constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
57<br />
mashamba kwa njia hiyo, mama na mzee wawekwe katika Title Deed. Kwa sababu hiyo itazuia mzee kuuza kama mama hajui.<br />
Hata mzee mwingine alisema mama, mzee na watoto waingizwe katika Title Deed. Ungefikiria namna gani?<br />
Elijah Ole Koptitat: Ardhi: Kuna ardhi ambayo inataliwa na mtu anaitwa Commissioner <strong>of</strong> Lands. Mimi kwa maoni yangu<br />
ningesema ya kwamba, iwe inaangaliwa iko chini ya wenyeji wa hapo hapo na sio Commissioner <strong>of</strong> Lands maana huyo anauza<br />
bila wenyewe kujua ardhi imeenda wapi.<br />
Elimu: Elimu iwe ni ya lazima kwa watoto wote, wavulana kwa wasichana na iwe ni ya lazima. Watoto wakifika umri wa<br />
kwenda shuleni, mtoto aende kwa lazima shuleni na elimu iwe ni ya bure. Pia mzazi au mtu yeyote akitoa mtoto wa kike shuleni<br />
kwa njia ya kwenda kuoza au mtoto wa kike akiwekwa mimba au kutoa tu mtoto wa kike kwa njia yeyote, huyu mtu<br />
ashitakiwe mara moja. Pia nafasi, intake ya Teachers Training Colleges, watoto wa sehemu kame, wafikiriwe kwa upande wa<br />
marks. Maana labda hawatakuwa sawasawa na watoto wa miji. Kwa hivyo mimi ningeomba watoto wa sehemu kame<br />
wafikiriwe wakati wa kupelekwa katika Teachers Training College.<br />
Uongozi katika sehemu mbalimbali: Uongozi uwe mikononi mwa wenyeji wa eneo fulani. Kwa mfano Chifu, Councillor na<br />
Mbunge, mtu ambaye ni mgeni aliyekuja kutoka mbali, aje kutafuta U-Chifu hapa katika sehemu ambayo yeye ni mgeni<br />
kwanza. Au Councillor aje kutafuta kazi ya Council hapa, wangepatiwa nafasi wenyeji, Chiefs, Councillor na hata Mbunge<br />
lakini sio mgeni. Kazi pia ya Serikali.<br />
Com. Bishop Njoroge: Sheria ambayo inatutawala inasema M<strong>kenya</strong> ambaye yuko mahali fulani, huwezi kumnyima haki kuwa<br />
katika cheo fulani. Sasa unataka tubadilishe hiyo sheria sasa tuseme kila mahali, mtu ambaye hajazaliwa hapo, hawezi kupata<br />
cheo fulani katika mahali pale?<br />
Elijah Ole Koptitat: Ndio sababu Bwana Commissioner tuko hapa tunabadilisha. Tunataka tubadilishe. Kazi ya Serikali<br />
ifikiriwe wenyeji wa eneo hilo kwanza. Kwa mfano kazi ikipeanwa interviews, watu ambao ni wa nje ndio hupatiwa zaidi kwa<br />
ajili inasemekana ya kwamba ndio wana market zaidi. Kwa hivyowatu wa area hiyo hiyo hata kwa kazi ya Serikali, kwa<br />
interviews first priority iende kwa wenyeji.<br />
Ya mwisho, ni watu kujipatia majina ya mahali ambapo sio kwao kwa ajili ya kutafuta kazi au kupita mitihani. Kuna watu wengi<br />
ambao katika nchi hii yetu ya Kenya wana majina ambayo si ya kwao. Lakini kwa ajili ya mitihani, ili waende Secondary<br />
schools au University au kazi, wanasema mimi ni Ole. Na kumbe sio Ole, yeye ni wa mahali pengine. Lakini kwa ajili ya kupata<br />
kazi, anajipatia jina la bandia. Kwa hivyo imi yangu ningesema ya kwamba, mtu achukue jina la kwao na kama hiyo ni riziki ya<br />
kazi kutoka kwa Mungu, atapata tu hiyo kazi. Kwa hivyo, mimi hayo ndio yangu.<br />
Com. Bishop Njoroge: Asante Bwana Koptitat kwa maoni hayo. Njoo hapa ujiandikishe katika register. Tukimaliza na huyu