constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
86<br />
Administration yaani Chiefs. Chiefs wawe wanachaguliwa na raia kwa sababu tumekuwa na shida ya mtu kuchaguliwa na mtu<br />
mmoja na kutaka atekeleze mapenzi yake mwenyewe na si masilahi ya mwananchi.<br />
Jambo la pili ni kuhusu mwanamke. Mwanamke katika jamii ya Wa-Maasai hana haki, hawana haki, kwa sababu Maasai akioa<br />
anaweza kumuacha yule mke wakati wowote anapotaka. Sasa Serikali kwa sababu hii Katiba inatengenezwa na wamama<br />
Wa-Maasai wamepoteza maisha yao kwa sababu wanapoachwa na wazee hakuna kipengele cha sheria kinachowasimamia.<br />
Maana kuna ndoa za kienyeji, zile za kawaida kinyumbani na huwa Serikali haitilii maanani hasa sana kwa upande wa jamii ya<br />
Wa-Maasai, wamama wengi. Hata wengine wanapata stress na kufa. Maana wanafukuzwa wakati wowote na hawalipwi<br />
chochote kutoka boma ile na labda amekaa miaka mingi akazaa na anafukuzwa, anaambiwa watoto ni wa bwana, mama<br />
anaenda hana mtoto, hana mali, hana shamba. Kwa hivyo harithi chochote.<br />
Kuhusu NGO’s zile ziko katika maeneo t<strong>of</strong>auti katika Kenya, ningependelea mimi kwa maoni yangu, Serikali iwe ikiingilia kati.<br />
Kuweko na wakilishi kutoka kwa Serikali kwa sababu kumekuwa na mchezo ambao unachezwa ambaye kama NGO’s zikija<br />
kuingia katika kufanya miradi, unakuta ni ya watu wachache, ndio wanaenda kufaidika nayo. Kwa hivyo ningeomba kwa mfano<br />
kama Chiefs ama wakilishi kutoka Serikali, wawekwe katika kila sehemu ambayo NGO inafanya kazi.<br />
Kuhusu afya, ningeomba Serikali iangalie kiasi cha umbali kutoka kwa kituo cha afya hadi kingine. Kwa sababu sikusema ziwe<br />
chache lakini sehemu ile ambayo iko na mingi ni sawa hata kama ni baada ya nusu kilomita kuwe na kituo cha afya ni sawa.<br />
Lakini kuna maeneo mengi hasa kama za jamii ambayo wanahamahama, unaweza kukuta hospitali karibu kilomita mia mbili ama<br />
mia moja, uende ukakute kituo cha afya ambayo inaweza kusaidia wananchi. Na kuna mambo matatu ambayo Serikali ya<br />
Kenya iliahidi wananchi kwamba watapambana na magonjwa na ujinga na ningeonelea kwa maoni yangu, kuwepo na kiasi ya<br />
umbali ambayo Serikali itaangalia, kuwepo na kituo cha afya cha Serikali.<br />
Kwa upande huo wa afya, ningependelea wale wahudumu wanaohudumu katika hospitali za Serikali wasiwe na biashara nje.<br />
Kama mtu ni daktari na afanye huduma pale. Kuweko na hiyo sheria. Kama mtu anataka biashara, akafanye biashara na aache<br />
ile maana kuna watu wengi wa Kenya ambao hawana kazi. Kwa sababu ukiangalia kama hospitali zetu hapa, unakuta madawa<br />
zote zimeenda kwa ma-clinics za watu binafsi. Ukienda pale unaandikiwa rundo ya madawa, ukienda pale unakuta ni madaktari<br />
wanauza zile madawa na kwa kweli imetuumiza sana.<br />
Kuhusu ardhi: Ninaonelea ya kwamba kuna watu wanaona labda mbuga kama group ranches kwa mfano, watu wengi wanaona<br />
wanafikiri ni sehemu ambazo hazina wenyewe ama hazina kazi. Lakini nigependa kusema tu kwamba hilo ni shamba la watu,<br />
inaweza kuwa lina watu mia sita na hawajakatiwa bado na wana watoto wengi zaidi lakini bado hawajagawiwa kwa sababu<br />
wanatumia kwa ufugaji. Ningeomba tu kwamba hata kama Katiba itapitisha kwamba, kuwepo na mahali ambapo Serikali ikatie<br />
watu hawana ardhi. Lile ni shamba la wenyewe na lina idadi ya watu wake, wapewe nafasi ya kujisimamia wenyewe na<br />
wapewe nafasi ya kujiandika wenyewe na hata kukaribisha mgeni kama atakuja alime. Lakini sio lazima awe mwenyeji eti kwa