constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
53<br />
ndio wanajua shida za wananchi wao.<br />
Soko huru imeumiza umma. Kwa hivyo hiyo soko huru ifutiliwe mbali. Ma-Chiefs wawe lakini wachaguliwe na watu wa eneo<br />
lake. Sio Bunge. Kwa sababu kunaweza kuwa kuna mpinzani, atachagua mwenzake na pengine hajaridhisha umma. Kwa hivyo<br />
Ma-Chief wawe lakini wachaguliwe na umma.<br />
Hospitali: Tuna shida ya mahospitali kwa sababu madaktari wetu wakuu wanafanya biashara. Unakuta daktari mkuu wa<br />
hospitali, anakuandikia madawa ya kwenda kuchukua kwa clinic fulani. Kumbe ni clinic yake. Kwa hivyo iangaliwe mfanyi<br />
biashara na muhudumu wa umma.<br />
Com. Bishop Njoroge: Unataka kusema ya kwamba, madaktari wana<strong>of</strong>anya kazi kwa mahospitali ya Serikali wasikubaliwe<br />
kuwa na clinics zao?<br />
Ibrahim K. Kailepi: Wasikubaliwe kuwa na clinics zao. Wanaumiza umma na waalimu wasikubaliwe wawe na biashara zao.<br />
Asanteni.<br />
Com. Bishop Njoroge: Thank you very much. Joseph Kulare.<br />
Joseph Kulare: Kwa majina ni Joseph Kulare kutoka Ilasit Loitoktok. Nikizungumzia hoja ya kwanza ni kwa President.<br />
President apunguzwe madaraka yake. Asiwe na madaraka ya juu zaidi kwamba akitaka kuvunja Bunge, anavunja tu bila taarifa<br />
yeyote. Ma-Chiefs, MPs, wawe wakichaguliwa na wananchi na wahudumu kwa muda wa miaka mitano ndio wafanyiwe<br />
elections. Hata President asikae kwa muda wa miaka kumi. Iwe full term. Mambo ya culture: Culture itupiliwe mbali kabisa<br />
especially Wa-Maasai wenzetu wanasoma kutoka form one, form four, wanaenda mambo ya ukarani, na hawa Ma-MPs<br />
wanatumia hawa makarani ku-succeed, kupitia kura daraja ya kwenda Bungeni. Pia the formation <strong>of</strong> the Government:<br />
Tunataka Serikali ya Majimbo ili Serikali iwe na uwezo wa kuangalia watu katika eneo hiyo na wajue idadi ya watu walioko<br />
katika eneo hilo. Especially ya kwetu Loitoktok, sijapendelea sehemu zingine ziwe hivyo lakini kama kwetu Loitoktok, tuna<br />
watu kutoka Tanzania, Rwanda, Burundi, wamepotelea huko for ages na huyo mtu akifa analeta shida. Hujui huyo mtu ametoka<br />
wapi na haujui alikuwa mharifu kutoka nchi fulani ndio akahamia upande huu. Kwa hivyo tuwe na formation ya Majimbo. Ikinge<br />
wale wenyeji wa hizo sehemu za hapo karibu.<br />
Land Act: Mashamba mimi nafikiria kwa council isiuzwe bila kupitia kwa familia iwapo tu kuna shida ya dharura ambayo<br />
ingefanywa waweze kuuza hiyo shamba. Kwa ajili mashamba unakuta inauzwa ma<strong>of</strong>isini, iki-signiwa tu na yule karani wa land,<br />
unakuta familia haijui mtoto wao ameuza shamba. Ukienda kwa Chifu, Chifu anakwambia wewe angalia ile sehemu yako<br />
uliachiwa, wacha huyu ale mali yake. Kwa hivyo Chiefs nao wasiwe na powers, kuwa na Kangaroo courts katika <strong>of</strong>isi zao.