TUESDAY, JULY 9TH, 2002 - ConstitutionNet
TUESDAY, JULY 9TH, 2002 - ConstitutionNet
TUESDAY, JULY 9TH, 2002 - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Com. Asiyo: Mpaka miaka kumi na nane? Sasa sema ya mwisho.<br />
Harun Kandie: Ya mwisho ningeenda upande wa siasa. Hii watu wetu wa siasa. Siku hizi wanaenda parliament wiki mzima.<br />
Zamani wakati wa ukoloni sisi tulikuwa vijana Mbunge alikuwa anakuja, ikifungwa parliament anakuja mahali kwa wananchi<br />
kuchukua maoni ya wananchi. Lakini siku hizi hatuoni.<br />
Com. Ayonga: Sasa hiyo unataka aje?<br />
Harun Kandie: Tunataka hiyo iwekwe sheria kwa sababu sisi tunaandika yeye.<br />
Com. Ayonga: Weka sheria.<br />
Com. Asiyo: Sasa hiyo sheria ndiyo tunataka utambie sasa mara hiyo sheria yako ndiyo tunataka.<br />
Harun Kandie: Sheria hii yake tunataka wakati bunge hakuna, akuwe na watu wake.<br />
Com. Asiyo: Na kama hakukuja?<br />
Harun Kandie: Basi wananchi watajua (interjection)<br />
Com. Asiyo: Kama hakukuja tupatie sheria hiyo natuandike namna gani?<br />
Harun Kandie: Sasa kama huyu mtu hajakuja inaonekana hajui kazi yake wananchi wata-vote yeye out.<br />
Com. Asiyo: Kwa hivyo (inaudible) ni watu wangapi wanaoweza wanataka huyu mtu arudi nyumbani wachague mbunge<br />
mwingine. Watu wangapi kwa (inaudible)<br />
Harun Kandie: Nikirudi nyuma kidogo kuna mzee ameandika mambo ya (inadible)<br />
Com. Asiyo: Kama mtu hajafanya kazi yake kama Mbunge, na watu hawatosheki unataka Mjumbe mpya unataka watu<br />
wangapi wazee waseme kwa kweli huyu hajafanya kazi yake ndiyo tuwe na mpango ya kufanya recall yaani kurudisha yeye<br />
nyumbani halafu mtu mwingine achaguliwe? Maana kuna fitina mingi kama yule mtu aliangushwa anaweza tafuta watu kumi na<br />
mbili watu elfu moja waandike barua huyu mtu arudi hapa hatujaona yeye hafanyi kazi tunataka aondolewe. Na hiyo imeleta<br />
fitina nyingi sana katika nchi hii ta Kenya. Na wewe unajua fitina ya (inaudible) sasa tuambie unataka tufanye namna gani?<br />
20