constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
18<br />
Ma-DC na Ma-PC wapitie Bunge. Wale ambao wanataka hiyo kazi, waombe katika Bunge, ijadilie jambo hilo ili kupatikane<br />
mtu ambaye ana kiwango ambacho kinawezekana na hiyo kazi. Kwa hivyo hayo madaraka yasiwe ya Rais, iwe katika Bunge.<br />
Katika mashamba, kila mtu awe na uhuru wa kununua shamba popote pale katika nchi ya Kenya, mahali ambapo anafaa akae.<br />
Thank you.<br />
Com. Bishop Njoroge: Thank you very much Paul. Jacob Partimo karibu.<br />
Jacob Partimo: Kwa majina mimi naitwa Jacob Partimo Munge, mkaaji wa Loitoktok. Ningependa kuchangia nikisema ya<br />
kwamba, kile ambacho ningependelea Katiba ichukue ni kuwe na Serikali ya Majimbo. Ninaposema Majimbo, nasema<br />
kwanzia ngazi ya Mkoa, hadi katika kijiji. Rasilimali zilizoko, ziweze kutawaliwa na lile jimbo, iweze kusaidia wakaaji wa ile<br />
sehemu. Mauzo za rasilimali hizo, ziuzwe katika vijiji. Wazee wa vijiji wanajua vile watakavyoweza kusaidia kila familia iliyoko<br />
pale.<br />
Ningelipendelea pia katika Katiba ya kwamba, masomo yawe ni ya bure, kwanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu na kuwe -<br />
tuangalie kuna sehemu zilizoendelea tangu wakati wa ukoloni. Unakuta mtoto wa Kajiado ambaye amepata B + hapati nafasi ya<br />
kuingia katika chuo kikuu. Kuingia katika Chuo Kikuu iangaliwe kulingana na kadiri na vile watu walivyo. Pia ningeweza<br />
kusema ya kwamba, Serikali iliyoko katika mamlaka, itupilie kitu kinachoitwa soko huru. Iweze kutunza wananchi wake.<br />
Wanyama pori: wanaua binadamu na malipo ni shilingi elfu thelathini. Napendekeza hizo sheria zinatudhulumu hivyo, zitupiliwe<br />
na iwe ni zaidi ya shilingi milioni tano kwa binadamu mmoja. Pia mifugo na uharibifu wa mashamba uweze kutunzwa. Wawe<br />
compensated. Serikali pia iweze kulinda haki ya kila mmoja. Ninaposema hivyo, nasema ya kwamba sheria za Ma-Chief, ziwe<br />
kama zilivyokuwa hapo awali. Sio ile ya 1998. Ili kuweza kutunza kila mmoja. 75% ya sheria za nchi hii ambayo inahusu<br />
Commissioner wa Ardhi ama Waziri wa Ardhi, aweza kutangaza sehemu kuwa ni sehemu ya wanyama wa pori. Hiyo sector<br />
itupiliwe kwa sababu wanakijiji wanajua manufaa ya hiyo ardhi.<br />
Kazi: Kazi, kulingana majimbo - mahali ambao umetoka, upate kazi pale lakini wataalamu wawekwe katika Serikali kuu.<br />
Asilimia sabini na tano, ipewe wenyeji. Rasilimali zilizoko katika sehemu, wananchi waweze kuwa na uhuru wa kuziuza. Kwa<br />
mfano mali wauze na wafanye matumizi katika kujiendeleza hali yao.<br />
Habari ya uuzaji wa ardhi: Nilisema ya kwama wanakijiji waweze kutawalana ndio tumesema Serikali ya Majimbo itoke<br />
kwanzia vijijini mpaka mkoani. Asante.<br />
Com. Bishop Njoroge: Umesema kwamba rasilimali ziwe za jimbo na jimbo litawale hizo rasilimali. Unaweza kutuambia,<br />
kama tutakuwa na Central Government, na Central Government itakuwa ni nini? Pia ningetaka kukuuliza, kama yale maji<br />
inakunyiwa Nairobi, inatoka Mt. Kenya na watu wa Central Province wakipewa ruhusa ya kutawala hayo maji, inaweza