constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
54<br />
Unaenda pale, yeye ndio anatatua kesi na hiyo kesi ingekaguliwa tu na elders wa eneo hilo.<br />
Tukija upande wa hospitali: Hospitali ziwe za bure, maji iwe ya bure na education. Kwa ajili watu wengi wameshakuwa maskini<br />
kabisa kwa ajili mkulima analima shamba, Serikali haitilii maanani huyo mkulima, chakula yake anatoa. Hajui specific price<br />
anaenda kuuza bei gani. Akikula leo mahindi ni shilingi mia tatu, mtoto anatakiwa elfu ishirini na tano Sekondari, kwa hivyo<br />
elimu iwe ya bure.<br />
Madaktari waongezewe mishahara na wanyimwe kufungua clinics. Ukienda especially our district hospital here Loitoktok,<br />
unaenda unaambiwa hakuna dawa, nenda clinic fulani. Na unakuta the same medicine imetoka kwa hiyo hospitali kubwa na<br />
ikaenda kwa hiyo. Kwa hivyo madaktari waongezewe mishahara, wasiwe na biashara yeyote ya hospitali ndogo ndogo kando<br />
ya hospitali kubwa kubwa.<br />
Group ranches at least isimamiwe na wenyeji na iwe na auditing kwa ajili hizi pesa tunapewa na K.W.S haitoshi. Tunataka<br />
iongezwe na iwe na auditing ijulikane hiyo hela kama ingesomesha watoto au ingetumiwa na individual. Unakuta mtu ameenda<br />
kununua gari, amenunua (inaudible) zake, unakuta hizo hela hazi-educate wale members wa group ranches, unakuta ina-educate<br />
mtu fulani kwa ajili ni Chairman. Especially unakuta wengine walikuwa wanasimamia group ranches, they are not helpful for the<br />
area. Unakuta anapewa pesa ya kwenda kusoma kwa masomo ya juu na ingali watoto native, wako nyumbani hawajasoma na<br />
hawajapewa hela ya kuwasaidia. Ni hayo tu.<br />
Com. Bishop Njoroge: Thank you Mr. Kulare. Francis Wambua? Akifuatwa na Paul Njenga. Paul Njenga yuko wapi? Peter<br />
Koptitat yuko? Unamfuata.<br />
Francis Wambua: Asante sana. Kwa majina naitwa Francis Wambua na mimi ni mfanyikazi wa sehemu hii ya Loitoktok.<br />
Ningependa kutoa maoni yangu juu ya hii Commission. Mwanzo ningependa kuangalia katika uchaguzi wa MPs na Councillors.<br />
Nikianzia na uchaguzi wa Rais, Rais angechaguliwa bila kuwa MP mahali popote. Achaguliwe asimame tu kama mtu kwa kiti<br />
cha Rais peke yake. Ili asikuwe mtu wa kupendelea sehemu yake aache sehemu ya nchi yake. MPs nao wachaguliwe watu<br />
ambao wamesoma hasa kwanzia kidato cha Form four. Wawe na elimu ya kutosha, sio watu wa kwenda kulala kwa Bunge,<br />
kuchukua mishahara mikubwa bure. Tukiangalia tena wangetakiwa wakae kwa miaka mitano ili uchaguzi ufanywe tena.<br />
Ya pili ningependa kuongea juu ya Land issues: Ardhi ya Kenya ingetakiwa kuwa ni ardhi ya Serikali na mwananchi kama<br />
angekuwa na kubwa, aruhusiwe kuwa tu na less than fifty acres. Akiwa na zaidi ya hiyo anyang’anywe, ipewe wale ambao<br />
wanaihitaji ambao hawana land na waendeleze. Kama mtu amepewa na hawezi kuendeleza, ichukuliwe ipewe mwingine<br />
anaweza kuiendeleza.<br />
Kabla hujatoka hapo, tumeambiwa hapa kuna watu kama Wa-Maasai ambao ni wafugaji na wanahitaji ardhi kubwa katika