You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
12<br />
muchana, warizi wa mali zako za milele. Utajirini ya huruma yako, ukumbuke, ee<br />
Bwana, watu wako wote, wenye kuwa hapa wanaomba pamoja nasi, na ndugu zetu wote,<br />
nchini na baharini ambao po pote panapotandaza ufalme wako, wanasihi mapendo yako<br />
kwa ajili ya wanadamu. Gawanya kwa wote huruma yako kubwa, ili tukiokolewa, roho<br />
na mwili, tuweze na uhuru wote kutukuza na kusifu milele, jina lako nzuri na tukukuza,<br />
Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
Sala wa tano ku Ibada ya Asubui.<br />
Hazina ya chemchem ya uzuri wote isiokauka, Baba Mtakatifu, mtenda maajabu,<br />
Mwenyezi, Rabi wa ulimwengu, wote tunakuabudu na tunakusihi, tukiita rehema na<br />
huruma yako kwa kutusaidia na kutukinga ku uzaifu wetu; utukumbuke, ee Bwana,<br />
tunakuomba pokea maombi yetu ya asubui kama uvumba mbele yako, ili hata mmoja kati<br />
yetu asikataliwe, lakini utuchunge sisi wote katika huruma yako. Kumbuka, ee Bwana,<br />
wale wanaokesha na kuimba sifa yako, na kwa sifa ya Mwana wako wa pekee, Mungu<br />
wetu na kwa Roho yako Mtakatifu. Uwe kwao, msaada na mulinzi; upokee malalamiko<br />
yao juu ya altare yako ya kimbingu na ya kiroho. Kwani uko Mungu wetu, na<br />
tunakutukuza Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, sasa na siku zote hata milele na milele.<br />
Amina.<br />
Sala wa saba ku Ibada ya Asubui.<br />
Ee Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, umetuamusha kitandani chetu na<br />
umetukusanya kwa saa ya maombi: kubali kufunikiza midomo yetu, pokea shukrani yetu<br />
na utufundishe mapenzi yako; kwa sababu hatujuwi ginsi ya kukuomba, isipokuwa kama<br />
wewe mwenyewe, Bwana, hautuongozi kwa Roho yako Mtakatifu. Tena, tunakuomba<br />
hata na hii saa, hatukutenda zambi, kwa neno, kwa vitendo ao kwa mawazo, kwa kusudi<br />
ao kwa siyo kusudi, ondoa, rejeza na samehe. Kwani kama unahukumu makosa, Bwana,<br />
nani basi ataishi? Lakini karibu nawe kuna wokovu. Wewe peke ndiwe Mtakatifu, wewe<br />
msaada wa nguvu na mlinzi wa mioyo yetu, kwako, ee Bwana, kuinua wimbo wetu<br />
wakati wowote ili uwezo wa utawala wako ubarikiwe na utukuzwe Baba, Mwana na<br />
Roho Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
Sala wa kumi na mbili ku Ibada ya Asubui.<br />
Tunakukuza, tunakuimbia, tunakubariki, tunakushukuru, ee Mungu wa mababu<br />
zetu kwani umetenga kivuli cha usiku na umetuonyesha tena mwangaza wa muchana;<br />
lakini tunasihi wema wako, utupe usamehe wa zambi, na katika huruma yako kubwa,<br />
upokee maombi yetu; kwani tunakimbilia kwako, Mungu wa huruma na wa uwezo;<br />
angazia mioyoni mwetu jua kweli la haki yako; angazia usikilizi wetu na ulinde tamaa<br />
zetu za mwili; ili tupate kutembea wastahilivu, katika mchana, katika njia ya amri zako<br />
na tukihukumiwa wastahilivu kwa kufurahi katika nuru tupate kufika ku uzima wa<br />
milele, kwa sababu karibu nawe kuna chemchem ya uzima. Kwani, wewe ndiwe Mungu<br />
wetu, na tunakutukuza Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele<br />
na milele. Amina.