constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
104<br />
Yampat mapelu: Ore naba nasuj ina.<br />
Translator: Yake ile ambayo itafuata hiyo,<br />
Yampat mapelu: Na ene wueji e nkisuma.<br />
Translator: Ni mambo ya elimu.<br />
Yampat mapelu: Ore ene wueji ena sukul ne primary.<br />
Translator: Mambo ya shule za Primary,<br />
Yampat mapelu: Nayieu nai neaku ene pesho.neaku aitabaiki ine pemaigil ta.<br />
Translator: Angependelea iwe ya bure.<br />
Lengete Kamete: Kwa jina naitwa Lengete Kamete. Na sina mengi ni machache mno. Langu la kwanza ningependelea<br />
mambo ya Electoral Commission ama Chairman wa Electoral Commission awe akichaguliwa na Parliament, isiwe tena ni Rais<br />
anateua mtu binafsi. Pia ningependelea mamboya President ama Rais, awe anaweza kuchaguliwa kwa muda wa mihula miwili.<br />
Kwa mfano awe kama miaka kumi kwa ile system iko Kenya sasa hivi. Hiyo system ya mihula miwili, pia Rais awe<br />
akichaguliwa tuseme kwa kabila hii, muhula huu. Muhula mwingine iwe ni kabila ingine. Kwa sababu naona kuna kabila zingine,<br />
Yesu atarudi kabla wengine hawajapata nafasi ya ku-enjoy huo muda. Kwa hivyo pia iangaliwe kwa makabila pia wahusike<br />
ama wawe wakichagua Rais wao.<br />
Com. Lethome: Unasema President achaguliwe kwa kila kabila?<br />
Lengete Kamete: Yes.<br />
Com. Lethome: Na tutafanyaje ili tujue the next kabila ama ni kura inapigwa au tunaenda alphabetical order ili tujue ile kabila<br />
inafuata?<br />
Lengete Kamete: Kwa mfano sasa hivi, Wakikuyu wameshakalia, Wakalenjin wameshakalia, sasa wengine tuseme kama ni<br />
Wakisii ama Wa-Baluhya ama ni Wa-Jaluo ama ni Wa-Maasai, wale ambao wana interest ya kuwa Rais, wasimame kwa kila<br />
kabila. Lakini Wa-Kikuyu na Wa-Kalenjin wasisimamishe mtu wao, zile kabila zingine kama kuna mtu anataka asimame na<br />
wananchi waamue ni mtu wa kutoka kabila gani mzuri.<br />
Com. Lethome: Kwa hivyo watakuja kupewa chance ingine baada ya miaka mia nne. Kwa sababu tuko na makabila arobaini<br />
na mbili mpaka saa hivi.