constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
4<br />
Watu wa Loitoktok, wanawakaribisha kwa moyo dhati kwa sababu haya mambo ya Katiba ni mambo ya maisha ya Wa<strong>kenya</strong>.<br />
Ama sivyo? Kwa hivyo nafurahia. Jana tulikuwa Rombo na kusema ukweli Wamaasai watu wanasema hawajasoma, lakini yale<br />
mawazo walipeana nina uhakika hata wale wameenda University hawataweza. Na hiyo ni kwa sababu ya uongozi bora tukiwa<br />
na Mheshimiwa, tukiwa na madiwani, tukiwa na wafanyikazi wa Serikali, viongozi wa dini, viongozi wa chama. Tumesema watu<br />
wajulishwe katika kila sehemu kuja kupeana maoni yao kwa mambo ya Katiba. Kwa hivyo nafikiri wale Wamaasai tulikuwa<br />
tunasema labda maoni yao itakuwa ni kasoro kwa sababu hawana masomo, lakini yale wamepeana, tunataka watu wa<br />
Loitoktok, hata mvuje record zaidi. Kwa sababu wasomi si wako hapa?<br />
Wale wasomi tunajivunia katika hii sehemu, si mko hapa? Kwa hivyo tunataka mpeane maoni yenu na mimi niko hapa<br />
kukaribisha hao wageni. Baada ya kuwakaribisha nitakuwa raia mwema kama nyinyi. Msinihesabu kama D.O. Kwa sababu ni<br />
lazima nije nisikize mambo ya Katiba. Leo niko D.O., kesho nitakuwa raia mwema kama nyinyi. Kwa hivyo ni kitu inahusu<br />
maisha yetu. Kwa hivyo Bwana Commissioner, kwa sababu muda nao ni kidogo na watu ni wengi, na bado watakuja wengi.<br />
Nasema karibuni Loitoktok na tunashukuru kwa nyinyi kufika, asanteni.<br />
Com. Bishop Njoroge: Asante Bwana D.O. Sasa mimi nataka kuwaambia vile tutaendelea. Kwanza nataka kutangaza kikao<br />
hiki kama kikao rasmi ya Katiba na tunapoketi hapa tujue tuna sheria ile inayo tusimamia kwa yale mambo ambayo tutafanya<br />
hivi leo. Jambo la kwanza, kila mtu atakuwa huru kusema maneno ambayo anafikiria inaweza kusaidia katika kuunda Katiba.<br />
Kama mjuavyo, Katiba hii ni watu wenyewe waseme wanataka iwe namna gani. Kwa hivyo msiogope kwamba D.O. yuko<br />
hapa. Hata wakati tuna P.C au Mawaziri wa Serikali, wanajua kwamba watu ni lazima wawe huru kusema yale wanayohitaji<br />
kusema. Hakuna mtu anaweza kufuatwa kwa sababu ya yale aliyoyasema leo. Ile Act ambayo inatutawala inasema, kila mtu<br />
ana uhuru. Lakini ningetaka kusema hivi; hakuna mtu ana uhuru kuzungumza juu ya mtu binafsi kwa njia yeyote mbaya ama<br />
njema. Kwa sababu ni Katiba tunafanya nini? Tunatengeneza. Ninataka kutoa mfano. Mtu anaweza kusema, tunataka mamlaka<br />
ya Rais ipunguzwe. Haya ni mapendekezo, inafaa. Lakini huwezi kusema juu ya mtu katika Serikali kwa njia yeyote mbaya kwa<br />
sababu hiyo haitaenda katika Katiba. Tumekubaliana hivyo? Na mtu akisema hivyo, nitamkataza kuendelea kwa sababu ni<br />
lazima tuwe na mapendekezo ambayo yataingia kwa Katiba. Unaweza kuwa na Mbunge na huna furaha naye, huna ruhusa<br />
kusema juu ya Mbunge. Unaweza kusema tunahitaji barabara. Sawasawa? Hayo ni mambo ya Kikatiba. Kwa hivyo hata kama<br />
tuna uhuru, hatuna uhuru wa kusema mabaya ya watu. Si hapo tumekubaliana?<br />
Jambo la pili, sisi ni Wa<strong>kenya</strong>, tunajua kuna shida nyingi. Tunajua kuna watu wengi hawana pesa ya kwenda kununua madawa.<br />
Tunajua mara ingine kwa mahospitali hakuna madawa. Kwa hivyo usituambie zile shida kwa urefu, tuambie mapendekezo yako<br />
ni nini, ili tutatue shida gani? Shida hiyo. Tukifanya hivyo, tutatumia muda mfupi na yale ambayo unasema, itasaidia kutengeneza<br />
Katiba hii. Kwa hivyo tunataka mapendekezo. Kama jana, kama vile D.O. alivyosema na Councillor pia alisema vizuri huko<br />
Rombo kwamba tunahitaji tu mapendekezo. Kwa sababu hiyo ndio itaenda kwa Katiba.