28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

gharama ya LPG yenyewe kwa sababu gesi sisi tunayo. Lakini ni lazima tuwe na uzalishaji wa hiyo<br />

LPG.<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuanzisha kituo cha kuzalisha kuweka kwenye magari<br />

nakubaliana na wewe. Tumesema humu ndani kwamba, ni lazima kuwe na vituo zaidi, huwezi<br />

mtu ukawa uko Mbagala kituo ni kimoja tu, mpaka uje Ubun<strong>go</strong>, ujaze urudi tena Mbagala, tukiwa<br />

na vituo kama sita au saba Dar es Salaam inaweza ikasaidia tunalifanyia kazi lakini pia na wingi<br />

wa magari uwepo. Sasa hivi kuna magari machache mno kwa kuwa na vituo kama nane au tisa.<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la mgawo wa umeme…<br />

SPIKA: Mheshimiwa Waziri pamoja na Muhimbili Hospitali, Dar es Salaam kutokuwa na<br />

umeme hivi sasa. Muhimbili hakuna umeme hakuna maji, jibu kwa pamoja.<br />

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, wakati tulipokuja hapa wiki<br />

iliyopita tatizo lilikuwa kwenye upatikanaji wa gesi Dar es Salaam na upatikanaji wa mafuta. Sasa<br />

hivi tumejiwekea utaratibu ambapo tunapata taarifa za mara kwa mara kwa kila asubuhi kuhusu<br />

nini kinachoendelea.<br />

Mheshimiwa Spika, kulingana na yale yaliyopatikana leo asubuhi, tunajua kwamba jana<br />

tulikuwa na matatizo grid ilitoka kido<strong>go</strong> usiku na kwa maana hiyo maeneo mengi yaliingia kwenye<br />

giza na baada ya mafundi wa TANESCO waliporudisha grid ndani ya dakika 45, maeneo mengine<br />

bado yakabaki chini. Kuhusu suala la Muhimbili naomba nikalifuatilie kwa sababu kwa upande wa<br />

Dar es Salaam mgawo uliokuwepo jana ulikuwa ni wa megawati 150 na ukiwa na mgawo wa<br />

megawati 150 kwa utaratibu wa kugawa kwenye maeneo maalum ya Dar es Salaam Muhimbili<br />

haiwezi kukosa umeme. Kwa maana hiyo, kwa umeme kido<strong>go</strong> utakaokuwepo ni lazima Muhimbili<br />

na maeneo mengine kama hospitali za Temeke ni lazima zipate umeme ndiyo utaratibu<br />

tuliojiwekea. Kama umeme hakuna Muhimbili ina maana kuna tatizo lingine lakini siyo la uzalishaji.<br />

Mheshimiwa Spika, naomba nirejee na tutajua tatizo hilo na tutalitolea taarifa.<br />

SPIKA: Ahsante, Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> maswali yamekwisha. Muda hautoshi kabisa na<br />

Wizara inayokuja ina wachangiaji wachache na inabidi tumalize leo kwa hiyo naendelea.<br />

Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> tuna wageni waliopo hapa.<br />

MBUNGE FULANI: Taarifa<br />

SPIKA: Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> naomba ukae, wageni waliofika Bungeni kwa ajili ya<br />

mafunzo ni wanafunzi 50 kutoka shule ya Sekondari ya Viwandani, wapo wapi wasimame walipo,<br />

ahsanteni, karibuni sana na msome kwa bidii. Tuna wanafunzi 25 wa Kidato cha Nne kutoka shule<br />

ya Star Evening Class programme Dodoma wengine walikuja jana na wengine wamekuja leo,<br />

wasimame mahali walipo, ahsanteni sana, msome kwa bidii hata kama ni evening programme.<br />

Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> tunao vion<strong>go</strong>zi 20 wa Wanawake wa Kanisa la Biblia, eneo la<br />

Dodoma wapo wapi wasimame, ahsanteni sana na tunawashukuru sana. Tunao wanafunzi 50 na<br />

Walimu wao kutoka shule ya sekondari ya Ng’ong’ona, Dodoma, karibuni sana. Tuna wanafunzi<br />

sita kutoka shule ya msingi Ubembeni, Kondoa wakifuatana na Walimu wao naomba wasimame,<br />

ahsanteni, karibuni sana na msome kwa bidii. Wageni wengine walitambulishwa jana.<br />

Mheshimiwa John Mnyika, Katibu wa Wa<strong>bunge</strong> wa CHADEMA, anawatangazia Wa<strong>bunge</strong><br />

wa CHADEMA kwamba, saa saba na robo mchana leo kutakuwa na kikao chao katika ofisi ya<br />

Kion<strong>go</strong>zi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.<br />

Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> ofisi inatangaza kwamba kuna nyaraka muhimu zifuatazo<br />

zitagawiwa kwa Wa<strong>bunge</strong> wote. Hizi ni Taarifa za utekelezaji wa ahadi za Serikali Bungeni kwa<br />

kipindi cha mwaka 2010/2011, halafu kuna taarifa ya Haki za Binadamu kwa mwaka 2010, The<br />

16

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!