ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
134<br />
yako, na ulianza kukatwa wakati tu uliajiriwa kazi. Sasa mpaka ufe tena ndio uje upewe hiyo pesa si unaona si vizuri Pengine<br />
hata watoto wanaweza kufikiria kukuua ndio waje wachukuwe hio pesa yako. Afadhali upewe hizo pesa, ndio uangalie welfare<br />
ya watoto wako ukiwa hai.<br />
Com. Ratanya: Sasa unataka review ya hiyo part ya Act hiyo ya pension<br />
Morris Gichaga: Ndio. Ya pili, sijaandika hiyo, hiyo nimeandika ni hiyo nimetaja, ya pili, ni katika vile tunaishi huku kwetu<br />
mashambani huku.<br />
Security – tunaambiwa mara kwa mara, hati wale watu wako na buduki zao, ambazo hawakuchukua kwa hari ya kawaida<br />
warudishe kwa serikali, ukirudisha, zingine unasikia zimetokea upande huyu mwingine, unakuja unapigwa unanyang’anywa mali<br />
yako, kama ni ng’ombe zinaenda, wanakuja wanachoma hata nyumba zako, sababu unaogopa kupigana na hao sababu wako<br />
na buduki. Sasa serikali haitilii maanane sana wakati unarudisha buduki, wahakikishe kila mtu amerudisha ndio watulinde, lakini<br />
wanarudisha upande mmoja na mwingine unambaki sasa kupigwa. Sasa, kama wanaona wanashidwa kututisha hizo buduki<br />
zote, waturuhusu kila nyumba ama tuseme kila village ipewe walinzi kwa sababu hata ukienda kwa chief ama kwa wapi,<br />
unaambiwa buduki hakuna hapa. Ata chief anajificha kwa msitu wakati wewe unaenda kujificha. Sasa kama ingewezekana, kila<br />
village, ipewe, wazee kama wawili watatu hivi wawe na buduki ya halali kutoka kwa serikali, walinde mali yao kwa sababu hata<br />
ukitegemea serikali sasa mali yako inaisha na hakuna mtu anakusaidia. Ni hayo tu nilikuwa nayo Bwana Commissioner. Asante<br />
sana.<br />
Com. Ratanya: Asante sana Morris kwa hayo machache yako, twende kwa Genevasi.<br />
Genevasi Kubai: Nasema asante, mimi naitwa Genevasi Kubai, maoni yangu ni juu ya ukulima. Tunataka serikali, iangalie<br />
wakulima kwa sababu saa ingine tunalima kahawa, tukipeleka huko factory, wakati pesa inakuja tunaambiwa hakuna pesa,<br />
kahawa yenu iliharibika. Saa ingine tukaambiwa mlilipwa pay out. Sasa wakulima sisi tunaumizwa, hatujui tutafanya kazi ingine<br />
wapi kwa sababu ukulima, serikali haituangalii kwenye ukulima, tunataka serikali ituangalie tukiwa wakulima. Ndio mimi<br />
nasema.<br />
Com. Ratanya: Okey asante sana, tumeshukuru, twende kwa Christine Muthau,<br />
Christine Muthau: Jina langu ni naitwa Christine Muthau, (then speaks in vernacular)<br />
Com. Ratanya: Uga riatwa riaku kiri microphone muthee wakwa .<br />
Utaje jina kwenya microphone mzee wangu,<br />
Peter N’toitharia: Naitwa Peter N’toitharia, jambo la kwanza nataka kuongea mambo ya Rais, mimi ningependelea, Rais