constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
59<br />
Serikali ifikirie wale hawana kwa sababu kuna watu wanarundikana kwa railway line, hii reserve. Hiyo railway line ambayo ni<br />
reserve iko na railway, watu wanarundikana huko hawana mashamba na sio kupenda kwao. Zilinyakuliwa na wale wenye<br />
mamlaka zamani.<br />
Lingine mtu kama awe tortured na ichunguzwe ionekane hakuwa na hatua, huyo mtu anakuwa compensated kwa sababu labda<br />
ni madai ya uwongo na rushwa ilitendeka labda pale. Kwa hivyo yangu ni hayo tu.<br />
Com. Bishop Njoroge: Hebu nikuulize, si ni heri ku-recommend kwamba kusiwe na torture. Mtu akishikwa anapelekwa<br />
mahakamani kuliko baadaye. Kwa sababu hiyo ni rahisi. Mtu akishikwa anapelekwa wapi? Mahakamani. Si hivyo ndivyo<br />
ilikuwa? Sawa. Nenda pale. Let’s have Benjamin S. Masharen, headteacher. Karibu.<br />
Benjamin S. Masharen: Asante sana Mwenyekiti, ningependa pia kutoa maoni isipokuwa mambo haya ya Katiba ni magumu<br />
sana na yanakuwa na detail yaani mambo yanaenda ndani sana lakini hata hivyo nitajaribu kutumia wakati mchache sana kwa<br />
sababu mimi ni Mwalimu wa historia. Nikisema ni ku-lecture itachukua muda mrefu sana.<br />
Jambo la kwanza muhimu zaidi ni kwamba mimi niko proponent au kwa kinaganaga, mimi naunga mkono Serikali ya Majimbo.<br />
Lakini sio hii Majimbo ya wanasiasa wa Kenya ya ukabila ya kutaka makabila fulani wafukuzwe katika jimbo hilo. Ile federal<br />
government kama ile ya United States <strong>of</strong> America, Canada na nchi zingine ambazo zimeendelea. Sitafafanua sana kwa sababu<br />
itachukua muda lakini ijulikane kwamba maoni yangu ni kwamba naunga mkono Serikali ya Majimbo. Nije hapa nyumbani kwa<br />
sababu mimi ni mtoto wa hapa nyumbani, ningependa kusema kwamba kwa sababu Katiba inahusu haki za watoto. Hapa tuna<br />
makabila ambayo wanahamahama katika nchi yetu, zinaitwa pastoral communities. Kuna pengine Wa-Maasai, Wa-Rendille,<br />
Borana, Wa-Somali na kadhalika. Ningependa Serikali au Katiba yetu ambayo tutakuwa tunatengeneza wakati huu, ichukulie<br />
maanani makabila haya. Natumai Mwenyekiti wakati ulikuwa unakuja huku kwa gari, ukiangalia huko sehemu zimeachwa<br />
kabisa.<br />
Ningependa Katiba ichukulie maanani makabila yanayohamahama na wawe classified kama endangered species. Kama vile<br />
tumesema ukimwi ni janga, tuseme pia makabila hawa, wawe endangered species na kuwe na Wizara maalum ambayo<br />
itahusiana na hali ya kuchunguza haki ya makabila haya. Kuwe na Wizara katika Serikali ya kuangalia masilahi yao. Masilahi<br />
kama elimu ya bure. Wawe hao watoto wanapewa chakula ya bure kama incentive. Kitu ya kuwaweka moyo wawe shuleni.<br />
Wawe na free medical services au matibabu ya bure. Wakimaliza shule wawe wanapewa priority katika employment.<br />
Wanapewa mstari wa mbele katika kuajiliwa ili wawe kama wale wengine na wawe pia kama incentive kuwapa moyo wale<br />
hawajasoma ndio waweze kusoma. Na wawe wanapewa priority katika admission, katika enrolment. Hata saa ingine pengine<br />
hawajafanya vizuri katika mitihani yao kwa sababu ya shida, kwa sababu ya ukame, sehemu wanaoishi wawe wanapewa<br />
priority. Jambo lingine kidogo kugusia tu kwa sababu muda hautaniruhusu ni kwamba pia wananchi na wanyama. Hawa