27.11.2014 Views

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

56<br />

mbao kabla ya miti kuwa imetoshea. Ningeomba kuwe na sheria kali ambayo mtu ataadhibiwa, hata awe ni Rais, awe ni nani,<br />

aadhibiwe kama anapeana ruhusu ama amepatikana akipasua mbao katika forest. Sehemu za chemchem ya maji ama mito,<br />

kando kando ya maji, ningependekeza kuwekwe sheria, mtu ambaye shamba yake imekaribia kwa maji, at least hatua fulani<br />

ziwe ni za miti, sio za kulimwa, ikabe hiyo maji.<br />

Kwa mfano katika hii sehemu yetu ya Nodrues, watu wale ambao wanaishi hiyo sehemu, ingetengwo hiyo ardhi iwe ni water<br />

catchment na ipandwe miti na wale wako hapo wahamishwe wapewe shamba mahali pengine ambao ni pazuri kama hapo.<br />

Lakini wale watafutiwe mahali kwa sababu wataharibu maji, kwa sababu mwanzo wata-pollute hiyo maji na tena watafanya<br />

ikuje kukauka haraka. Kwa hivyo national resources ni lazima zitunzwe kwa njia ya hali ya juu. Pawe na sheria inasimamia<br />

hivyo. Asanteni.<br />

Com. Bishop Njoroge: Elijah Ole Koptitat, akifuatwa na Simon Gachuru. Simon Gachuru yuko?<br />

Elijah Ole Koptitat: Mimi ninaitwa Elijah Koptitat, sio Peter. Yangu ya kwanza ni juu ya Rais. Rais awe ni mtu ambaye<br />

anachaguliwa na watu wote. Waziri Mkuu pia nafasi yake ipatikane. Nafasi ya Waziri Mkuu pia ni nafasi ambayo ingefaa<br />

ipatikane. Mbunge achaguliwe mtu ambaye amemaliza form 4, isiwe chini ya form 4, form 4 na juu. Pia nominated MPs kuwe ni<br />

mama au mlemavu. Asiwe ni mtu ambaye ni mwanamume anaweza kwenda kujitafutia kura. Lakini maana mama hawezei<br />

kutembea sana, labda anaolewa. Au mlemavu hawezi kutembea kwa hivyo ningesema hiyo nafasi ya nominated MP, iwe ni ya<br />

akina mama na walemavu.<br />

Councillor awe pia ni mtu wa form four and above. Asiwe tena mtu wa chini wa Primary school. Provincial Administration<br />

idumu kama kawaida. Iendelee tu kama kawaida lakini ningeomba kwa nafasi ya Ma-Chiefs, Chief awe ni mtu wa kutoka pia<br />

naye O’level na kuendelea juu. Asiwe chini ya O’level. Na pia awe anachaguliwa na wale watu wa hiyo location anayotaka<br />

kusimamia. Maana hii kazi ya kwenda interviews huko kwa wilaya, saa ingine inachaguliwa mtu ambaye hafai kabisa. Kwa<br />

hivyo ingefaa kabisa awe anachuguliwa na wale watu wake wanaotaka kumsimamia. Mambo ya national parks iwe chini ya<br />

Local Aauthority kama game reserves kwa hivyo isiwe tena chini ya Central Government.<br />

Serikali, mimi kwa maoni yangu ningependa Serikali ya Majimbo kabisa. Serikali ya Majimbo ianzishwe hasa kutoka uchuguzi<br />

huu ambao tunaenda sasa.<br />

Land Control Boards: Mashamba yauzwe na familia nzima na sio mzee tu au mama kama hana bwana. Awe ni mama tu<br />

mwenyewe anaenda kuuza shamba kwa sababu ana familia mwenyewe. Iwe inauzwa na familia nzima, wakubaliane na wote<br />

waende kwa Land Control Board waseme ya kwamba, tumekubalia kwa ajili ya hili tatizo na hili basi lipewe kwanza.<br />

Com. Bishop Njoroge: Wacha nikuulize kabla hujafika hapo. Huko Kimana, tuliambiwa kwamba ili kuzuia kuuzwa kwa

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!