constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
61<br />
hapa mbele. Hawa ni wanafunzi wa shule na tutawakubali kupeana maoni ili waweze kurudi kwa shule. James Ngugi aje basi.<br />
James Ngugi: Asante sana. My name is James Ngugi, Mwalimu wa shule ya upili ya Ilasit Secondary School na nina maoni<br />
machache kuhusiana na kubadilishwa kwa Katiba ya Kenya. Kwanza nitazungumzia sana hasa kuhusu idara ya elimu kwa<br />
sababu mimi ni Mwalimu. Ningependekeza katika shule za msingi, kuwepo na shule maalum ambazo zitashughulikia wanafunzi<br />
ambao ingawaji sio wazuri sana katika yale masomo ya darasani na ni wazuri katika ile elimu nyingine kama ya ufundi, tailoring<br />
na kadhalika. Kuwe na shule maalum ambayo itaanzia kushughulikia masilahi ya hawa watoto wao kutoka katika shule za<br />
msingi hadi katika vyuo vikuu. Hata kuwe na mitihani ya kitaifa ambayo inahusiana na hiyo.<br />
Hiyo ni ya kwanza. Pili ningezungumzia kuhusu lugha ya Kiswahili na ningependekeza ya kwamba lugha ya Kiswahili iwe<br />
inafundishwa ama iwe ni somo la ufundishwaji kutoka katika shule ya msingi hadi vyuo vikuu. Hata vyuo viweke ile ndio ili<br />
kuleta ushikamano na ili kuleta hali fulani ya umoja katika nchi hii ya Kenya. Kwa hivyo kufungamana na hayo, ningependekeza<br />
ya kwamba kuwe na chama fulani ama kuwe na idara fulani katika wizara ambayo itahusiana na kuleta mbinu fulani ama<br />
mitakati fulani ambayo itachangia katika kuhakikisha ya kwamba Kiswahili kinafahamika na kila M<strong>kenya</strong>.<br />
Ya tatu ningependekeza ya kwamba hizi shule za kitaifa, zilikuwa chache sana na hizi shule kwa maoni yangu zilichangia sana<br />
katika kuleta ya ushikamano Kenya nzima na nikechangia ya kwamba hizi shule ziongezwe. Kwa sasa tuna shule kumi na nane<br />
tu za kitaifa hapa Kenya na tukiangalia hata katika wilaya hii, hakuna shule hata moja kama hiyo ya kitaifa. Na ningependekeza<br />
shule hizi ziongezwe kwa kupitia Wizara ya elimu, ihakikishe ya kwamba zitakuwa nyingi zaidi. Angalao kila wilaya kuwe na<br />
shule moja ya kitaifa. Halafu nikizungumzia kidogo kuhusu vyuo vikuu, ningependekeza ya kwamba wale Vice-Chancellors ama<br />
wale wakuu wa vyuo hivyo, ningeomba ya kwamba, isiwe Rais wa nchi ndiye ambaye ndio kiongozi pale. Bali iwe ni kiongozi<br />
msomi wa pale chuo kikuu. Kwa sababu inakuwa ni vigumu sana kuingilia au kuchanganya siasa na uongozi. Kwa hivyo<br />
ningependekeza ya kwamba hawa wawe ni wasomi ambao wanachaguliwa na wale wasomi katika chuo kile.<br />
Halafu pia ningependa pia kuzungumzia kuhusu swala la waalimu na ningependekeza ya kwamba mishahara ya waalimu pamoja<br />
na marupurupu yao na hali zozote zile za kikazi, zishughulikiwe na Katiba ambayo itakuja sasa. Iwe ya kwamba, maongezi ama<br />
mapatano yeyote kati ya Serikali na vile vyama vya waalimu, iwe ni kama sheria na isiwe inaweza kubadilishwa kwa hali yeyote<br />
ile.<br />
Halafu nikimalizia ningependa kuzungumzia pia kuhusu somo la Katiba. Ningependekeza kwamba pawe na somo la Katiba<br />
kutoka katika shule ya msingi. Ndio ili watu waweze kujua nchi yao. Kuna mifano mingi sana ya watu ambao hawajui nchi yao,<br />
hawajui namna nchi inavyoongozwa. Hawajui mambo ya haki yao na ningependekeza ya kwamba kuwe na somo la Katiba ama<br />
somo la Serikali - jina lenyewe, wale ambao wanahusika wanaweza kutoa jina nzuri. Iwe inaanzia katika shule ya msingi hadi<br />
kufikia katika vyuo vikuu. Asante sana.