TUESDAY, JULY 9TH, 2002 - ConstitutionNet
TUESDAY, JULY 9TH, 2002 - ConstitutionNet
TUESDAY, JULY 9TH, 2002 - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Com.Asiyo: Kwanza jiandikishe pale halafu ukae. Nataka kuuliza kuna mtu moja hapa ambaye angependa kusema kitu<br />
ambaye anaona mtu hajasema? Anaitwa nani? Kitu ambacho hakijasemwa anaitwa Boniface Kimwei. Boniface ulikuwa wapi<br />
wakati huu wote? Hapana hapana tuliita mara nyingi sana.<br />
Com. Ayonga: Sema hicho kitu<br />
Com. Siyo: Kidogo sana na ile haijasemwa<br />
Com. Ayonga: May be majina kwanza.<br />
Boniface Kimwei: Majina yangu ni Boniface Kimwei, ni mwalimu katika hii division. Now yangu ambayo ningpenda<br />
kupendekeza ni kwamba huu, - wakati mtu ako na mali yake kwa shamba lake serikali inaingilia. Hatungependa serikali<br />
iingilie. Mfano wakati uko na mali yako unakuta ya kwamba badala ya wewe ukate ile miti ndiyo wewe utumie, serikali lazima<br />
upate idhini kutoka kwa serikali (interjection)<br />
Com. Asiyo: Hiyoni haki ya serikali na ni vizuri na hiyo ni sheria mzuri sana na tutahimiza hiyo.<br />
Boniface Kimwei: Lakini tungependa kubandilisha hiyo sheria mtu awe ana control mali yake yeye mwenyewe. Jambo la pili ni<br />
kwamba kuna watu ambaye ni disabled, ni viwete. Utakuta wale watu serikali yetu tukufu haizingatii sana. Ningeonelea kwa<br />
maoni yangu ya kwamba serikali yenyewe itenge kiasi fulani cha pesa na ipatiwe katika wizara fulani, ndiyo iwe ikisaidia wale<br />
disabled wawe kama wale Wakenya wengine tuweze kuinua uchumi yetu katika Kenya.<br />
Ya tatu ni kwamba hii sheria inatungwa katika Kenya hii, inaongewa kwa lugha ingine ambayo mwananchi wa kawaida hawezi<br />
elewe. Ningeomba, baada ya kumaliza kutunga sheria hiyo sheria itafusiriwe katika lugha mbali mbali za makabila zetu za<br />
Kenya.<br />
Com. Asiyo: Hiyo tayari imeandikwa na pia itakuwa hivyo.<br />
Boniface Kimwei: Na pia iwekwe mahali ambapo wananchi wanaweza fikia kama District Coordinator awe na moja na<br />
Library (interjection)<br />
Com.Asiyo: Hata huyo alisema itakuwa ofisi yake.<br />
Boniface Kimwei: Jambo la nne ni kuhusu elimu katika nchi yetu. Utakuta ya kwamba elimu katika nchi yetu kila mtu anakuja<br />
na syllabus mwaka huu tunabadilisha hii, mwaka huu tunabadilisha hii, tungependa elimu tuwe na syllabus ingegaa hata miaka<br />
ishirini au ishirini na tano. Lakini si kubadilisha tukifika mwaka huu tunabadirisha ukifika mwana huu tunabadilisha, ukifika<br />
mwaka ule tunabadilisha. Yangu ni hayo asanteni sana.<br />
Com. Ayonga: Kuna neno ambalo tumeambiwa tukoka kila pahali, kwamba usiseme kiwete, si wewe ni mwalimu?<br />
Boniface Kimwei: Yes, Sir.<br />
77