27.11.2014 Views

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

104<br />

Yampat mapelu: Ore naba nasuj ina.<br />

Translator: Yake ile ambayo itafuata hiyo,<br />

Yampat mapelu: Na ene wueji e nkisuma.<br />

Translator: Ni mambo ya elimu.<br />

Yampat mapelu: Ore ene wueji ena sukul ne primary.<br />

Translator: Mambo ya shule za Primary,<br />

Yampat mapelu: Nayieu nai neaku ene pesho.neaku aitabaiki ine pemaigil ta.<br />

Translator: Angependelea iwe ya bure.<br />

Lengete Kamete: Kwa jina naitwa Lengete Kamete. Na sina mengi ni machache mno. Langu la kwanza ningependelea<br />

mambo ya Electoral Commission ama Chairman wa Electoral Commission awe akichaguliwa na Parliament, isiwe tena ni Rais<br />

anateua mtu binafsi. Pia ningependelea mamboya President ama Rais, awe anaweza kuchaguliwa kwa muda wa mihula miwili.<br />

Kwa mfano awe kama miaka kumi kwa ile system iko Kenya sasa hivi. Hiyo system ya mihula miwili, pia Rais awe<br />

akichaguliwa tuseme kwa kabila hii, muhula huu. Muhula mwingine iwe ni kabila ingine. Kwa sababu naona kuna kabila zingine,<br />

Yesu atarudi kabla wengine hawajapata nafasi ya ku-enjoy huo muda. Kwa hivyo pia iangaliwe kwa makabila pia wahusike<br />

ama wawe wakichagua Rais wao.<br />

Com. Lethome: Unasema President achaguliwe kwa kila kabila?<br />

Lengete Kamete: Yes.<br />

Com. Lethome: Na tutafanyaje ili tujue the next kabila ama ni kura inapigwa au tunaenda alphabetical order ili tujue ile kabila<br />

inafuata?<br />

Lengete Kamete: Kwa mfano sasa hivi, Wakikuyu wameshakalia, Wakalenjin wameshakalia, sasa wengine tuseme kama ni<br />

Wakisii ama Wa-Baluhya ama ni Wa-Jaluo ama ni Wa-Maasai, wale ambao wana interest ya kuwa Rais, wasimame kwa kila<br />

kabila. Lakini Wa-Kikuyu na Wa-Kalenjin wasisimamishe mtu wao, zile kabila zingine kama kuna mtu anataka asimame na<br />

wananchi waamue ni mtu wa kutoka kabila gani mzuri.<br />

Com. Lethome: Kwa hivyo watakuja kupewa chance ingine baada ya miaka mia nne. Kwa sababu tuko na makabila arobaini<br />

na mbili mpaka saa hivi.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!