28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

wakati pamoja na kurekebishiwa mishahara yao. Nitashukuru endapo Serikali itapokea maombi<br />

yangu.<br />

Mheshimiwa Spika, tano, malipo ya Mirathi. Vile vile kuna matatizo makubwa sana ya<br />

Wasimamizi wa mirathi kupata malipo kwa muda mfupi. Kwani kumekuwa na ucheleweshaji usio<br />

na msingi wakati walengwa wa mirathi hiyo wakiwemo watoto wakiendelea kupata shida.<br />

Naiomba Serikali ni lini ucheleweshaji huu utakwisha na huduma hii pia kutolewa Mikoani katika<br />

Hazina Ndo<strong>go</strong> kwa asilimia mia.<br />

Mheshimiwa Spika, sita, gharama ya kununua magari ya Wa<strong>bunge</strong> kuwa kubwa.<br />

Napenda kuijulisha Serikali kuwa fedha walizopewa Wa<strong>bunge</strong> za mkopo wa kununua magari ya<br />

kufanyia kazi za U<strong>bunge</strong> zimekuwa ndo<strong>go</strong> kulingana na magari bei kuwa kubwa. Hivyo, magari<br />

aina ya Mkonga yananunuliwa kwa Shilingi Milioni tisini, hapo bado gharama ya kulipa ushuru<br />

bandarini hujalipa pamoja na Serikali kuchangia gharama hiyo yaani Exemption.<br />

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali kuangalia upya namna ya kusaidia tatizo hili kwani<br />

wako Wa<strong>bunge</strong> wengi ambao magari yao yapo bandarini wameshindwa kuya<strong>go</strong>mboa.<br />

Namwomba Mheshimiwa Mkulo Waziri mwenye dhamana atoe majibu ili kuwanusuru<br />

Wa<strong>bunge</strong>.<br />

Mheshimiwa Spika, mwisho, napenda kumalizia mchan<strong>go</strong> wangu ambao nategemea<br />

Serikali itaungana nami. Hivyo basi, naunga mkono hoja na nawatakia utekelezaji wenye tija kwa<br />

Watanzania.<br />

MHE. DKT. WILLIAM A. MGIMWA: Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kumpongeza<br />

Mheshimiwa Waziri yeye binafsi pamoja na Manaibu Waziri wa Fedha kwa kazi yao nzuri. Baada<br />

ya utangulizi huo naomba sasa nichangie kama ifuatavyo:-<br />

Kwanza, Mifuko ya Mashirika ya Umma (Social Security Funds). Hotuba inaonesha<br />

kwamba Mifuko hii imekuwa ikikusanya michan<strong>go</strong> ya wanachama na kulipa wastaafu<br />

wanachama wa Mifuko hii vizuri. Hata hivyo, Bunge tunahitaji kupata ufafanuzi wa utendaji wa<br />

Mifuko hii katika maeneo nyeti yafuatayo:-<br />

(1) Ukwasi wake (Liquidity of the Social Security funds).<br />

(2) Uwekezaji (Investments).<br />

(3) Risk Management reports.<br />

Mheshimiwa Spika, taarifa hizo (1), (2) na (3) zitaliwezesha Bunge kuelewa kiwan<strong>go</strong> cha<br />

usalama wa Mifuko hii na uwezo ziada (excess financial capacity) kuendelea kutoa huduma<br />

zinazohitajika.<br />

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri anaombwa kutufafanulia mambo haya.<br />

Mheshimiwa Spika, ni changamoto ya kuongeza mapato ya Serikali. Mheshimiwa Waziri<br />

amebaini kuwepo kwa changamoto hiyo hapo juu lakini hakuna maelezo ya mikakati ya<br />

kukabiliana na changamoto hiyo. Nionavyo mimi ili kuikabili changamoto hiyo, yafuatayo lazima<br />

yafuatwe au yazingatiwe:-<br />

Kwanza, uhakika wa umeme. Bila uhakika wa kuwa na umeme au kuendelea kuwa na<br />

mgao wa umeme kutasababisha uzalishaji viwandani ushuke sana au usiwepo kabisa na hivyo<br />

Serikali kukosa mapato. Serikali inashauriwa kuharakisha kutatua tatizo hili kama Wizara ya Nishati<br />

ilivyoahidi.<br />

42

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!