27.11.2014 Views

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

68<br />

Translator: Kwa hivyo ni hayo tu. Asanteni.<br />

Com. Bishop Njoroge: Mama njoo pale. Unasikia wanaume sasa tuko katika shida. Njoo hapa Mzee.<br />

Samuel Kahiu: Jina langu ni Samuel Kahiu. Nikichangia mjadala huu wa Katiba, tunaona Ma-Chifu watu wakichaguliwa kama<br />

zamani. Ma-Chifu wawe wakichaguliwa na raia kama zamani wakati wa enzi ya Mzee. Mwananchi wa Kenya ana haki ya<br />

kukaa pahali popote anataka kukaa na akimaliza kama miaka ishirini, awe akigombania kiti chochote, akiwa ni Chifu, akiwa ni<br />

Mbunge, awe akigombania maanake watoto wale wamezaliwa hapo wamekua na wakuwa watu wakubwa. Kwa upande wa<br />

wananchi, mwananchi wa Kenya apewa heshima kama watu wale wengine kama Wahindi, Waarabu, maana ukiangalia kama<br />

mtu anaitwa Mwarabu, anaweza kupiga mwananchi wa Kenya na asiulizwe na mtu.Maana yake mwananchi wa Kenya hana<br />

nafasi ya kujitetea maana ni pesa inaingia.<br />

Kitu kinaitwa Majimbo, hiyo itupiliwe mbali. Maanake kuna kufunikwa kwa watu (inaudible). Na hii Majimbo ndio huleta utata,<br />

ukiangalia kama Uganda, kwingineko kuko na uchacha shauri ya hii Majimbo. Watu wale mia nne, watu wale wana taabu,<br />

hawapatiwi pesa ya kuridhisha. Wapatiwe pesa ya kuweza kuenda kuangalia kazi yake maana sasa ameacha kazi.<br />

Madiwani: Madiwani wale wanateuliwa, wawe wakiteuliwa juu ana masomo. Kwa hivyo sina mengi ni hayo tu.<br />

Com. Lethome: Asante sana Mzee Samuel. Julius Ntei Korati yuko? Simon Maritei? Lawrence Karanja. Muteli Minduti,<br />

Tepai Tapokoi, James M. Wahome. Karibu Wahome. Joseph Kiutho yuko?<br />

James Wahome: Kwa majina ni James Mburu Wahome. Yangu ninapendekeza Rais awe anachaguliwa na wananchi wote<br />

bila kutoka kwa chama chochote na awe hana mamlaka makubwa kama hiyo ya kuteua wasimamizi wa sehemu hizo za kama<br />

Ma-Judges na wale wengine ambao wanasimamia hata kama ni kuchagua hao wasimamizi wa vyuo vikuu. Wawe<br />

wanachaguliwa kupitia kwa Parliament. Pia ninapendekeza wanaochagua wawe na uwezo wa kupitisha vote <strong>of</strong> no confidence<br />

na Mbunge wao kama hawatendei vyema.<br />

Pia ninapendekeza habari ya mashamba. Kwa kweli tuna watu ambao wana mashamba vikundi vikundi ama hapa na pale na<br />

bado ana shamba moja kubwa ambayo haitumiki. Unasikia mtu ana acre elfu ishirini na tano na hali kuna mwananchi ambaye<br />

hana hata chochote. Ninafikiria iwe ni haki ya mtu yeyote katika Kenya apate ardhi. Pia ninapendekeza iwe ni haki ya masomo<br />

kwa kila mtoto ama yeyote yule ako Kenya. Iwe ni haki. Upande huo wa masomo kutoka kiwango cha chini mpaka cha juu,<br />

Serikali iwe inaangalia. Kama ni hao walimu wapate mishahara mikubwa na kwa njia hiyo tutaepusha hawa watu wa chokora<br />

na hao watu wengine ambao tunaona hawana elimu. Kufikia hapo, ninaona iwe ni haki ya mtu kuishi popote pale na ikiwa ana<br />

rasilimali mahali pale anaishi, awe na haki pia ya kugombania kiti chochote kile cha utawala. Kwa hayo machache asante.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!