constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
85<br />
Koyan Ole Masunga: Ingine, tuko na shida na tunashukuru hii Katiba kwa maana tuko na mahospitali. Serikali ya ukoloni<br />
zamani ilikuwa ya bure. Tumepata uhuru wetu na ni kama hayo mambo imekuwa mabaya.<br />
Com. Bishop Njoroge: Ungetaka hospitali iwe ya bure?<br />
Koyan Ole Masunga: Tungetaka hospitali iwe ya bure.<br />
Com. Bishop Njoroge: Kwenda nyingine.<br />
Koyan Ole Masunga: Madaktari wanyimwe zile hospitali zao za nje. Ingine ya tatu ni ya mashule. Mashule nayo pia, wakati<br />
wa ukoloni, mkoloni alikuwa anasomesha watoto na sasa Serikali yetu sasa, (inaudible). Kwa hivyo tunataka masomo ya bure.<br />
Hakuna Serikali na Serikali.<br />
Ya nne, upande wa Agriculture. Agriculturist, hawafanyi kazi yao. Tunasikia jina tu agriculturalist lakini hatumuoni. Kulinda miti<br />
yote ilikuwa imekatwa na huyu mtu alikuwa, kwa hivyo wao hawafanyi kazi. Kwa hivyo nchi imekuwa jangwa kwa vile wale<br />
waliokuwa wanalinda hiyo misitu, hawalindi.<br />
Upande wa veterinary: Naye veterinary pia, zamani wakati wa mkoloni, walikuwa wanaangalia mifugo yetu lakini sasa<br />
hawaangalii ni jina tu veterinary ni sisi tunasimamia mali yetu. Kwa hivyo nayo Serikali iangalie.<br />
Ya tano, tunataka Majimbo. Sio Majimbo ya mtu ahame mwenye alikuwa amehamia hapa. Tupewe Majimbo lakini tulinde mali<br />
yetu na tuangalie hasara na faida. Wakulima wamekuwa watu wa bure. Hakuna faida yeyote tunapata. Tunataka Serikali<br />
iangalie bei ya mkulima maana mkulima ni kama mtu amefungwa na mkulima kama anakwama, hata Serikali haiko. Kwa hivyo<br />
mkulima aangaliwe sana. Mambo ya kibarua, kibarua iko juu lakini mavuno yako chini.<br />
Com. Bishop Njoroge: Mzee, nenda kwa pointi yako ya mwisho.<br />
Koyan Ole Masunga: Pointi yangu ya mwisho, Serikali yetu tukufu, Rais wetu awe na kipindi cha miaka kumi. Wabunge<br />
wetu wawe na kipindi cha miaka tano kama kawaida. Wabunge wetu, zile pesa wanamwaga mwaga ovyo ovyo, aje amwage<br />
kwa mashule. Sio kuja kununua watu. Asante.<br />
Com. Bishop Njoroge: Rev. Simon Kanaiya? Karibu.<br />
Rev. Simon Kanaiya: Majina yangu ni Rev. Archdeacon Kanaiya na mimi ni mkaaji wa hapa Loitoktok na nimeshukuru sana<br />
kupata nafasi hii kujadili juu ya Katiba ambayo ndio inaangalia masilahi ya Kenya. Jambo la kwanza ni kuhusu mambo ya