constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
68<br />
Translator: Kwa hivyo ni hayo tu. Asanteni.<br />
Com. Bishop Njoroge: Mama njoo pale. Unasikia wanaume sasa tuko katika shida. Njoo hapa Mzee.<br />
Samuel Kahiu: Jina langu ni Samuel Kahiu. Nikichangia mjadala huu wa Katiba, tunaona Ma-Chifu watu wakichaguliwa kama<br />
zamani. Ma-Chifu wawe wakichaguliwa na raia kama zamani wakati wa enzi ya Mzee. Mwananchi wa Kenya ana haki ya<br />
kukaa pahali popote anataka kukaa na akimaliza kama miaka ishirini, awe akigombania kiti chochote, akiwa ni Chifu, akiwa ni<br />
Mbunge, awe akigombania maanake watoto wale wamezaliwa hapo wamekua na wakuwa watu wakubwa. Kwa upande wa<br />
wananchi, mwananchi wa Kenya apewa heshima kama watu wale wengine kama Wahindi, Waarabu, maana ukiangalia kama<br />
mtu anaitwa Mwarabu, anaweza kupiga mwananchi wa Kenya na asiulizwe na mtu.Maana yake mwananchi wa Kenya hana<br />
nafasi ya kujitetea maana ni pesa inaingia.<br />
Kitu kinaitwa Majimbo, hiyo itupiliwe mbali. Maanake kuna kufunikwa kwa watu (inaudible). Na hii Majimbo ndio huleta utata,<br />
ukiangalia kama Uganda, kwingineko kuko na uchacha shauri ya hii Majimbo. Watu wale mia nne, watu wale wana taabu,<br />
hawapatiwi pesa ya kuridhisha. Wapatiwe pesa ya kuweza kuenda kuangalia kazi yake maana sasa ameacha kazi.<br />
Madiwani: Madiwani wale wanateuliwa, wawe wakiteuliwa juu ana masomo. Kwa hivyo sina mengi ni hayo tu.<br />
Com. Lethome: Asante sana Mzee Samuel. Julius Ntei Korati yuko? Simon Maritei? Lawrence Karanja. Muteli Minduti,<br />
Tepai Tapokoi, James M. Wahome. Karibu Wahome. Joseph Kiutho yuko?<br />
James Wahome: Kwa majina ni James Mburu Wahome. Yangu ninapendekeza Rais awe anachaguliwa na wananchi wote<br />
bila kutoka kwa chama chochote na awe hana mamlaka makubwa kama hiyo ya kuteua wasimamizi wa sehemu hizo za kama<br />
Ma-Judges na wale wengine ambao wanasimamia hata kama ni kuchagua hao wasimamizi wa vyuo vikuu. Wawe<br />
wanachaguliwa kupitia kwa Parliament. Pia ninapendekeza wanaochagua wawe na uwezo wa kupitisha vote <strong>of</strong> no confidence<br />
na Mbunge wao kama hawatendei vyema.<br />
Pia ninapendekeza habari ya mashamba. Kwa kweli tuna watu ambao wana mashamba vikundi vikundi ama hapa na pale na<br />
bado ana shamba moja kubwa ambayo haitumiki. Unasikia mtu ana acre elfu ishirini na tano na hali kuna mwananchi ambaye<br />
hana hata chochote. Ninafikiria iwe ni haki ya mtu yeyote katika Kenya apate ardhi. Pia ninapendekeza iwe ni haki ya masomo<br />
kwa kila mtoto ama yeyote yule ako Kenya. Iwe ni haki. Upande huo wa masomo kutoka kiwango cha chini mpaka cha juu,<br />
Serikali iwe inaangalia. Kama ni hao walimu wapate mishahara mikubwa na kwa njia hiyo tutaepusha hawa watu wa chokora<br />
na hao watu wengine ambao tunaona hawana elimu. Kufikia hapo, ninaona iwe ni haki ya mtu kuishi popote pale na ikiwa ana<br />
rasilimali mahali pale anaishi, awe na haki pia ya kugombania kiti chochote kile cha utawala. Kwa hayo machache asante.