You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
57<br />
nifunguwe milango iliyo paka wewe peke uliumba kwa kuingia na mapendo yako<br />
imara. Utaingia na kwangaza mawazo yangu mabaya, ninasadiki kweli haukufukuza<br />
muke mtenda zambi aliyekuja kwako na machozi mbele yako, haukusukuma nyuma<br />
mkosefu anaotubu, wala haukumkatalia mwivi wakati walipotambua ufalme wako; ama<br />
haukumzarau aliyekuja kutubu haukumwacha, lakini wote waliyekuja kwako kutubu,<br />
uliwaweka fasi ya warafiki wako, wewe mbarikiwa pekee wakati wowote, sasa na milele<br />
bila mwisho. Amina.<br />
<strong>SALA</strong> 5<br />
<strong>YA</strong>LE<strong>YA</strong>LE <strong>YA</strong> MTAKATIFU YOANNE KRISOSTOMO<br />
Bwana Yesu Kristu, unisafishe mimi mkosefu na mtumishi mwovu. Sahau na<br />
unisamehe makosa na zambi niliyokutukana nayo tangu utoto wangu mpaka siku ya leo<br />
na saa hii: Isipokuwa kwa akili ao kwa upiswa, kwa sauti kwa vitendo ao kwa mawazo,<br />
kwa zoezo ao maana yangu yote. Kwa maombezi ya yule aliyekuzaa bila mbegu, Bikira<br />
Maria Mama yako, yeye peke kitumaini chetu kisichochanganyikwa, msaada na wokovu<br />
wangu; unirudishe mstahilivu nikomunike bila hukumu ku maisha yasiyo mwisho, yenye<br />
uzima na maumbo ya maondoleo ya zambi zangu, na uzima wa milele kwa utakaso,<br />
mwangaza, utunzo na afya ya moyo na mwili wangu kwa maondoleo na maangamizi ya<br />
mawazo yangu mabaya, ya kusudi na kwa mawazo yangu ya ngiza ililetwa na roho za<br />
ngiza na kali. Kwa kuwa kwako ni utawala, uwezo na sifa; Utukufu na ibada kwa Baba<br />
na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu, sasa na siku zote hata milele na milele. Amina.<br />
<strong>SALA</strong> 6<br />
<strong>YA</strong> MTAKATIFU YOANNE DAMASCENI.<br />
Ee Rabi, Bwana wetu Yesu Kristu, Mungu wetu, wewe peke una uwezo wa<br />
kuondoa zambi, wewe rafiki wa wanadamu, unisamehe zambi zangu zote ninazofahamu<br />
na nisizofahamu, nistahili bila kuhukumiwa, niungane na mafumbo yako Matakatifu ya<br />
bumungu yenye kuleta uzima. Bila kuvuta azabu, masumbuko na kuongeza zambi zangu,<br />
nitakaswe na niwe rahani ya uzima wa ufalme utakayokuja, ukingo na msaada zitawanye<br />
wadui zangu na ziondoe zambi zangu nyingi. Kwa sababu uko Mungu Mwema, wa<br />
huruma na wa mapendo ya wanadamu na tunakushukuru na Baba, na Mwana na Roho<br />
Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.<br />
<strong>SALA</strong> 7<br />
<strong>YA</strong> SIMEONI MUTHEOLOGO MUP<strong>YA</strong><br />
Kwa midomo iliochafuka, kwa roho mubaya, kwa ulimi ulioambukizwa, kwa<br />
moyo muchafu, kamata sala, ee Kristu wangu, usinifukuze mbali nawe, kwa vitendo na<br />
mifano yangu mibaya, hata kwa ukosefu wangu wa haya, unisaidie niseme kwa uhodari,<br />
ee Kristu wangu, yote yaliyo ndani ya roho yangu, lakini ni vizuri zaidi unifundishe,<br />
yaliyo ya kutenda na yaliyo yakunena. Nilifanya zambi kuliko zile za mzinifu, ambaye<br />
aliposikia wapi unapoikala, alinunua manukato, alipofika akapakaa kwa uhodari, miguu<br />
yako, Kristu wangu, ya Rabi na ya Mungu wangu.<br />
Kama vile haukumufukuze yule, aliyejikaribia kwa haraka kwa haraka. Pamoja<br />
nami mwana, usinifukuze mbali nawe, unipe miguu yako nitakayogusa na kuyabusu, na<br />
kwa mitoni mingi ya machozi, kama manukato ya bei mingi, nitakuja kwa uhodari<br />
kukupakaa. Kwa machozi yangu unisafishe mwana, unitakase, ee Bwana. Uniachilie<br />
ukosefu wangu; unipe rehema yako. Unapojua idadi ya zambi zangu, unajua madonda<br />
yangu; na unajua maumivu yangu; lakini unapojua imani yangu, unajua haraka yangu, na