constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
12<br />
itarudishwa kwetu tukiona ya kwama yeye hafai. Na kwa hivyo tutarudishiwa na wananchi watapewa maoni yao. Wakishatoa<br />
yale maoni, yale maoni ndio yatapelekewa wale Ma-MP na vote <strong>of</strong> no confidence ambayo itakuwa ni fifty five percent.<br />
Ikipitishwa basi yule President anatoka na tuna-elect another President.<br />
Huduma za lazima: Huduma za lazima ni kama elimu, health na kadhalika. Sasa katika huduma za lazima, kwanza katika elimu.<br />
Elimu ni muhimu katika nchi na kwa hivyo, lazima elimu iendelezwe na wale ambao ni pr<strong>of</strong>essional. Sio mtu tu ambaye hawezi<br />
kuendeleza elimu. Wanasiasa wameachiwa mamlaka mengi sana katika kuendeleza elimu. Kwa mfano tukichukua 8-4-4,<br />
ilikuwa ni elimu mzuri lakini kwa sababu wanasiasa waliingilia, wa leo utakuta kwamba inaonekana ni kama sio chombo<br />
ambacho kilikuwa ni cha muhimu. Na ingali ilikuwako ni kumsaidia yule mtoto, akitoka nje iweze kumsaidia katika pande<br />
mbalimbali. Kwa hivyo maoni yangu ni kwamba pr<strong>of</strong>essionals waachiwe ku-draw the curriculum na waachiwe pia kuendeleza<br />
katika elimu. Pia health hivyo hivyo.<br />
Biashara zimewekwa vikwazo vingi sana. Lazima uwe na licence, pia kodi ziko nyingi nyingi na hizo kodi utakuta ya kwamba<br />
yule, kama ni kijana ama ni mzee ambaye amekuwa retrenched or so, hawezi akaendeleza ile biashara kwa sababu ile kodi<br />
iliyoko ni nyingi sana. Kwa hivyo kodi iondolewe katika pande za biashara na hata ikiwa ni katika mambo ya kutoa vitu hivi,<br />
kama ni biashara kidogo kidogo, mama anakwenda jikoni kununua vitu vidogo vidogo, hizo biashara zimewekwa kodi ya aina<br />
yeyote, ziondolewe.<br />
Com. Bishop Njoroge: Bwana Philip, umetumia dakika kumi, nakupatia dakika moja.<br />
Philip Leshinka: Sasa tunaanza mashamba. Mashamba wakulima wapatiwe mbegu kwa sababu ukulima ni uti wa mgongo<br />
katika nchi hii. Wapatiwe mbegu na chemicals za kuweza kuondoa wadudu na kadhalika. Pia soko wakulima wapatiwe.<br />
Halafu jambo la mwisho ni juu ya mazingira. Mazingira ni jambo la muhimu zaidi na ni lazima kila mtu ahimiziwe kuweka<br />
mazingira safi. Kama ni mambo ya ukataji wa miti, ukataliwe mbali, kama ni mambo ya kwenda kulima kando kando ya mito,<br />
ukataliwe mbali. Kama ni mambo ya kuenda kukata miti, pahali ambapo vianzo vya maji zipo, ukataliwe mbali. Na ni hayo tu.<br />
Com. Bishop Njoroge: Tupate Bernard Kamau.<br />
Bernard Kamau: Asante sana kwa kunipa muda wa kusema. Kitu cha kwanza, pesa ya Serikali inatakiwa itoke kwa Bunge.<br />
La pili, jina ukabila lipigwe marufuku hata ikiwa ni kwa mkutano. Ya tatu, tunatakiwa tuwe tukiuliza maswali kwa mkutano. Ya<br />
nne, Kenya inatakiwa kuwe na vyama vitatu. Ya tano, Mbunge angetoka chama hiki, aende chama kingine, kusifanywe<br />
uchaguzi tena, kukae namna hiyo. Yangu ni hayo.<br />
Com. Lethome: Neno ukabila umesema liwe katika mkutano? Hebu fafanue.