You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
MASWALI:<br />
<strong>Al</strong> Akh Nusra: Sayyid tulikuwa na mushkil juu ya walimu na<br />
mashekh wako wa kwanza walokusomesha.<br />
Jawabu: Nilipelekwa chuoni kwa Sayyid Shekhe baba ake Sayyid<br />
Hassan Shekh na alikuwa bibi msomeshaji mkubwa huko ni mwana Aisha,<br />
wakimwita Mwana Ashati, nikisoma Qur an huko halafu baada ya kuhitimu<br />
nikawa nasomesha huko huko chuoni. Mwisho nikaenda kwa chuo cha<br />
Sayyied Abdul Fattah bin Ahmad ndugu yake Sayyid Abal Hassan nikawa<br />
nasomesha huko na huko nilikuwa na wasaa mwingi kwa sababu niliachiwa<br />
chuo jioni yote ningekuwa nayo mimi nikiendesha. Wakati huo huo kila<br />
baina Magharib na Ishaa ninakwenda msikitini, nilimuogopa sana Shariff<br />
Aboud, wa pili Sayyid Abdul Fattah alikuwa mkali. Siku moja sikwenda<br />
Msikitini akanambia: “Baada ya leo ikiwa hukuja msikitini utaona”.<br />
Tangu siku hiyo mpaka leo ikifika Magharib na Ishaa hutafuta pahali penye<br />
Msikiti niingie kwa woga nilioupata kwa hiyo nilikwenda akanianzisha<br />
Babu baada ya Babu nikasoma Safina halafu Risala halafu Taali-mul<br />
mutaalim, Durarul bahia, Riadhal badia, Muqadimatu hadhramiya,<br />
Rubul ibada, Ghaya. Nilipofika kwenye Babu swalatu mayyit, intakal<br />
ila rahmati Lah na sikwenda kusoma kwa yeyote siku ambazo nnasoma huko<br />
illa kwa Sayyied Abal Hassan nikisoma na Nahau siku alizokuwako Unguja,<br />
kenda Pemba siku nyingi. Ikawa nakwenda kidogo kidogo sana kama<br />
natambaa lakini Taalimul-mutaallim inasema usifanye ghasia kubadilisha<br />
badilisha walimu kwa hivyo nimekaa vile vile ikiwa wale walimu<br />
wanakutosheleza bila shaka lakini Mwalimu unamuona si mwalimu<br />
wakutosheleza kwa kukuongoza ukitaka kwenda kwa mwengine akwambie<br />
aa unaambiwa huna rukhsa, rukhsa, mtu hupata mwalimu wa kweli.<br />
Halafu darasa akaichukuwa Sayyid Abal Hassan tukasoma<br />
Umdatus salik Msikitini kwa Shariff Abudu Msikiti wa Vikokotoni pale<br />
yote yanapita hapo. Kulikuwa Msikiti Vikokotoni pale tukisoma Umdatu<br />
salik hivo hivyo tukawa tunasoma kidogo kidogo sana mara anasafiri<br />
anakwenda Pemba akachume Karafuu, afanye basi hivyo hivyo, kidogo<br />
kidogo. Tukaja tukaanza na shereh ya Ghaya baada tulipomaliza Umdati<br />
salik ikawa wakati huo ikawa nakwenda Darasani kwa Sayyid bin Jafar.<br />
Ikawa nasoma kidogo kidogo bila ya darasa Mimi mwenyewe tu kama<br />
Bidaayatul hidayat katika vitabu nakumbuka nilisoma. Bidayatul hidaya<br />
nilisoma na kitabu cha Mashairi Fiqhi Zubad na darasani kwake kila<br />
asubuhi kila nikiwa sendi Skuli hapa skuli au nilipokuwa nipo<br />
16.