19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

12<br />

muchana, warizi wa mali zako za milele. Utajirini ya huruma yako, ukumbuke, ee<br />

Bwana, watu wako wote, wenye kuwa hapa wanaomba pamoja nasi, na ndugu zetu wote,<br />

nchini na baharini ambao po pote panapotandaza ufalme wako, wanasihi mapendo yako<br />

kwa ajili ya wanadamu. Gawanya kwa wote huruma yako kubwa, ili tukiokolewa, roho<br />

na mwili, tuweze na uhuru wote kutukuza na kusifu milele, jina lako nzuri na tukukuza,<br />

Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />

Sala wa tano ku Ibada ya Asubui.<br />

Hazina ya chemchem ya uzuri wote isiokauka, Baba Mtakatifu, mtenda maajabu,<br />

Mwenyezi, Rabi wa ulimwengu, wote tunakuabudu na tunakusihi, tukiita rehema na<br />

huruma yako kwa kutusaidia na kutukinga ku uzaifu wetu; utukumbuke, ee Bwana,<br />

tunakuomba pokea maombi yetu ya asubui kama uvumba mbele yako, ili hata mmoja kati<br />

yetu asikataliwe, lakini utuchunge sisi wote katika huruma yako. Kumbuka, ee Bwana,<br />

wale wanaokesha na kuimba sifa yako, na kwa sifa ya Mwana wako wa pekee, Mungu<br />

wetu na kwa Roho yako Mtakatifu. Uwe kwao, msaada na mulinzi; upokee malalamiko<br />

yao juu ya altare yako ya kimbingu na ya kiroho. Kwani uko Mungu wetu, na<br />

tunakutukuza Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, sasa na siku zote hata milele na milele.<br />

Amina.<br />

Sala wa saba ku Ibada ya Asubui.<br />

Ee Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, umetuamusha kitandani chetu na<br />

umetukusanya kwa saa ya maombi: kubali kufunikiza midomo yetu, pokea shukrani yetu<br />

na utufundishe mapenzi yako; kwa sababu hatujuwi ginsi ya kukuomba, isipokuwa kama<br />

wewe mwenyewe, Bwana, hautuongozi kwa Roho yako Mtakatifu. Tena, tunakuomba<br />

hata na hii saa, hatukutenda zambi, kwa neno, kwa vitendo ao kwa mawazo, kwa kusudi<br />

ao kwa siyo kusudi, ondoa, rejeza na samehe. Kwani kama unahukumu makosa, Bwana,<br />

nani basi ataishi? Lakini karibu nawe kuna wokovu. Wewe peke ndiwe Mtakatifu, wewe<br />

msaada wa nguvu na mlinzi wa mioyo yetu, kwako, ee Bwana, kuinua wimbo wetu<br />

wakati wowote ili uwezo wa utawala wako ubarikiwe na utukuzwe Baba, Mwana na<br />

Roho Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />

Sala wa kumi na mbili ku Ibada ya Asubui.<br />

Tunakukuza, tunakuimbia, tunakubariki, tunakushukuru, ee Mungu wa mababu<br />

zetu kwani umetenga kivuli cha usiku na umetuonyesha tena mwangaza wa muchana;<br />

lakini tunasihi wema wako, utupe usamehe wa zambi, na katika huruma yako kubwa,<br />

upokee maombi yetu; kwani tunakimbilia kwako, Mungu wa huruma na wa uwezo;<br />

angazia mioyoni mwetu jua kweli la haki yako; angazia usikilizi wetu na ulinde tamaa<br />

zetu za mwili; ili tupate kutembea wastahilivu, katika mchana, katika njia ya amri zako<br />

na tukihukumiwa wastahilivu kwa kufurahi katika nuru tupate kufika ku uzima wa<br />

milele, kwa sababu karibu nawe kuna chemchem ya uzima. Kwani, wewe ndiwe Mungu<br />

wetu, na tunakutukuza Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele<br />

na milele. Amina.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!