17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

MASWALI:<br />

<strong>Al</strong> Akh Nusra: Sayyid tulikuwa na mushkil juu ya walimu na<br />

mashekh wako wa kwanza walokusomesha.<br />

Jawabu: Nilipelekwa chuoni kwa Sayyid Shekhe baba ake Sayyid<br />

Hassan Shekh na alikuwa bibi msomeshaji mkubwa huko ni mwana Aisha,<br />

wakimwita Mwana Ashati, nikisoma Qur an huko halafu baada ya kuhitimu<br />

nikawa nasomesha huko huko chuoni. Mwisho nikaenda kwa chuo cha<br />

Sayyied Abdul Fattah bin Ahmad ndugu yake Sayyid Abal Hassan nikawa<br />

nasomesha huko na huko nilikuwa na wasaa mwingi kwa sababu niliachiwa<br />

chuo jioni yote ningekuwa nayo mimi nikiendesha. Wakati huo huo kila<br />

baina Magharib na Ishaa ninakwenda msikitini, nilimuogopa sana Shariff<br />

Aboud, wa pili Sayyid Abdul Fattah alikuwa mkali. Siku moja sikwenda<br />

Msikitini akanambia: “Baada ya leo ikiwa hukuja msikitini utaona”.<br />

Tangu siku hiyo mpaka leo ikifika Magharib na Ishaa hutafuta pahali penye<br />

Msikiti niingie kwa woga nilioupata kwa hiyo nilikwenda akanianzisha<br />

Babu baada ya Babu nikasoma Safina halafu Risala halafu Taali-mul<br />

mutaalim, Durarul bahia, Riadhal badia, Muqadimatu hadhramiya,<br />

Rubul ibada, Ghaya. Nilipofika kwenye Babu swalatu mayyit, intakal<br />

ila rahmati Lah na sikwenda kusoma kwa yeyote siku ambazo nnasoma huko<br />

illa kwa Sayyied Abal Hassan nikisoma na Nahau siku alizokuwako Unguja,<br />

kenda Pemba siku nyingi. Ikawa nakwenda kidogo kidogo sana kama<br />

natambaa lakini Taalimul-mutaallim inasema usifanye ghasia kubadilisha<br />

badilisha walimu kwa hivyo nimekaa vile vile ikiwa wale walimu<br />

wanakutosheleza bila shaka lakini Mwalimu unamuona si mwalimu<br />

wakutosheleza kwa kukuongoza ukitaka kwenda kwa mwengine akwambie<br />

aa unaambiwa huna rukhsa, rukhsa, mtu hupata mwalimu wa kweli.<br />

Halafu darasa akaichukuwa Sayyid Abal Hassan tukasoma<br />

Umdatus salik Msikitini kwa Shariff Abudu Msikiti wa Vikokotoni pale<br />

yote yanapita hapo. Kulikuwa Msikiti Vikokotoni pale tukisoma Umdatu<br />

salik hivo hivyo tukawa tunasoma kidogo kidogo sana mara anasafiri<br />

anakwenda Pemba akachume Karafuu, afanye basi hivyo hivyo, kidogo<br />

kidogo. Tukaja tukaanza na shereh ya Ghaya baada tulipomaliza Umdati<br />

salik ikawa wakati huo ikawa nakwenda Darasani kwa Sayyid bin Jafar.<br />

Ikawa nasoma kidogo kidogo bila ya darasa Mimi mwenyewe tu kama<br />

Bidaayatul hidayat katika vitabu nakumbuka nilisoma. Bidayatul hidaya<br />

nilisoma na kitabu cha Mashairi Fiqhi Zubad na darasani kwake kila<br />

asubuhi kila nikiwa sendi Skuli hapa skuli au nilipokuwa nipo<br />

16.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!