Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
MASWALI:<br />
Swali (1) <strong>Al</strong> Akh. Sabri: Nafsi inakaa katika Roho au Moyo?<br />
Jawabu: Ndo wewe Nafsi, Nafsi ndo wewe.<br />
Swali (2) <strong>Al</strong> Akh. Sabri: Nataka kuelewa makaazi yeke ni<br />
wapi?<br />
Jawabu: Haina makaazi ndo wewe. Si wewe umeazimia kuja hapa leo? Basi<br />
wewe ndio Nafsi, haina pahala mahsusi na Roho ndo Nafsi yenyewe lakini<br />
inapokwenda juu sana ikatakasika ikasafika ikatulizana inaitwa Roho. Na Roho<br />
ina maana hicho kinachotupa uhai. Ina maana kadha wa kadha. Ukitafuta<br />
Roho katika mwili huiyoni na Moyo kazi yake nyengine. na Moyo wanautumia<br />
Sufia kwa maana mbili tatu. Moyo huu kama wakinga kinga na wa mwengineo<br />
na Bin Adam wake anayo hiyo hiyo- Saalal lahul afwal-afya-kuna na Moyo<br />
wanautumia hiyo Nafsi inapogeuka ikinyanyuka hali fulani wanaita Qalbi lakini<br />
hayo ndio hayo nnochotaka kuja kusema: “Nafsi ndio wewe”.<br />
Swali (3) <strong>Al</strong> Akh Marjebi: Nauliza kwamba hii nafsi inapobadilika<br />
kutoka katika Nafsil Ammaral, Nafsi Lawamma Nafsil Mulhima inakuwa<br />
ile Nafsi yenyewe au mwili unabadilika?<br />
Jawabu: Ni Nafsi. Mwili haubadiliki kitu mwili unakuwa controlled na zile<br />
Nafsi ikiwa <strong>Al</strong> Ammara, unayoipeleka katika mchezo ikiwa Lawwama<br />
unaipeleka huko mwili hauna kazi mwili na kama dubwana la mutukari lile basi<br />
ukipeleka speed kubwa ikipeleka ndogo ukipeleka huku unafaata basi<br />
unategemea uko katika hali gani.<br />
Swali (4)<strong>Al</strong> Akh Abdul Samad: Na kila Nafsi kutoka katika ile ya<br />
mwanzo mpaka hiyo ya mwisho kuna nyuradi maalumu ambazo unaweza<br />
ukafanya ziweze kubadilika?<br />
Jawabu: Naam, ukipata mlezi kama hapana walezi unapochukuwa kidogo<br />
unatoka katika hali moja katika hali ya pili iliyobaki ni kukithiri nyuradi<br />
unazopewa za Twariqa zinafanya sababu hata unageuka kutoka kwenye hali moja<br />
na kwenda kwenye hali nyengine mwanzo mwanzo hapana kama kuleta Lailaha-illaa<br />
Llahu mara nyingi kila ukiweza, njiani wapi wapi La ilaha illa<br />
Llahu ndio dawa ya watu kama sisi wenye Nafsir Ammarat bi sui mpaka<br />
atakapokwenda mbele.<br />
23.