ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
79<br />
mambo ya mali, ningetaka serikali, isaidie watu na, tulipa pesa yeyote ya maji, tungetaka hata serikali ijengee watu hii storage<br />
tanks ya maji, ili ikikuwa ni wakati ya kiangazi, wawe wakitumia hayo maji. Lakini ningetaka hata hiyo serikali, itusaidie na<br />
kuchiba hiyo misima, ile ya chini ili watu wapate maji ya kutosha.<br />
Mambo ya Education – tungetaka education iwe free from standard one mpaka standard 8. Tungetaka iwe free na hata<br />
ikakataa kuwa free, iwe garama inagawanywa na iwe kidogo.<br />
President – President naye asiwe over law na awe kwa vipindi viwili tu.<br />
Parties – Ningetaka vyama viwe chache kwa sababu ingine watu wanatafuta tu pesa. Iko zingine hazipati hata mjumbe kwa<br />
parliament au councilor, sasa wengine wanaendelea kukaribisha hiyo vyama ili wapate pesa. Tungetaka naye kiwe kidogo.<br />
Ushirika – vyama vya ushirika, tungetaka mtu yule, kwa sababu vyama vya ushirika wengine wanakula pesa, hakuna pesa<br />
wanapunguza, tunaktaka mtu yule atakula pesa ya ushirika tena ashitakiwe, afungwe, akifungwa, akirudi, ashitakiwe tena na<br />
kama ni mali yake yauzwe.<br />
Asante sana.<br />
Com. Ratanya: Asante sana Kaberia, pengine kuna swali. Hakuna swali kwa hivyo enda usign register. Na kama una<br />
memorandum ungetaka kupeana tungeshukuru. Na anafuata ni Jeremiah Mwiti.<br />
Jeremiah Mwiti: Asante kwa viongozi ambao wako mbele yetu, na jina langu naitwa Jeremiah mwiti. Sheria kifungo ile<br />
inasimamia, Barbara tunataka ichunguzwe sana kwa maana yule mwenye kupewa kadarasi, iko mahari saa ingine anaficha ama<br />
anatua. Iko njia zamani, mzungu akiwa hapa kulikuwa na njia ya watu ya mguu, na njia ya maji, na njia ya gari. Hakuna maji<br />
iliokuwa ikienda kwa shamba la mtu halafu aende afunge. Hio sheria kama ingeolekebishwa, ama ilituwa iangaliwe sana<br />
iwekwe kwa huyu mwenye kuweka kadarasi hiyo ya barabara, hatumii vile sheria ama vile barabara inatakikana.<br />
Ya pili, President hatakiwi kuwa overall kwa maana akiwa overall anaweza kuua hata mtu akakosa kuwa huru.<br />
Com. Ratanya: Overall ni kama kusema je Unaweza ata kusema kwa Kimeru.<br />
Jeremiah Mwiti: Asiwe juu ya sheria, kwa maana anaweza kuua mtu ama kusema watu wanyongwe wote katika Kenya na<br />
hakuna mtu atamuuliza.<br />
Hii ingine, Sheria yote, ifanywe na parliament kwa maana tukisema kama sisi wameru tuko na Njurincheke, yule mkisii naye<br />
atasema ingine, huyu mwingine naye aseme ingine. Sheria itakuwa inaharibika. Wacha sheria yote tupeleke kwa parliament kwa<br />
maana tuko na wajumbe kila nchi hapo. Utadi wote uko parliament kwa maana sasa nikisema Njurincheke ndiye inafaa<br />
kufanya sheria, mkalenjin naye aseme hiyo tutaharibu sheria.<br />
Kwa Kenya yetu, tuko na President, President akiwa mwanamme, mdogo yake awe mwanamke, kwa maana naelewa