constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
9<br />
Constitution. Ambayo katika district, itakuwa tu wakati kura inafanywa elections. Tuwe na Local Authority, kutoka Local<br />
Authority tuwe na Regional Authority.<br />
Com. Lethome: Hiyo Regional Authority itakuwa katika ngazi gani?<br />
Rev. Elias Ntoipo: Unamaanisha nini unaposema ngazi gani?<br />
Com. Lethome: Will it be at the Provincial level?<br />
Rev. Elias Ntoipo: Yes. It will be at the Provincial level.<br />
Com. Lethome: Majimbo will be a Province?<br />
Rev. Elias Ntoipo: It will be a Province. Ndio. Kama Rift nasema kwamba, igawe mara tatu, iwe North, iwe South, na<br />
Central. Hiyo ndio namaanisha. Kwamba ni region, sio katika kikabila. Aah ah - katika wale watu ambao wanakaa katika<br />
sehemu fulani ya given area.<br />
Com. Bishop Njoroge: Asante kwa maoni hayo. Palashina Ole Sunkuri.<br />
Palashina Ole Sunkuri: Mimi kwa majina ni Palashina Ole Sunkuri. Maoni yangu ni kwamba wakati mzungumzaji<br />
alipozungumzia mambo ya nchi kukuja kugawanywa kama sehemu ya Loitoktok hii. Ilikuwa iko kiwango ambayo wale<br />
wataalamu wa zamani walikuwa wanatuweka. Anasema kila mtu ni elfu moja. Lakini wakati huu, sijui vile ilifanyika mpaka<br />
wengine wanapata elfu tatu kwa kazi na wengine wako na zaidi ya elfu tatu. Nikaona hapo ni kama wagawaji ardhi<br />
wananyanyasa wengine. Tunataka kila kitu kiwe sawa.<br />
Kwa sababu kuna watu ambao hawana uwezo na wanaweza kunyanyaswa na wale ambao wako na uwezo. Sasa, kuja hapo<br />
tena kuweka ile tunaita Land Control Board, imemaliza watu kabisa. Ziko familia ambazo saa hii, hakuna hope hata ya acre<br />
moja. Kwa sababu ile kitu inatendeka hapo, tunakuta familia ni Mzee anaenda kuuza shamba, watoto hawajui, mama hajui, ni<br />
karatasi tu tunapelekea Mzee, aambiwe katika hiyo land ambayo alikuwa anaishi. Hiyo tumeona hapo, ni wanyanyasaji<br />
wakubwa kwa sababu hawa wananchi wenyewe wapewe ardhi yao. Waangaliliwe ardhi yao vile wanakaa. Kwa sababu<br />
mambo mengine unaona kama Commissioner wa Land huko Kajiado, hata huyu anaishi Kajiado, hana pesa ya kwenda huko<br />
kulalamika. Wanakimbia hapa hapa tu, kuzunguka kama chura akiwa ndani ya maji na hakuna kitu mtu anaweza kufanya. Sasa<br />
ardhi inaenda namna hiyo. Sehemu moja.<br />
Ya pili, tuko na mila, ambayo saa ingine tunakuwa kama Uongozi.