constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
42<br />
walizoahidiwa na Serikali hapo awali. Kama ni mshahara wapewe kwa sababu waliahidiwa. Au kama aliyeahidi aseme alikuwa<br />
wapi wakati aliahidi. Kwa hivyo wapewe nafasi wajieleze na wapewe haki zao kwa sababu wakiambiwa watafutwe sababu<br />
wanaitisha haki zao, wataletwa wale wengine ambao hawana ujuzi, pia kama madaktari hivo hivo.<br />
Katika upande wa elimu, kuna bursaries ambazo zinatoka kutoka kwa Serikali na tungeomba zipewe watoto kutoka makabila<br />
zote wakati zinapogawanywa kwa mashule. Tusiambiwe eti wewe umetoka karibu na Kiambu, upelekewe huko, wewe<br />
umetoka wapi upewe huko. Kama ni hapa, wapewe watoto wote wale wanahitajika kupewa ambao hawana uwezo wa<br />
kuelimishwa. Wafanyi biashara pia hapa au sehemu zote labda nchini, wananyanyaswa na Serikali ya Wilaya sijui kama ndio<br />
wanasimamia upande wa County Councils. Ma-licences inakuwa juu zaidi, watu hawaridhiki hata kama wanalipa lakini<br />
wanalipa shingo upande. Kwa hivyo hapo, pia waangalie kama watapunguza. Kwa sababu hakuna kitu tunaongezewa, ile pesa<br />
tunaongeza. Lakini hiyo biashara au vitu vina nini……na soko isiwe huru sana. Wananchi wanaumizwa.<br />
Kuna wafungwa: Wafungwa pia katika nchi tunaona hakuna haki. Unakuta hata kama ni mtu amechukuliwa kama suspect hapa,<br />
pahali popote hata kama si hapa. Unakuta anachukuliwa kama tayari amefanya ile kitu na kumbe hata hakuna investigation<br />
ilifanywa. Akihukumiwa kufungwa, anateswa, hali ya kutosha au pia wanawekwa kama magunia ya mahindi katika cell.<br />
Ningeomba waangaliwe.<br />
Nominated Councillors kama wale labda wataanguka upande huu, waangaliwe kama yule ambaye alikuwa namba mbili<br />
kushindwa. Kwa hivyo wasichague tu, fulani kama ni wa DP, upewe DP. Kama ni KANU, lazima wachague nominated kutoka<br />
kwa .<br />
Ya mwisho kuna hizi enquiries zinatengenezwa na Rais kila wakati. Unasikia labda mtu ameuawa, enquiries zinaundwa Nairobi,<br />
zinakaa miaka sita, sisi tukingojea tusikie baada ya mwaka, inakaa miaka kumi, labda mwingine amezeeka na hatajua ni nini<br />
iliendelea. Tungeomba wawe wakichukua huo wakati kwa muda mfupi na kutupatia ripoti haraka.<br />
Mwisho, ningesema….<br />
Com. Bishop Njoroge: Katika sheria iliyoko ni kwamba Commission za Enquiries, Rais amepewa mamlaka, ikiwa kuna kitu<br />
anataka kujua kwa ajili ya Serikali yake, anaweza kuitisha Commission <strong>of</strong> Enquiries, na sheria haijasema ni lazima awaambie<br />
wananchi. Isipokuwa mpende hiyo sheria iondolewe. Lakini kulingana na sheria iliyoko, hana wajibu wa kutuambia amepata<br />
nini. Kwa hivyo ni juu yenu kusema, tunataka ikae au isikae. Lakini sio makosa yake kwamba hakusema. Kwa sababu sheria<br />
inamruhusu kufanya nini? Kufanya hivyo.<br />
John K. Gichia: Nilikuwa nikisema, kuliko labda kuna ripoti tunangoja tusikie mahali alifanya kitu fulani. Isichukue miaka<br />
mingi.