You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>Al</strong> habib Seyyid Umar bin Abdallah bin Seyyid Ahmad <strong>Al</strong> Sheikh Abu<br />
Bakar bin Salim (Mwinyi Baraka ). Amezaliwa Zanzibar katika mwaka<br />
1918. Naye alikuwa ni miongoni mwa vijana walionyanyukia katika malezi<br />
kamili ya Uislamu. <strong>Al</strong>ipomaliza masomo yake ya mwanzo katika Qur an<br />
<strong>Al</strong>iendelea kuhudhuria Majaalis za jioni katika misikiti mbalimbali mjini hapo.<br />
<strong>Al</strong>ikuwa ni kijana ambaye uwezo wake katika kuhifadhi Qur an na uzingatiaji<br />
katika masomo ya skuli ulikuwa ni wakupigia mfano. Katika skuli, masomo<br />
yake ya msingi na yale ya sekondari aliyapata katika shule za kawaida za<br />
Serikali ya Zanzibar.<br />
Baada ya kufanya vyema katika masomo ya Cambridge, aliweza kuendelea<br />
katika Chuo kikuu cha Makerere Uganda. Kwa muda wa miaka mitatu<br />
alikuwepo chuoni hapo kuweza kuhitimu Shahada ya: “Diploma in Bias and<br />
Biology”. Mara baada ya kuhitimu masomo yake, alirejea Zanzibar ambapo<br />
alianza kufundisha masomo ya Dini ya Uislamu, na pia alifundisha Biology<br />
katika Vyuo Vya Waalimu Dole na Beitil El Rass.<br />
Kwenye miaka ya hamsini mwanzoni, <strong>Al</strong> Habib alienda tena kusoma<br />
London Uingereza katika School of Oriental And African Studies. Ambapo<br />
alipewa Shahada ya Diploma katika Islamic and Comperative Law. Na pia<br />
alitunukiwa Shahada ya Diploma katika Lugha ya Kiarabu. <strong>Al</strong>iporejea tena<br />
Unguja katika mwaka 1955, <strong>Al</strong> Habib aliteuliwa kushika Wadhifa mwingine<br />
tena Principal katika Muslim Academy, kuanzia mwaka 1960 – 1963. kisha<br />
alipatiwa Schoolarship kutoka Commonwealth kwenda Oxford Univesity<br />
Uingereza. Huko alifaulu vyema katika masomo yake “Comperative Religion<br />
And Philosophy”. Hapo akatunukiwa Degree ya Ph.D.<br />
<strong>Al</strong> habib Umar alikuwa ni miongoni mwa masheikh wanaotuminiwa<br />
katika kuzilea Roho/Nafsi za waumini. Ambao pia wanajulikana kuwa ni<br />
Masheikh wa Kisufi (Taswauf). Miungini mwa Masheikh zake ni pamoja na <strong>Al</strong><br />
Habib Umar Bin Abu Bakar Bin Sumeity, na pia <strong>Al</strong> Habib Ahmad Bin Hussein<br />
Bin Abu Bakar Bin Salim.<br />
Siku ya tarehe tatu March 1988, Sawa na Mwezi 17, Rajab, 1408, Mwaka<br />
wa Kiislamu ilikuwa ni siku nzito iliyojaa majonzi kwa wale wote waliokuwa<br />
wakimfahamu <strong>Al</strong> Habib Umar Bin Abdallah (Mwinyi Baraka). Kwani<br />
<strong>Al</strong>itwawafu akiwa huko katika Visiwa vya Comoro.<br />
“Tunamuomba Mwenyezi Mungu Sub hanahu Wata`ala, ainyanyue<br />
juu Roho yake, Yeye pamoja na Masheikh wote wengine, Maulamaa<br />
pamoja na watu wema wote ambao wametangulia katika Imaan”.<br />
“Amin”