constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
27<br />
Kuhusu masomo: Masomo kulingana na vile ninaona ya kwamba, masomo katika Kenya tunaambiwa ni ya bure lakini tunaona<br />
bado haijakuwa ya bure. Masomo tungependa iwe ya bure kwa sababu watu wengi katika Kenya hawana rasilimali, hawana<br />
mapato. Na tunaona watoto wao, hasa ndio unakuta wanapita katika shule. Lakini kwa sababu ya kuwa hawana mapato,<br />
watoto hao wataendelea na masomo. Kwa hivyo masomo iwe ya bure.Vile vile, matibabu. Tunaona ugonjwa hauchagui tajiri<br />
kwa sababu ndio ana pesa ya kujitibu. Tajiri na maskini wanapatwa na ugonjwa hali sawa. Kwa hivyo ningependekeza<br />
matibabu yawe ya bure. Ili watu waweze kuokolewa maisha yao.<br />
Kuhusu ardhi, kusema ukweli ardhi ya Wamaasai, imenyakuliwa kwa njia ambayo hatujui imetokana na nini. Kwa sababu<br />
wanyama sio eti kwamba wanyama wanazaliwa Maasaini peke yake. Lakini tunaona ya kwamba ardhi yetu iliyonyakuliwa kam<br />
Amboseli na Tsavo West National Park, tunaona ni ardhi ambayo ingeweza kusaidia wananchi hasa katika hali ya kilimo na<br />
kupanda miti rasilimali ya aina mingi, tunaona ardhi yetu imenyakuliwa ambayo tunaweza pata manufaa nayo. Ningependekeza<br />
hiyo ardhi irudishwe kwa wenyewe. Maana tangu Wamasai walipopatikana, hakuna siku Maasai amekuwa adui na mnyama na<br />
ndio maana kwao ndio wanyama wanabaki. Na watajua vile wataendelea kukaa na wanyama.<br />
Kuhusu MPs, ningependekeza kuwa, uchaguzi unap<strong>of</strong>anyika, Mbunge achunguzwe na watu wake kwa miaka miwili,<br />
akionekana hakuna kazi anaweza fanya, itolewe kura ya kusipokuwa na imani naye, aondolewe. Ili wananchi wasiendelee<br />
kuumia kwa muda huo wote. Kwa sababu kama wananchi watakuwa wakikaa kwa miaka mitano katika taabu, hata mwezi<br />
mmoja ni shida licha ya miaka mitano. Unakuta…..<br />
Com. Bishop Njoroge: Nakupatia dakika moja.<br />
Isaiah Ole Samana: Hata hivyo nimemaliza. Kwa hivyo ningependekeza ya kwamba iendelee. Kuhusu mambo ya Ma-Chiefs,<br />
Ma-Chiefs waendelee kwa sababu wao ndio wanaelewa shida na taabu ya familia zile ziko karibu na wao. Wao ndio wazaliwa<br />
na wanajua shida, na umaskini na unyanyasaji wa wale watu. Kwa hivyo ningependekeza Chief aendelee kubaki, Provincial<br />
Administration yote kutoka Sub-Chiefs, mpaka Province iendelee. Asante.<br />
Com. Lethome: Ngojea kidogo kuna swali hapa. Kuhusu zile National Parks, wasema ardhi ya Wamaasai, warudishiwe<br />
Amboseli na Tsavo. Wa-Sumburu nao wakisema yao warudishiwe, Meru National park warudishiwe. Unapendekeza yaani<br />
Kenya tusiwe na any National park ama vipi? Kwa sababu it has to be curved out kutoka kwenye ardhi ya watu fulani. Kwa<br />
hivyo unapendekeza katika Kenya tusiwe na National Parks zozote ama vipi?<br />
Com. Bishop Njoroge: Ningetaka kuongeza hapo, katika mapato mengi kutoka National Park, zinaenda kwa Central<br />
Government na ndio expenditure ya Serikali inatokana hapo. Hivi ni kusema kwamba mapato hayo sasa haitakuwa ya<br />
CentalGovernment, ungetaka iwe ya Jimbo, kwa hivyo Central Government itafute njia kufanya mapato yake.