Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
vyeo kama alivyokuwa Sayyidna Abdul Qadir “Mikh-daa”?<br />
Jawabu: Wako waliofika huko, wako wasiofika, wako walofika wako<br />
wasofika bila shaka Lahum Dara-ja-tun-indal Lah.<br />
Swali (11) <strong>Al</strong> Akh Abdul Samad: Cheo cha Mikda Sayyidna Abdul<br />
Qadir katunukiwa na nani?<br />
Jawabu: Kajitahidi kafanya mujahada kapigana na Nafsi kaenda kazunguka<br />
katika majangwa miaka na miaka na miaka kaivunja Nafsi yake kaivunja kabisa<br />
hata hamna kitu. Hivyo ndio njia ya kupatia Uwalii, kuivunja Nafsi hata katika<br />
alama ya kuwa kaivunja Nafsi yake kabisa aliazimia kufunga miaka 15<br />
mfululizo. Siku ya mwisho ya kufunga miaka kumi na tano karibu na magharibi<br />
akamuona mtu - Rehmal Lahu man shariba ha-dhal ma-l. “Mwenyezi<br />
Mungu amrehemu mtu atakaekunywa maji haya” Sayyidna Abdul Qadir<br />
akasema “Nini funga yangu ya miaka 15 mbele ya dua ya mtu huyu”.<br />
Na hajapata kukutana nae lakini Nafsi yake ilivunjika Tawa-dhui isokuwa na<br />
kiasi Mungu akamnyanyua cheo kikubwa. Seyyidna Ahmad Rifa-i katika<br />
yalomnyanyua sana kulikuwa na mbwa mgonjwa na Seyyidna Ahmad Rifai<br />
bado madhehebu yake ni Shafii na Mbwa ni najisi Mughalladha kwa Shafii<br />
akamchukuwa akaenda nje ya mji akamkogesha akampa dawa na nini mpaka<br />
akapona Mwenyezi Mungu akapendezewa nae khasir Nufus.<br />
Swali (12) Akh. Abdul Samad: Katika ubeti wa Manaqib wa Seyyidna<br />
Abdul Qadir: “Wakulu Walii lahu Qadami waana Qadami Nabii badiri<br />
tamami…….”<br />
Jawabu: Haya baada ya kwisha huko juu.<br />
Swali (13) Akh. Abdul Samad; Basi amemkanyaga vipi Mtume SAW<br />
kwenye Unyayo?<br />
Jawabu: Walii, Walii, hakusema Nabii. Qadami ala raqbatil kuli Walii.<br />
Lakini wanasema Mawalii wengi kuwa hii sio iliomtafautisha Sayyidna Abdul<br />
Qadir na Mawalii wengine alikuwa juu sana kuliko hapa wako Mawalii wengine<br />
wanapata Daraja hiyo hata wanawake hii ni daraja tu Maqama basi Sayyidna<br />
Abdul Qadir yuko wapi na Mambo yalomtafautisha na Mawaliii wengine.<br />
Swali (14) Akh. Abdul Samad: Ni sahihi katika kisa cha miraji<br />
26.