You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Swali la nne: Ungetufafanulia vipi kuhusu Twarika (kinjia ya)<br />
Dhwahir na batwin, na nini hukumu ya mwenye kupinga kufaa kwake<br />
(katika Uislamu kwa Jumla)?<br />
Jawabu: Hiyo peke yake sio mambo madogo ukisema kidogo utapoteza<br />
watu<br />
Swali la tano: Ungetufafanulia vipi kuhusu swala la Mahaba kwa<br />
jumla na kuna tafauti gani kati yake na Ishq na<br />
Ishtiyaq na Wudd.<br />
Jawabu: Hilo ndo kabisa halisemeki haiwi kabisa, hayasemeki<br />
Swali la sita: Nini ufananuzi wa hizi nafsi saba (1) <strong>Al</strong> ammarat (2) <strong>Al</strong><br />
lawama (3) <strong>Al</strong> Mulhima (4) <strong>Al</strong> Mutmaina (5) <strong>Al</strong> Radhiya (6) <strong>Al</strong> Mardhia<br />
(7)<strong>Al</strong> Kamila?<br />
Jawabu: Wama-ubarriu nafsi-inna nafsa ha ammaratu bi sui…………….. Hilo<br />
kadhalika nilijaribu karibu karibuni nimeanza kushika Msikiti Jibril <strong>Al</strong> khamis<br />
baada ya kusomwa Ratibul Attas, tukiwapo Unguja. Siku moja nimesoma<br />
Nafsil ammara na sikumaliza kwa hivyo itachukua muda hata mtu azimalize<br />
nafsi hizo. Na ni maneno yenye faida sana kwa watu namna kwa namna hata<br />
wasiokuwa Waislamu. Nakumbuka nilikwenda Makerere niliitwa kutoa<br />
khutba moja juu yake sijui niliita nini lakini nilipita njia hiyo walikuwa<br />
Amerikans nani na nani. Wakastaajabu sana. Nilikuwa safari moja. Nilikuwa<br />
Malay siku zile ilikuwa Maley kabla haijaja Malaysia. Nikenda pahala<br />
nikachukuliwa pahala nikenda nikatoa khutuba nikaalikwa nikaambiwa<br />
Jumaatano wanakusanyika watu wa Dini namna kwa namna, na kila wiki anatoa<br />
mmoja katika mtu wa dini moja wapo (na siku ile ilikuwa zamu ya dini ya<br />
mkiristo) lakini kwa wewe tulivyokusikia leo unasema tutakupa fursa wewe<br />
useme. Nilikuwa katika nyumba ya Ambasidor baada ya kutoa khutba yule<br />
Ambasidor akaniambia: “Ahsante sana, Today for the first time I have<br />
Understood may religion” anasema leo kwa mara ya mwanzo nimeifahamu<br />
dini yangu mwenyewe lakini nilikuwa hata sifahamu, lakini leo ndio kwanza<br />
nimefahamu kupitia njia hizi- <strong>Al</strong> Ammara, Lawama, Mulhima, Mutmaina,<br />
Radhia, Mardhia, kamila. Jazaka llahu kheir. Mara nyingi nimepita njia hiyo<br />
kila pahala. Kidogo pana migeuzo geuzo kidogo lakini ni msingi mkubwa wa<br />
spiritualism. Spritual Development.<br />
Wafaqana Llahu lima yuhibu wa yardha.<br />
18.