ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
ON 17TH MAY, 2002 - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
72<br />
Mirungi Atunus: Asante sana kwa mwenyekiti. Kwa majina naitwa Atunus Mirungi kutoka upande wa Ngania. Jambo langu<br />
nataka lisiwe maanane ni hii na zungumzia. Mara mingi tumesikia ya kwamba ati serikali inapeana masomo ya bure kwa<br />
wananchi na hivyo sio ilivyo. Kama upande wa primary school, tumesikia ati serikali ilipeana masomo ya bure na tukiendelea na<br />
haya maneno, tunaangalia pande ya waalimu wa nursery school wanalipwa na wazazi na hiyo inakuwa na shida mingi sana kwa<br />
upande wa wazazi. Kwa maoni yangu nataka kama mwalimu wa nursery school awe ameajiriwa na serikali na isiwe maanani<br />
kwa sababu, na akiajiriwa lazima awe na experience na qualification ya college kama waalimu wengine na awe ameajiriwa na<br />
serikali sio wazazi.<br />
Jambo langu la pili, nazungumzia kuhusu hawa vijana wanaambiwa wanatia wasichana wa wenyewe mimba na wakawaacha.<br />
Ile jambo yani ninataka kusema hivi, kama vijana anaenda kwa mzee fulani, atie msichana miimba, na aende, serikali imchukulie<br />
hatua, kama ni huyu kijana akikataa kuoga huyo bibi alee huyo mtoto mpaka wakati umri wake ufike wa kuchukua kitabulisho.<br />
Maoni yangu mengine mwenyekiti, nasema ya kwamba, twende upade wa uchaguzi, kama ni ile contact zinapeanwa kwa<br />
ukalabati, tumesikia ya kwamba pande fulani kuna ukalabati inafanywa na mtu fulani. Hayo nami nataka kuyatia maanani ya<br />
kwamba, mtu akipewa kazi ya ukalabati, awe na qualification ya kutengeneza hiyo ukalabati, sio experience ya pesa. Naona<br />
kuna wale wako na qualifications lakini hawana pesa za kwendesha hiyo nini<br />
Jambo la tatu, nataka pande ya President, p<br />
Com. Ratanya: Goja kidogo, kuna watu ambao wanapiga kelele huko nje, mnajua mkiendelea namna hio itaingia kwa record<br />
yetu hapa. Kwa hivyo mnyamaze. Kwa hivyo endelea Atunas.<br />
Murungi Atunus: Kwa upande ya President, nataka serving President awe ako na sada ya degree na sio sada ya kupandikwa.<br />
Na upande ya bunge, mtu achaguliwe akiwa na umri wa miaka arubaine kwenda 75 na upande wa udiwani, local authorities,<br />
awe na elimu ya O’ level na nataka ata wale ambao wamechaguliwa wakiwa chini ya form 4 wasiruhusiwe hata kuomba kula<br />
kwa uchaguzi ujao<br />
Jambo lingine langu na la mwisho, naongea kuhusu hii mambo ya administration, upande wa chief, chief awe amechaguliwa na<br />
watu kwa mlolongo na awe amefikisha kiango cha O’ level na pande ya serikali, askali akishika mtu, sio lazima aweke kwa<br />
kambi kwa sababu ako na mabrother, ashike mtu apeleke yeye kwa koti mara moja sio kuweka mtu kwa cell. Kwa hayo<br />
machache namalizia hapo.<br />
Com. Ratanya: Asante sana Atunas kwa hayo machache. Sasa kuna Kobia Ritari Isaiah.