constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
26<br />
Ya pili, siku hizi Serikali imenyima sisi haki. Kwa sababu wakati tuliandikwa sisi kazini, ichague mtu amesoma kwa sababu kazi<br />
ya bunduki sio lazima usome. Kazi ya kuandikwa kama askari sio lazima usome. Lakini siku hizi Wamaasai wametupwa kando,<br />
hawaandikwi kwa kazi, wanakuja kuandika watu wengine wanasema ni watu wa Kajiado, wanaacha wa Loitoktok.<br />
Tunapendekeza uajiri kama wa zamani, inasaidia. Kwa sababu ukifika area ya Umasaaini unakuta mtu amemaliza Standard<br />
eight, Form four yuko nyumbani. Serikali itusaidie sisi, tujisaidie sisi, tuandikwe kama zamani vile tulivyoandika na tulimaliza kazi<br />
yetu. Hatujasoma lakini hiyo kazi inaendelea vizuri mpaka wa leo tuko kazini. Sasa mimi sina mengi sana kwa sababu niligusia<br />
pahali ya majimbo na pahali ya masomo ndio nafaa nigusie kidogo. Kwa sababu area yetu imeenda kwa sababu tunapatiana<br />
kwa yule mtu ako na hope kidogo. Yule ambaye anaambiwa, ‘nifanye kitu fulani halafu nikupatie kazi.’ Serikali iangalie hapo.<br />
Sasa mimi sina mengi sana, ilikuwa ni hivyo tu na naomba Serikali iangalie kwa mambo hayo.<br />
Com. Bishop Njoroge: Haman Ole Nsuki. Isaiah Ole Samana. Isaiah?<br />
Isaiah Ole Samana: Yangu nitaanza moja kwa moja kulingana na vile nilivyoanza. Kwa majina naitwa Isaiah Ole Samana,<br />
mimi ni mkaaji wa Loitoktok sub-district. Yangu ya kwanza ni kuhusu Provincial Administration ama utawala wa mikoa.<br />
Utawala wa mikoa kwa mapendekezo yangu, ningependa iendelee kudumu. Sababu ni kwamba utawala wa mikoa, hiyo<br />
inaunganisha ama inapatanisha mtu kwa mtu. Utawala wa mkoa unaimarisha maendeleo na kuunganisha wananchi. Ni chombo<br />
cha kuunganisha wananchi na Serikali.<br />
Kuhusu madiwani: Madiwani mimi katika mapendekezo yangu, madiwani wanyimwe mamlaka. Kwa sababu gani? Diwani<br />
anapochaguliwa kuwa diwani, anakuwa na chance ya kunyakua ardhi ama kunyakua plots. Na kwa mapendekezo<br />
ningependekeza kuwe na kamati katika ward ya huyo diwani ambayo itakuwa ikihusika na mambo ya kupeana plot kwa<br />
wananchi.<br />
Kuhusu wafanyikazi: Wafanyikazi wa kila idara, tungependa wawe asilimia sabini. Wawe ni wenyeji wa hiyo sehemu. Kwa<br />
sababu tunaona ya kwamba wafanyikazi wengi unakuta wanatoka katika nje, sio wakaaji wa hii sehemu na wakaaji wa hii<br />
sehemu wengi wao wamesoma. Lakini kwa sababu ya godfathers huko mbele, unakuta wale wenyeji weanakosa kazi. Kwa<br />
hivyo kwa mapendekezo ninaona ya kwamba wafanyikazi wa kila idara wawe wenyeji wa hiyo sehemu. Asilimia sabini.<br />
Kuhusu Land Control Boards: Mashamba: Ningependekeza ya kwamba watu wanapouziana mashamba, waanze katika ngazi<br />
ya chini mashinani. Kwa sababu tunaona ya kwamba watu wengi siku hizi wanauziana mashamba na wanapelekana katika kazi<br />
ya mbele, ya juu zaidi. Bila kupitia ngazi za chini. Watoto hawajui, jirani hawajui, relative ya huyo mwenye kuuza hawajui. Kwa<br />
hivyo tungependekeza hiyo sheria ibadilishwe iwe mawelewano ya kuuziana mashamba ianze huko chini ndio wenyewe wapate<br />
kujua ya kwamba watoto watabakishiwa na sehemu ama huyo mtu asiuze kwa sababu kutakuwa na vile tutaweza msaidia hiyo<br />
ardhi ibaki.