Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
nilipokuweko hapo hapana mtu alosalisha isipokuwa mimi. Basi kwa<br />
hivyo wengi hawa Makhalifa wa Twariqal Qadiriya, furui kadha wa<br />
kadha nimekutana nao. Furui zipo nyingi za Twariqatil Qadiriya na<br />
katika hao ni Sayyid Ashekh Muhammed el fa-tih- ndo alotupenda<br />
sana Sudan, wala si mtu mzee sana . <strong>Al</strong>lah yamunnu alayhi bil a-<br />
fiya.<br />
Wao silsila yao Branch yao ni As-sammaa-ni na huyo<br />
As-sammaa-ni alikuweko Ijaz babu yake ndo alochukuwa huko na<br />
Baba yake akaja akawa Khalifa Walii Mkubwa halafu akaja akachukua<br />
yeye.<br />
Nikakutana na mwengine Khano khalafu ndo nimekuja nikajua<br />
kuwa yeye kachukuwa Twariqa kwa huyo Bwana Muhammed El<br />
Fatah khalafu kenda Baghdad kenda kukamilisha.<br />
Vile vile nimekutana na Khano mtu wa ajabu, mtu wa ajabu<br />
mwana chuoni mlezi ana watu kadha wa kadha anawalea na anavitabu<br />
katunga na hivi natawadhui kubwa nilipokwenda kumtizama kakataa<br />
kukaa juu ya kiti nikamwambia basi na mie sikai nikamwambia basi<br />
kama hukai nitamwambia mtoto akalete kiti: “Mtoto lete kiti”,<br />
kumbe halafu kamuashiria kua usilete kenda kakaa chini Ah! Mie<br />
nangojea kiti hapa mpaka tumeondoka kiti hakijaja. Tukaja<br />
tukakutana na Muridi wengi wengine watu wa Biashara wakubwa watu<br />
wa nini watu namna kwa namna.<br />
Siku moja nimekutana nae katika Baytullahil Hara-m, hata<br />
akanambia kuwa kenda Baghdadi kaambiwa kule Baghdadi kua “Kaja<br />
Umar Abdallah hapa” na Mashekhe wetu wa huku kama Sayyid Abal<br />
Hassan na wengineo na nimekutana nao Pakistani, Siria, Masri,<br />
Maghrib wapi, wapi wamejaa Masheikhe wa <strong>Al</strong> Qadiriya ndo maana<br />
nikasema: “Aja-zani ghayra wa-hidin fi Twariqatil Qadiriyya”<br />
Wa awwal man ad-khalani fi ha-dhihi da-ira mwanzo<br />
alonitia ndani ya daira hii, Huwa Seyyid Swa-fis sarira- ndani ya<br />
Roho yake ni safi <strong>Al</strong>ladhi kana lahu an twawri Nafsihi mayyil.<br />
Hamili upande wa Nafsi, Abdul Fat-tah bin Ahmad Jamali Leyl<br />
huyu ndugu yake mkubwa Sayyid Abal Hassan Mkubwa wake ndo<br />
mwanzo tangu udogoni alinichukuwa tunakwenda kwenye daira<br />
32.