TUESDAY, JULY 9TH, 2002 - ConstitutionNet
TUESDAY, JULY 9TH, 2002 - ConstitutionNet
TUESDAY, JULY 9TH, 2002 - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
asiongeze mwingine. (laughter)<br />
Com. Asiyo: Asante sana. Hebu jiandikishe pale (inaudible) pole pole sio shida wewe weka tu. Ukisema msichana asizae<br />
mtoto mwingine, kama wanaume wangekuwa wanazaa dunia ingejaa leo. Kwa hivyo usikate shauri kwa wasichana waki<br />
…unaweza weka meathali umalize hapo. Asante sana sasa tunataka kumsikiliza mzee Harun Kandie. Tafadhali fika mbele kwa<br />
mambo machache sana kwa maana naona una karatasi hapo. Kwanza sema majina yako yote ili ishikwe na machine halafu<br />
uongee kwa muda mfupi sana kama dakika tatu.<br />
Harun Kandie: Asante sana Commissioner, na Commissioner mwenzako. Kwa jina ni Harun Kandie. Yangu ninaenda<br />
upande wa uongozi kwa upande wa machief ile style tungefuata. Style ile tungefuata kwa upande wa machiefs kuandika zamani<br />
wamababu zetu, walikuwa wanaendea kwa elders, kujua ni nyumba gani inastahili kuongoza wananchi. Na ilikuwa mzuri. Hiyo<br />
njia ilikuwa mzuri kwa wakati huo.<br />
Com. Asiyo: Sasa kwa wakati huu unataka wapigiwe kura au wafanye namna gani?<br />
Harun Kandie: Ile kitu ilikuja kuharibu Bwana Commissioner ni kuwa wanasiasa walikuja wakaingilia hiyo kitu, so<br />
wakaharibu ikawa baya.<br />
Com. Asiyo: So unapendekeza namna gani?<br />
Harun Kandie: Napendekeza iwe wazee elders, wawe watapewa jukumu ya kuangalia kama ni chiefs ama ni assistant chiefs<br />
wanagaa chini katika vijijini na kuona ni mtoto wa nyumba gani inafaa kuongoza sisi.<br />
Com. Asiyo: Hao wazee hawawezi kupewa kitu kidogo halafu wachague mtu (inaudible)<br />
Harun Kandie: Zamani ilikuwa hakuna hiyo walikuwa wanaongoza tu.<br />
Com. Asiyo: Zamani hakukuwa na kitu kidogo. Na sasa?<br />
Harun Kandie: Hii kitu kidogo ndiyo inaharibu mambo.<br />
Com.Asiyo: Sasa tutafanya namna gani?<br />
Harun Kandie: Wazee walikuwa wanajua ni nini wanaendelea na wazee wakigaa wanao mambo yao ya ndani.<br />
Com. Ayonga: Sasa hao wawezi kuonea nyumba fulani tu ndiyo inafaa kuwa inatawala na hali nyumba ile haitagawana?<br />
16