constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
62<br />
Com. Bishop Njoroge: Jiandikishe pale. Josephat Kilingu? Ningetaka kuwaambia sasa tuzungumze kwa haraka. Tuna listi ya<br />
watu mia moja thelathini na sita na tumefikia tu namba hamsini na nne. Kwa hivyo mnaona ni watu wengi. Msip<strong>of</strong>anya haraka,<br />
kuna wengine hawatazungumza.<br />
Josephat Kilungu: Nashukuru sana kwa kupata nafasi hii. Kwa majina yangu ni Josephat Kilungu kutoka shule ya upili ya<br />
Ilasit. Niko hapa kutoa maoni yangu kuhusu.<br />
Com. Bishop Njoroge: Which form are you in?<br />
Josephat Kilungu: Form four.<br />
Com. Bishop Njoroge: How old are you?<br />
Josephat Kilungu: I am twenty-two years. Nimekuja hapa kutoa maoni yangu kuhusu Katiba ya Kenya. Kwanza kabisa<br />
ningependa kuzungumza kuhusu masomo ya shuleni. Kwa kweli kabisa kama sisi wanafunzi tunaumia sana kwani masomo<br />
shuleni yamekuwa mengi sana kiasi kwamba yanatuchosha. Kwa hivyo kama ingewezekana ni vyema kama masomo<br />
yangepunguzwa. Masomo yapunguzwe yawe angalao hata kama ni tano, halafu wanafunzi ndio waweze kupata nafasi ya<br />
kusoma masomo hayo. Pia katika shule, mashule mengi humo nchini, kuna wazazi ambao ni maskini ambao hawawezi<br />
kuwafundisha wanafunzi au hawana fedha za kuwafundisha wanafunzi wale. Kwa hivyo ni vyema kama Serikali ingetoa msaada<br />
wa fedha na pia vyakula katika mashule yetu. Ndiposa, wale wazazi ambao hawawezi kuwahitimu wanafunzi wao kifedha ama<br />
kivyakula, wafaidike katika masomo yetu pia.<br />
Pia, kuna mashule ambazo zimechanganyikana. Kuna shule zetu Kenya, zile shule zinafanya vizuri unakuta ni shule ambazo ni za<br />
wavulana peke yao ama wasichana peke yao. Kwa hivyo ningependa Serikali yetu iweke shule zote ziwe, kama ni za<br />
wasichana ziwe - za wasichana peke yake. Kama ni za wanaume, basi ziwe za wanaume peke yake. Hizi shule za<br />
mchanganyiko, zisiwe kabisa katika nchi yetu. Kwa sababu ukiangalia, shule zinafanya vizuri ni hizo.<br />
Com. Bishop Njoroge: Don’t explain. Go straight to the point.<br />
Josephat Kilungu: Pia ningependa mashule yapewe magari kwa sababu shule nyingi ziko na shida za usafiri. Kwa hivyo ni<br />
vyema Serikali kama ingepata magari ya kusafiria huko shuleni. Pia tungependa Serikali kama ingepeana mafunzo kuhusu<br />
Katiba. Mambo kama haya ya Katiba kuna mashule mengi sana hayajui mambo ya Katiba. Kwa hivyo ni vyema kama<br />
tungepata mafunzo ya Katiba huko shuleni. Pia mafunzo kuhusu afya ni vyema. Magonjwa kama haya hatari hatari, ni vyema<br />
kama Serikali ingetupatia mafunzo kuhusu haya magonjwa. Tungefurahia sana. Pia kuna haya masomo ya computer. Ingekuwa