27.11.2014 Views

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

4<br />

Watu wa Loitoktok, wanawakaribisha kwa moyo dhati kwa sababu haya mambo ya Katiba ni mambo ya maisha ya Wa<strong>kenya</strong>.<br />

Ama sivyo? Kwa hivyo nafurahia. Jana tulikuwa Rombo na kusema ukweli Wamaasai watu wanasema hawajasoma, lakini yale<br />

mawazo walipeana nina uhakika hata wale wameenda University hawataweza. Na hiyo ni kwa sababu ya uongozi bora tukiwa<br />

na Mheshimiwa, tukiwa na madiwani, tukiwa na wafanyikazi wa Serikali, viongozi wa dini, viongozi wa chama. Tumesema watu<br />

wajulishwe katika kila sehemu kuja kupeana maoni yao kwa mambo ya Katiba. Kwa hivyo nafikiri wale Wamaasai tulikuwa<br />

tunasema labda maoni yao itakuwa ni kasoro kwa sababu hawana masomo, lakini yale wamepeana, tunataka watu wa<br />

Loitoktok, hata mvuje record zaidi. Kwa sababu wasomi si wako hapa?<br />

Wale wasomi tunajivunia katika hii sehemu, si mko hapa? Kwa hivyo tunataka mpeane maoni yenu na mimi niko hapa<br />

kukaribisha hao wageni. Baada ya kuwakaribisha nitakuwa raia mwema kama nyinyi. Msinihesabu kama D.O. Kwa sababu ni<br />

lazima nije nisikize mambo ya Katiba. Leo niko D.O., kesho nitakuwa raia mwema kama nyinyi. Kwa hivyo ni kitu inahusu<br />

maisha yetu. Kwa hivyo Bwana Commissioner, kwa sababu muda nao ni kidogo na watu ni wengi, na bado watakuja wengi.<br />

Nasema karibuni Loitoktok na tunashukuru kwa nyinyi kufika, asanteni.<br />

Com. Bishop Njoroge: Asante Bwana D.O. Sasa mimi nataka kuwaambia vile tutaendelea. Kwanza nataka kutangaza kikao<br />

hiki kama kikao rasmi ya Katiba na tunapoketi hapa tujue tuna sheria ile inayo tusimamia kwa yale mambo ambayo tutafanya<br />

hivi leo. Jambo la kwanza, kila mtu atakuwa huru kusema maneno ambayo anafikiria inaweza kusaidia katika kuunda Katiba.<br />

Kama mjuavyo, Katiba hii ni watu wenyewe waseme wanataka iwe namna gani. Kwa hivyo msiogope kwamba D.O. yuko<br />

hapa. Hata wakati tuna P.C au Mawaziri wa Serikali, wanajua kwamba watu ni lazima wawe huru kusema yale wanayohitaji<br />

kusema. Hakuna mtu anaweza kufuatwa kwa sababu ya yale aliyoyasema leo. Ile Act ambayo inatutawala inasema, kila mtu<br />

ana uhuru. Lakini ningetaka kusema hivi; hakuna mtu ana uhuru kuzungumza juu ya mtu binafsi kwa njia yeyote mbaya ama<br />

njema. Kwa sababu ni Katiba tunafanya nini? Tunatengeneza. Ninataka kutoa mfano. Mtu anaweza kusema, tunataka mamlaka<br />

ya Rais ipunguzwe. Haya ni mapendekezo, inafaa. Lakini huwezi kusema juu ya mtu katika Serikali kwa njia yeyote mbaya kwa<br />

sababu hiyo haitaenda katika Katiba. Tumekubaliana hivyo? Na mtu akisema hivyo, nitamkataza kuendelea kwa sababu ni<br />

lazima tuwe na mapendekezo ambayo yataingia kwa Katiba. Unaweza kuwa na Mbunge na huna furaha naye, huna ruhusa<br />

kusema juu ya Mbunge. Unaweza kusema tunahitaji barabara. Sawasawa? Hayo ni mambo ya Kikatiba. Kwa hivyo hata kama<br />

tuna uhuru, hatuna uhuru wa kusema mabaya ya watu. Si hapo tumekubaliana?<br />

Jambo la pili, sisi ni Wa<strong>kenya</strong>, tunajua kuna shida nyingi. Tunajua kuna watu wengi hawana pesa ya kwenda kununua madawa.<br />

Tunajua mara ingine kwa mahospitali hakuna madawa. Kwa hivyo usituambie zile shida kwa urefu, tuambie mapendekezo yako<br />

ni nini, ili tutatue shida gani? Shida hiyo. Tukifanya hivyo, tutatumia muda mfupi na yale ambayo unasema, itasaidia kutengeneza<br />

Katiba hii. Kwa hivyo tunataka mapendekezo. Kama jana, kama vile D.O. alivyosema na Councillor pia alisema vizuri huko<br />

Rombo kwamba tunahitaji tu mapendekezo. Kwa sababu hiyo ndio itaenda kwa Katiba.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!