28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mheshimiwa Spika, nadhani suala la vyanzo vya mapato ni muhimu sana kuliangalia. La<br />

pili, ni kwamba napata tatizo sana na shilingi yetu ya Tanzania inavyomomoyoka. Thamani yake<br />

inavyoshuka siku hadi siku. Ni jambo mojawapo la kusikitisha sana. Mimi hua nasikitika kwa<br />

sababu taarifa tunazopata ni kwamba dhahabu yetu inapanda bei katika soko la ulimwengu.<br />

Inapanda vizuri tu siku hadi siku. Sasa mimi siyo mchumi. Lakini wako wachumi hapa. Hivi ni kwa<br />

kiasi gani dhahabu hii inaweza ikasaidia shilingi yetu ya Tanzania isiendelee kushuka thamani.<br />

Hakuna mchan<strong>go</strong> wowote wa dhahabu hii ambayo inapanda siku hadi siku thamani yake<br />

ikasaidia kupunguza tatizo hili la kushuka thamani kwa shilingi yetu ya Tanzania (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika u<strong>go</strong>mvi mwingine ambao tunaupata ni kwa sababu ya kushuka kwa<br />

thamani yetu ya shilingi. Kwa sababu juzi Serikali ilifanya kazi nzuri ikapunguza bei ya mafuta.<br />

Lakini hata siku tatu nne hazijafika tukarudi kule kule kwenye bei zile za zamani za mafuta. Na<br />

sababu iliyoelezwa ni kwamba shilingi yetu imeendelea kuoungua na kwa sababu wenzetu hawa<br />

wananunua mafuta kwa dola na kadhalika.<br />

Sasa tuna jitihada gani basi sasa ya kuilinda hii shilingi yetu. Mimi nadhani Mheshimiwa<br />

Waziri pamoja na Gavana wa Benki Kuu ipo haja kubwa sana ya kuangalia nana ya kuisitiri hii<br />

shilingi yetu ya Tanzania ili kusudi maisha bora kwa kila Mtanzania yanaweza yakapatikana. Kama<br />

shilingi yetu itaendelea kupanda siku hadi siku kama inavyofanya sasa kwa kweli hata hayo<br />

maisha bora kwa kila Mtanzania ni vigumu sana kupatikana.<br />

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ombi langu au ningenda Mheshimiwa Waziri anisaidie<br />

baadaye ni kwa kiasi kupata kwa bei ya dhahabu na madini mengine yana mchan<strong>go</strong> katika<br />

kusaidia mmomonyoko huu au kudon<strong>go</strong>ka hii thamani yetu ya shilingi ya Tanzania. Pili, mimi sina<br />

uhakika kama usimamizi wetu katika masuala ya money laundry na Bureau de Change uko<br />

perfect, sina hakika. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, huko ni katika baadhi ya maeneo ambapo fedha za nchi za nje<br />

zinapotea sana. Tunahitajni kila dola moja, dola mbili, dola tatu au kila aina ya fedha zetu za<br />

kigeni ili tuweze kijikimu katika mambo yetu mbalimbali. Lakini katika mambo haya mawili ni kweli<br />

tuna soko huria tumeanzisha haya mambo ya Bureau de Change sina uhakika kama usimamizi<br />

uko wa kweli kweli wa dhati kabisa kutoka Benki Kuu na Wizara katika kuona kwamba<br />

hatudanganywi danganywi na hatuibiwi. Hisia za walio wengi ni kwamba tunaibiwa sana katika<br />

hizi Bureau de change ndio hiosia za watu wengi.<br />

Sasa naomba na Serikali na hili nalo hebu waliangalie na waturidhishe kweli usimamizi uko<br />

mzuri, hatudanywi, hatuibiwi Nitashukuru sana kupata maelezo. Lakini katika money laundry<br />

pia pamoja na Sheria imepita hivi lakini nina wasi wasi kwamba ziko fedha nyingi ambazo<br />

hazieleweki, hazitozwi kodi, zinasambaa ndani ya nchi. Kwa ajili hiyo nchi inapata matatizo.<br />

Mheshimiwa Spika, baada ya hapo nizungumzie suala la pensheni. Penseheni ni muhimu<br />

kwa wananchi wetu. Huko nyuma nadhani suala la pensheni halikuangaliwa vizuri. Ndiyo maana<br />

watu waliostaafu kwa kweli maisha yao ni dhalili sana, duni sana. Kama anakumbuka sawa sawa<br />

juzi juzi tulikuwa tunasoma gazeti hapa Katibu Mkuu wetu Mstaafu, Mheshimiwa Philip Mangula,<br />

alipokuwa anajibu baadhi ya tuhuma hapa, anasema anaishi kwa pensheni yake ni shilingi laki<br />

moja na thelani. Hivi laki moja na thelani kweli kwa mtu kama yeye atafanyaje.<br />

Lakini hata kwa siku za nyuma mlimsikia Generali Sarakikiya naye akilalamika hivyo hivyo<br />

kwamba kipensheni kile anachopata ni kido<strong>go</strong> sana.<br />

Mheshimiwa Spika, ni vizuri sana tukawa tunaangalia namna ya kuboresha pensheni zetu<br />

hizi. Kwa sababu pensheni ikiboreka na watu wakawa na uhakika kama pensheni zao zitakuwa<br />

nzuri mtu hatapenda kuingia kwenye vishawishi. Wakati mwingine watu wanalazimika kuingia<br />

kwenye vishawishi vya kufanya mambo ya ovyo ovyo kwa sababu anajua kesho na kesho kutwa<br />

huko hajui maisha yake yatakuwa namna gani. Hajui, anasema bora nichukue changu mapema<br />

ili kusudi huko mbele ya safari na mimi niweze kuishi kama wengine.<br />

26

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!