ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
42<br />
Com. Abubakar Zein: Asante sana mzee Ratanya, habari ya asubuhi Kama mlivyo ambiwa, mimi naitwa Abubakar Zein, ni<br />
commissioner kutoka tume ya kurekebisha katiba Kenya, na ningependa kuongezea kidogo tu alioyasema Mzee Ratanya ili kazi<br />
yetu iwe ya rahisi, na iwe na nidhamu. Katika kuongezea, ulipoingia hapa pale nje ulikuta kuna mtu anaadikisha majina, sio<br />
Sasa yale majina huandikwa kwa number na sisi tutafuata orodha hiyo kufuata majina na mna hiyo. Ukiitwa jina lako,<br />
unatakikana uje ukae hapa, ushike microphone, utaje jina lako kabla hujaanza kuzungumza, na ni mhimu sana wewe kutaja jina<br />
lako, kwa sababu gani Huyu binti mliojurishwa kwenu anainua mkono, kazi yake yeye ni ku-record mazungumzo yote<br />
anayozungumzwa hapa kwa tape recorder, ndio tusipoteze hata neno moja. Ndio saa ingine ukiona saa ingine hatuandiki,<br />
ukasema hatuandiki, ukasema hawa namna gani maneno nasema lakini haandiki. Kila neno tuna-record na tutaliandika chini<br />
tukishafika Nairobi wanaendelea na kazi hizo Nairobi. Na kama alivyosema Mzee Ratanya, karatisi unaotupa kila kitu<br />
tutasoma, kwa hivyo usiwe na wasi wasi kuhusu maneno mengine yatapotea. Ndio maana tuna-record hayo maneno, utaje jina<br />
lako na uzungumze ndio awe na record vizuri.<br />
Lingine la mhimu kufahamu ni kwamba, juu ya kwamba umepewa uongozo wa lugha, lakini kuna muongozo mwingine wa lugha<br />
kule kwetu Mombasa wanasema, watu wakisumza katika hadhala kama hii, kikao kama hiki, wanatakiwa watumie lugha ya<br />
muluwa, yaani lugha ambayo haitamkasirisha mtu yeyote, kama mzee yuko pale ukitumia lugha hio aone ni lugha ambayo inafaa<br />
kutumika mbele ya wazee. Kama mama yuko hapa, utumie lugha ambao inaweza kutumika mbele ya mama. Kwa hivyo ni<br />
lugha yenye heshima ambayo haitumii matusi.<br />
Kitu kingine, kwamba masungumzo unayozumza hapa, maoni unayotoa hapa wewe unalidwa kisheria, sheria hii iliounda<br />
mabadiriko ya katiba, inakulida wewe kikamirifu, hautachukuliwa hatua yeyote kwa maoni unaozungumza hapa. Kama tulienda<br />
kwingine wakasema, sasa nikisema maneno mengine, yakikasirisha mtu fulani au kasisi fulani, au chama fulani, au office fulani, si<br />
nitapata taabu Tunasema hapana, hakuna atakayekasirika, akikasirika atamezea hivo hivo tu na hasira zake lakini hakuna<br />
hatua unaweza kuchukuliwa wewe. Sijui kama tunaelewana hapo, lakini hiyo haina maana, unajua nchini kwetu tunasungumza<br />
habari ya uhuru, kama sasa huo ndio uhuru wa mwananchi kuzungumza maneno yake kwa uhuru, hio haina maana. Uhuru<br />
hauendi bila kuhajibika, au haina maana hiyo Hatutakubali mtu hapa kuja kuanza kutukana mtu mwingine, aseme mtu fulani, ni<br />
hivi na hivi, hii mambo ya kubadilisha katiba hayahusu watu. Tunataka mapendekezo yako kuhusu katiba. Kama alivyosema<br />
commissioner mwenzangu, unaweza kuwa na malalamiko miingi lakini hayo malalamiko, hayatatusaidia sisi ikiwa hautatwambia<br />
tunapendekeza hivi na hivi na hivi kutatua matatizo haya. Kwa hivyo hatutakubali kuingiliana watu kuchafuliana majina, au<br />
kutukana wengine, na mtu akifanya hivyo tutamsimamisha tuseme subiri.<br />
Lingine la mhimu kufahamu, ni kwamba kama alivyosema Commisisoner Ratanya, tutakaa hapa mpaka jioni, na tutatumia list hii<br />
lakini sisi lakini sisi huwaomba ruhusu wananchi kama nyinyi mbele kwamba kukiwa kuna sababu za kutosha, sisi kutokufuata<br />
list hii, tumuite mtu ambaye pengine hayuko kwenye list, au juna lake liko mwisho kwa sababu za kutosha. Kwa mfano, aje bibi<br />
mmoja hapa mja mzitu, na hawezi kusubiri kwa mda mrefu kukaa chini, sijui kama mtatupa ruhusa bibi kama huyo apewe nafasi<br />
asungumze aende nyumbani.