constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
44<br />
Ma-Chiefs: Nafikiri Ma-Chiefs, ninaweza kusema ya kwamba Ma-Chiefs wakae vile walikuwa wakikaa na wawe ni wale<br />
Ma-Chiefs ambao wamechaguliwa katika ile sehemu ambayo wananchi wamezaliwa hapo. Awe ni wa hapo. Sio kwamba<br />
tunaweza kupendekeza iwe eti ni watu wa kwenda transfer. Hiyo hapana na sasa wawe ni wale ambao ni wananchi katika ile<br />
sehemu. Kwa hivyo kwa hiyo ninasema asante sana, sina mengi sana ila tu, niongeze ya kwamba, Serikali ibadilishe hayo<br />
mambo kwa njia ambayo inafaa. Kwa hivyo asante sana, mimi sikuwa na mengi.<br />
Com. Lethome: Asante sana. Jiandikishe. Daniel Molunkei.<br />
Daniel Molunkei: Kwa majina naitwa Daniel Molunkei, mkaaji wa Loitoktok. Kwanza ningependa tu kuzungumzia mambo<br />
ya Administration. Kwamba Administration ibaki vile vile na kuwa na PC, DC, hadi ngazi za chini za Chiefs, na Assistant<br />
Chiefs. Ila tu, ni kwamba iangaliwe Review Act ya uajiri wa Ma-Chiefs kwa kuwa tunaona ya kwamba wakati wakitangaza<br />
kuajiriwa kwa Ma-Chiefs. Unakuta ya kwamba hawafuati ile sheria, wengine wengi hapa katika eneo hili letu ni kwamba<br />
tumechaguliwa Ma-Chiefs ambao hata hawajui kuandikia mkubwa wake Bwana D.O. ripoti, ambao ni aibu kubwa sana. Sijui<br />
hiyo sheria mchunguze muangalie ni wapi kumekosewa. Kwa upande wa Ma-Chiefs pia, tungelipenda sheria ile ya zamani ya<br />
miaka zilizopita ya kwamba Ma-Chiefs wawe wakichaguliwa na raia wao katika eneo lao.<br />
Lingine ni mambo ya masomo, limezungumziwa zaidi lakini kwa upande wangu na maoni yangu, ningeonelea tu kwa mambo ya<br />
marks. Ya kwamba irudishwe ile sheria ya zamani ya kujaribu kuangalia zile remote areas na marks za watoto wa remote areas<br />
an wale amao wanaishi katika rural areas zipandishwe. Isiwe mtoto anafanya K.C.P.E na marks zake zitakuwa ni sawa na yule<br />
ambaye ako Nairobi. Kwa upande pia ya waalimu, itafutwe sheria ambayo ilikuwa hapo awali. Sijui imepotelea wapi, ya public<br />
funds mis-use ambapo Ma-Headmaster wengi wametumia fedha za shule na shule kuadimika. Na nafikiri hiyo ndio imeleta<br />
shida nyingi ya hapa watu wengi wanaanza kusema mashule na vitu kama hizo. Turudishe zile sheria za zamani.<br />
Mambo ya health: Health pia tungeliomba iwe completely free kama zamani ila tu in-patients waweze kulipa yale madai kidogo<br />
tu ya kitanda. Lakini kila kitu mpaka madawa iwe ni huru. Pia sheria iangaliwe ya kuanzisha mambo ya clinics, hizi private<br />
clinics. Imekuwa kwamba watu wegni wameanzisha tu private clinics. Unakuta ya kwamba kuna mtu ambaye yeye ni daktari<br />
mkuu na ameruhusiwa katika ki-pr<strong>of</strong>ession na sheria lakini anatumia watu wengine ambao sio pr<strong>of</strong>essionals wa kuweza<br />
kuendeleza ma-private clinics. Kwa hivyo tungeliomba sheria hiyo ya Ministry <strong>of</strong> Health, iangaliwe kwa maakini kwa sababu<br />
tuna mahospitali ambazo ni duni na kulingana na mambo ya utajiri ama mambo ya kipekee tuna shida hizo.<br />
Ya pili ni mabmbo ya K.W.S., ningeliomba sheria za zamani ziweze kuwa kwa sababu K.W.S. ni parastatal na sheria za<br />
wanyama wa pori ambayo iko katika Ministry <strong>of</strong> Tourism, iangaliwe irudi hasa kwa upande wa compensation. Compensation<br />
tulikuwa tunalipwa fedha na nafikiri kulikuwa na sheria ambayo ilikuwa imewekwa. Hapa mtu akiuawa na wanyama kama vile<br />
wale wa mbele walisema hakuna fedha ambazo wanalipwa. Mashamba hailipwi.