constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
63<br />
ni vizuri sana kama computer lessons zingekuwa compulsory kwa kila mwanafunzi. Kwa sababu kuna mashule mengi hawana<br />
computer. Kwa hivyo ni vizuri kama ingekuwa compulsory kwa kila mwanafunzi.<br />
Pia usalama shuleni. Mashule mengi hayana usalama. Ni vyema kama Serikali ingepeana usalama huko shuleni ili mambo kama<br />
kuchomwa kwa wanafunzi, kesi kama hizo ziishe. Pawe na usalama. Masomo kama ya hesabu ama haya ya science, masomo<br />
haya yamekuwa magumu sana na hapo mbeleni ukiangalia ni vyema, watu walikuwa wanafanya vizuri haya masomo. Kwa hivyo<br />
inamaanisha kuna jambo fulani ambalo limefanya au vitu vimeongezwa, haya masomo yakawa magumu mno. Kwa hivyo ni<br />
vyema kama ingerahisishwa ili angalao wanafunzi wawe wakipita maana mbeleni walikuwa wanapita lakini sasa hawapita.<br />
Kumaanisha ya kwamba kuna vitu ambavo viliongezwa huko ambazo zinasababisha wanafunzi waanguke.<br />
Com. Bishop Njoroge: Unasema standard iletwe chini ili wanafunzi wapite?<br />
Josephat Kilungu: No.<br />
Com. Bishop Njoroge: Sema yako ya mwisho.<br />
Josephat Kilungu: Langu la mwisho, Muungano wa Jumuiya ya Afrika Mashiriki. Ingekuwa ni vizuri sana, wakati viongozi<br />
wanakutana kwenda kutoa maoni yao katika Muuongano wa East Africa, ni vyema pia kama wanafunzi wangepewa nafasi<br />
wanashiriki katika hiyo mikutano ndio tujue ni nini inaendelea. Kwa hayo machache, nashukuru sana.<br />
Com. Bishop Njoroge: Thank you very much. Very clear thinking, come here and register. I wish you well in your studies.<br />
Tupate Esther Wangechi. Karibu.<br />
Esther Wangechi: Nashukuru sana kwa nafasi hii ambayo ninakuja kutoa maoni yangu kuhusu Katiba. Jina langu ni Esther<br />
Wangechi kutoka shule ya upili ya Ilasit. Kwa maoni yangu, ningependa katika kila shule kuwe na hii <strong>of</strong>isi ya guiding and<br />
counseling. Ukiangalia wanafunzi wengi, wengine wanaacha shule kwa kukosa mawaidha.<br />
Jambo la pili shule ziongezwe. Shule na pia waalimu waongeze ili elimu katika mashule iwe bora. Jambo lingine ni, ukiangalia si<br />
wazazi wote wana uwezo wa kuwasomesha vyema watoto wao. Kwa hivyo ningependelea Serikali ipeane kama ni bursaries za<br />
shule na pia vitabu hizi za textbooks ili wanafunzi waweze kufaulu vizuri.<br />
Jambo lingine ni elimu ya wasichana. Wanafunzi wasichana wapewe nafasi ya kusoma katika viwango vyote vya elimu.<br />
Ukiangalia wanafunzi wengi hawamalizi shule maana wanaozwa. Jambo lingine ni usawa wa vifaa katika mashule. Ningependa<br />
mashule yote yawe na usawa wa vifaa. Si kwamba mashule mengine ni bora kuliko mengine. Kwa mfano katika maabara, vifaa<br />
viwe sawa katika shule zote.