28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

kuanzisha Mji mdo<strong>go</strong> wa Madaba. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri je, ni hatua gani sasa<br />

imefikiwa katika kuanzishwa huo Mji Mdo<strong>go</strong> wa Madaba<br />

WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kumpongeza<br />

dada yangu Mheshimiwa Jenista Mhagama M<strong>bunge</strong> wa Peramiho, kwa jinsi anavyofuatilia kwa<br />

ukaribu sana kupatikana kwa Mji wa Madaba. Nadhani kila fursa anayoipata hapa ndani<br />

anazungumzia Mji Mdo<strong>go</strong> wa Madaba. Niseme kwamba baada ya kusikia kilio cha Mheshimiwa<br />

M<strong>bunge</strong> wakati tunajadili Bajeti ya Waziri Mkuu, Ofisi yangu inatuma wataalam kwenda Itigi kule<br />

Manyoni ambako umeombwa Mji Mdo<strong>go</strong> pamoja na Madaba ili kazi hiyo ya mipaka na nini<br />

lazima ifanyike ili muda muafaka ukifika tutaifanya Madaba kupata hadhi ya Mamlaka ya Mji<br />

Mdo<strong>go</strong>.<br />

Na. 494<br />

Fedha Zinazopatikana kwa Kuweka Mlio wa Wimbo<br />

Kwenye Simu ya Mkononi<br />

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:-<br />

Simu za mkononi zinatumia baadhi ya milio ya nyimbo za wasanii wetu na pindi mtu<br />

anapopiga simu anaambiwa abonyeze alama ya nyota kwenye simu yake ili achague wimbo<br />

anaoutaka uingizwe kwenye simu yake lakini anakatwa kiasi fulani cha pesa:-<br />

(a)<br />

makato hayo<br />

(b)<br />

Je, Serikali katika makato hayo inafahamu ni kiasi gani wasanii wanafaidika na<br />

Je, Serikali inapata kiasi gani cha kodi kwenye makato hayo<br />

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-<br />

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, M<strong>bunge</strong> wa<br />

Namtumbo lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-<br />

(a) Mheshimiwa Spika, Makampuni ya Simu nchini hununua nyimbo za wasanii kutoka<br />

makampuni yanayosambaza kazi za wasanii hao. Hivyo, Makampuni ya Simu hulipa gharama<br />

zinazotokana na tozo hizo kwa makampuni yaliyopewa haki ya kununua na kuuza kazi za wasanii.<br />

Hata hivyo, napenda kumfahamisha Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> kwa kuwa Wizara yangu inawasiliana<br />

na Wizara ya Habari, Vijana na Utamaduni na Michezo ambayo inaratibu shughuli za haki miliki za<br />

wasanii nchini ili kuweza kufahamu kwa kiasi gani wasanii wanafaidika kutokana na nyimbo zao<br />

kutumika katika simu za mkononi.<br />

(b) Mheshimiwa Spika, mapato yanayokusanywa na Makampuni ya Simu kutokana<br />

na watumiaji wa simu za mkononi kuingiza nyimbo katika simu zao ni sehemu ya mapato<br />

yanayotokana na huduma zingine kama vile za kupiga simu, kutuma ujumbe mfupi wa maneno<br />

na huduma za intaneti ambayo yote kwa pamoja hutengeneza mapato ya jumla ya Makampuni<br />

hayo ya Simu ambapo Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato (TRA) hukusanya mapato hayo<br />

kulingana na viwan<strong>go</strong> vya kodi ya mapato kwa wakati husika.<br />

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza<br />

maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa kwa sasa kila huduma katika simu za mkononi hukatwa<br />

fedha ni zaidi ya hizi alizozitaja Mheshimiwa Naibu Waziri. Je, Serikali ina mechanism ya kutosha ya<br />

kutambua makato yote yanayokatwa na Makampuni haya ya Simu ili kuweza kukatwa kodi na<br />

kujazia katika Mfuko Mkuu wa Serikali<br />

Pili, kwa kuwa biashara hii ya simu za mkononi ina wateja wasiopungua milioni 16 na kama<br />

Serikali inao uwezo huo wa kutambua hizo transactions zote na je, inaweza kuja kila baada ya<br />

miezi mitatu kutwambia imekusanya kiasi gani cha fedha<br />

8

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!