<br />
imefikiwa katika kuanzishwa huo Mji Mdo<strong>go</strong> wa Madaba<br />
WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kumpongeza<br />
dada yangu Mheshimiwa Jenista Mhagama M<strong>bunge</strong> wa Peramiho, kwa jinsi anavyofuatilia kwa<br />
ukaribu sana kupatikana kwa Mji wa Madaba. Nadhani kila fursa anayoipata hapa ndani<br />
anazungumzia Mji Mdo<strong>go</strong> wa Madaba. Niseme kwamba baada ya kusikia kilio cha Mheshimiwa<br />
M<strong>bunge</strong> wakati tunajadili Bajeti ya Waziri Mkuu, Ofisi yangu inatuma wataalam kwenda Itigi kule<br />
Manyoni ambako umeombwa Mji Mdo<strong>go</strong> pamoja na Madaba ili kazi hiyo ya mipaka na nini<br />
lazima ifanyike ili muda muafaka ukifika tutaifanya Madaba kupata hadhi ya Mamlaka ya Mji<br />
Mdo<strong>go</strong>.<br />
Na. 494<br />
Fedha Zinazopatikana kwa Kuweka Mlio wa Wimbo<br />
Kwenye Simu ya Mkononi<br />
MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:-<br />
Simu za mkononi zinatumia baadhi ya milio ya nyimbo za wasanii wetu na pindi mtu<br />
anapopiga simu anaambiwa abonyeze alama ya nyota kwenye simu yake ili achague wimbo<br />
anaoutaka uingizwe kwenye simu yake lakini anakatwa kiasi fulani cha pesa:-<br />
(a)<br />
makato hayo<br />
(b)<br />
Je, Serikali katika makato hayo inafahamu ni kiasi gani wasanii wanafaidika na<br />
Je, Serikali inapata kiasi gani cha kodi kwenye makato hayo<br />
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-<br />
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, M<strong>bunge</strong> wa<br />
Namtumbo lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-<br />
(a) Mheshimiwa Spika, Makampuni ya Simu nchini hununua nyimbo za wasanii kutoka<br />
makampuni yanayosambaza kazi za wasanii hao. Hivyo, Makampuni ya Simu hulipa gharama<br />
zinazotokana na tozo hizo kwa makampuni yaliyopewa haki ya kununua na kuuza kazi za wasanii.<br />
Hata hivyo, napenda kumfahamisha Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> kwa kuwa Wizara yangu inawasiliana<br />
na Wizara ya Habari, Vijana na Utamaduni na Michezo ambayo inaratibu shughuli za haki miliki za<br />
wasanii nchini ili kuweza kufahamu kwa kiasi gani wasanii wanafaidika kutokana na nyimbo zao<br />
kutumika katika simu za mkononi.<br />
(b) Mheshimiwa Spika, mapato yanayokusanywa na Makampuni ya Simu kutokana<br />
na watumiaji wa simu za mkononi kuingiza nyimbo katika simu zao ni sehemu ya mapato<br />
yanayotokana na huduma zingine kama vile za kupiga simu, kutuma ujumbe mfupi wa maneno<br />
na huduma za intaneti ambayo yote kwa pamoja hutengeneza mapato ya jumla ya Makampuni<br />
hayo ya Simu ambapo Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato (TRA) hukusanya mapato hayo<br />
kulingana na viwan<strong>go</strong> vya kodi ya mapato kwa wakati husika.<br />
MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza<br />
maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa kwa sasa kila huduma katika simu za mkononi hukatwa<br />
fedha ni zaidi ya hizi alizozitaja Mheshimiwa Naibu Waziri. Je, Serikali ina mechanism ya kutosha ya<br />
kutambua makato yote yanayokatwa na Makampuni haya ya Simu ili kuweza kukatwa kodi na<br />
kujazia katika Mfuko Mkuu wa Serikali<br />
Pili, kwa kuwa biashara hii ya simu za mkononi ina wateja wasiopungua milioni 16 na kama<br />
Serikali inao uwezo huo wa kutambua hizo transactions zote na je, inaweza kuja kila baada ya<br />
miezi mitatu kutwambia imekusanya kiasi gani cha fedha<br />
8