ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
40<br />
Roselyn Nyamato - Programme Officer<br />
George Kariuki - Asst. Programme Officer<br />
Zipporah Wambua - Verbatim Recorder.<br />
George Kimanthi - Co-ordinator<br />
Jimmy Muketha - Chairman<br />
George Kimanthi: Leo tuko na fulaha kubwa hapa Mikinduri, vile tumekuwa tukimwambia, leo tuko na commissioners,<br />
tumekuja hapa Mikinduri kuchukua maoni yenu, nitamueleza majina yao baadaye lakini ningeomba kwanza tuanze na maombi,<br />
mmoja wenu atuongoze kwa maombi.<br />
Mr. Kubai: Natuombe, Baba wetu uliye binguni, tunakushukuru baba kwa kutuwesesha kuona huu mchana wa leo, tena baba<br />
yetu kufikisha hata wageni wetu hapa Mikinduri ili kuongoza hali hii kulekembisha katiba, Mngu baba wetu tunakuomba baba,<br />
wewe ndiye unachagua wafaume ama viongozi, baba tunakuomba utuchagulie kiongozi anayefaa kutuongoza baba.<br />
Tumeteseka na ufisadi, na rushwa baba tunakuomba, kiongozi utakayemchagua akomeshe rushwa akomeshe ufisadi, ili baba<br />
watoto wetu wapate ujira, baba wetu uliye binguni, yeyote atakayeongea leo hii hapa Mikinduri, baba mpe nguvu na uwezo ya<br />
kuongea yale yatawezesha hii katiba ya Kenya kuweko kwa njia nzuri, baba wetu tunaomba kwa Kenya nzima, baba kuna<br />
magojwa mengi, shida nyingi za ukosefu wa kazi, na kadhalika. Baba tunaziweka mikononi mwako, ili yeyote atakayeongea<br />
aongee akiwa umemjaza roho wako mtakatifu. Twakuomba hayo machache tukijua baba utatukamilishia kwa jina la mwana<br />
wako bwana wetu Yesu Kristo. Amen.<br />
George Kimanthi: Asante sana bwana Kubai, kwanza kabisa mimi naitwa George Kimanthi. Labda kuna wengine ambao<br />
sijawai kutana na hao hapa lakini nakubuka nimekuwa katika vikao mingi hapa, kuona kazi yenu huko _____ (inaudible). Ni<br />
kawaida yetu kutabulisha wale tuko nao katika kila mikutano. Naona hapa tuko na chairman wa committee Mr. Jimmy<br />
Muketha. Halafu tuko na mwingine, wengine hawajafika, kuna wengine kwao ni mbali sana kama huko _______(inaudible) na<br />
kuna huyu mwingine ako hapa nje, Isaiah King’eru, mnamjua Kwa upande huyu tuko na commissioners kama vile<br />
tumemwambia, tuko na commissioner Zein Abubakar, halafu tuko na commissioner Domiziano Ratanya. Hapa tuko na<br />
prorgramme officers, tuko na Roselyn Naymata, halafu tuna Mr. George Kariuki, na Zipporah Ndunge. Hawa ndio tuko nao<br />
leo kuchukua maoni yenu kwa sababu hii ndio ile stage mhimu sana katika hii shughuli yetu ya kulekebisha katiba ya Kenya.<br />
Kwa hivyo mimi leo sitakua na mengi ya kusema, nataka tu kumuomba mshikilie yale watakaomwambia, watamueleza vile<br />
wanataka nyiny mtoe maoni yenu. Langu ni kumuomba tu muwe watulifu, msipige makirere, mfuate ile mtakaoambiwa, ile<br />
talatibu mtakaopatiwa mfuate sababu kama mnajua watu watakua wengi sana hapa na ukiambiwa uchukue dakika tatu ama ni<br />
mbili, ushikilie hapo usije kukaa hapa sana, kuongea saana kwa sababu kila mtu anataka kupewa nafasi ya kuongea. Si ni hivo<br />
Kwa hivyo nitamuomba Commissioner Damiziano Ratanya ampe ule utalatibu mtakaofuata na atamueleza zaidi kile wangetaka<br />
mfanye kama wananchi wa hapa Mikinduri.