27.11.2014 Views

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

43<br />

Com. Bishop Njoroge: Kwa hivyo ungetaka ikae au iondolewe?<br />

John K. Gichia: Enquiries ziendelee lakini zisikae muda mrefu.<br />

Com. Lethome: Matokeo yake, ungependa yatangazwe kwa watu ama iwe siri ya Rais?<br />

John K. Gichia: Hatutaki iwe siri ya Rais. Kama ni mambo kama kifo cha Ouko, ambao watu wengi walilia kujua. Hatukujua<br />

nani aliua? Labda mpaka saa hii wanajua. Tungependa tuwe tukiambiwa wazi.<br />

Ya mwisho, nasikia kuna watu wanasema mambo ya Administration iondolewe kama Chief. Mimi ningeonelea Administration<br />

yote, ikae hivo hivo. Security pia ambayo iko nchini, iendelee hivyo hivyo. Kwa sababu sioni sababu uondoe Chief. Labda<br />

anayelalamika Chief aondolewe, labda ni mkatili katika eneo lake. Kwa hivyo naomba Administration ikae hivyo hivyo.<br />

Asanteni.<br />

Com. Bishop Njoroge: Asante John. Tupate Samuel Nyaoga. Medingi Ole Mlaroni. Karibu Mzee. Taja jina lako kwanza.<br />

Medingi Ole Mlaroni: Mimi kwa majina naitwa Medingi Ole Mlaroni. Mimi ni Mzee ambaye anaishi sehemu ya Ole Leti,<br />

katika sehemu za Rongai. Mimi naeleza mapendekezo yangu; ya kwanza napendekeza Raisa awe na uwezo wa kusimamia<br />

Kenya mzima. Halafu pendekezo la pili, ninapendekeza ya kwamba, Kenya iwe na Serikali ya Majimbo lakini iwe Rais ndiye<br />

anasimamia wote.<br />

Pendekezo langu la tatu ni kwamba katika sehemu ya Wa-Maasai. Kuna sehemu nyingi imeenda kama Amboseli. Kama<br />

sehemu hiyo ambayo ilikuwa inaitwa Tsavo. Irudishwe iwe mikononi ya wenyeji.<br />

Jambo lingine la tatu ni kwamba masomo katika sehemu ya Wa-Maasai inakuwa dhiifu kidogo. Ningeomba Ma-Chief wapewe<br />

nafasi, kabisa waweze kuwa na sheria ya kusema watoto wapelekwe shuleni. Kwa sababu tunaona masomo siku hizi ndio kitu<br />

kikubwa ambacho unaweza kumuachia mtoto wako. Kwa hivyo Ma-Chief, mimi napendekeza Ma-Chief wachukue sheria<br />

hiyo, iwe ni sheria katika nchi ya Wa-Maasai ama katika Kenya.<br />

Jambo lingine Councillors: Ma-Councillors ambao wanachaguliwa katika Kenya, wao wenyewe wanachukua madaraka yao na<br />

hakuna kitu anaweza kuwapa wananchi sawasawa kulingana na vile inatakikana. Iwe plots, Councillor awe na kamati yake,<br />

ambayo inatoka katika ile eneo ambayo inasimamia Ward yake ili wakae na kugawa zile plots. Isiwe anakuja na agawie watu<br />

wale anawapenda. Anaweza kuwa anagawia ndugu yake ama anagawia mtu ambaye alikuwa rafiki yake. Kwa hivyo tunataka<br />

Councillors wawe ni watu ambao watakuwa na kamati ambayo itasimamia plots.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!