27.11.2014 Views

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

27<br />

Kuhusu masomo: Masomo kulingana na vile ninaona ya kwamba, masomo katika Kenya tunaambiwa ni ya bure lakini tunaona<br />

bado haijakuwa ya bure. Masomo tungependa iwe ya bure kwa sababu watu wengi katika Kenya hawana rasilimali, hawana<br />

mapato. Na tunaona watoto wao, hasa ndio unakuta wanapita katika shule. Lakini kwa sababu ya kuwa hawana mapato,<br />

watoto hao wataendelea na masomo. Kwa hivyo masomo iwe ya bure.Vile vile, matibabu. Tunaona ugonjwa hauchagui tajiri<br />

kwa sababu ndio ana pesa ya kujitibu. Tajiri na maskini wanapatwa na ugonjwa hali sawa. Kwa hivyo ningependekeza<br />

matibabu yawe ya bure. Ili watu waweze kuokolewa maisha yao.<br />

Kuhusu ardhi, kusema ukweli ardhi ya Wamaasai, imenyakuliwa kwa njia ambayo hatujui imetokana na nini. Kwa sababu<br />

wanyama sio eti kwamba wanyama wanazaliwa Maasaini peke yake. Lakini tunaona ya kwamba ardhi yetu iliyonyakuliwa kam<br />

Amboseli na Tsavo West National Park, tunaona ni ardhi ambayo ingeweza kusaidia wananchi hasa katika hali ya kilimo na<br />

kupanda miti rasilimali ya aina mingi, tunaona ardhi yetu imenyakuliwa ambayo tunaweza pata manufaa nayo. Ningependekeza<br />

hiyo ardhi irudishwe kwa wenyewe. Maana tangu Wamasai walipopatikana, hakuna siku Maasai amekuwa adui na mnyama na<br />

ndio maana kwao ndio wanyama wanabaki. Na watajua vile wataendelea kukaa na wanyama.<br />

Kuhusu MPs, ningependekeza kuwa, uchaguzi unap<strong>of</strong>anyika, Mbunge achunguzwe na watu wake kwa miaka miwili,<br />

akionekana hakuna kazi anaweza fanya, itolewe kura ya kusipokuwa na imani naye, aondolewe. Ili wananchi wasiendelee<br />

kuumia kwa muda huo wote. Kwa sababu kama wananchi watakuwa wakikaa kwa miaka mitano katika taabu, hata mwezi<br />

mmoja ni shida licha ya miaka mitano. Unakuta…..<br />

Com. Bishop Njoroge: Nakupatia dakika moja.<br />

Isaiah Ole Samana: Hata hivyo nimemaliza. Kwa hivyo ningependekeza ya kwamba iendelee. Kuhusu mambo ya Ma-Chiefs,<br />

Ma-Chiefs waendelee kwa sababu wao ndio wanaelewa shida na taabu ya familia zile ziko karibu na wao. Wao ndio wazaliwa<br />

na wanajua shida, na umaskini na unyanyasaji wa wale watu. Kwa hivyo ningependekeza Chief aendelee kubaki, Provincial<br />

Administration yote kutoka Sub-Chiefs, mpaka Province iendelee. Asante.<br />

Com. Lethome: Ngojea kidogo kuna swali hapa. Kuhusu zile National Parks, wasema ardhi ya Wamaasai, warudishiwe<br />

Amboseli na Tsavo. Wa-Sumburu nao wakisema yao warudishiwe, Meru National park warudishiwe. Unapendekeza yaani<br />

Kenya tusiwe na any National park ama vipi? Kwa sababu it has to be curved out kutoka kwenye ardhi ya watu fulani. Kwa<br />

hivyo unapendekeza katika Kenya tusiwe na National Parks zozote ama vipi?<br />

Com. Bishop Njoroge: Ningetaka kuongeza hapo, katika mapato mengi kutoka National Park, zinaenda kwa Central<br />

Government na ndio expenditure ya Serikali inatokana hapo. Hivi ni kusema kwamba mapato hayo sasa haitakuwa ya<br />

CentalGovernment, ungetaka iwe ya Jimbo, kwa hivyo Central Government itafute njia kufanya mapato yake.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!