Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
95<br />
Ni tangu Siku Kuu ya kuzaliwa kwake Bwana Yesu Kristu tarehe 25<br />
Desemba mpaka tarehe 6 Januari. Tunakula vyakula vyote, paka siku moja mbele ya<br />
Epifania ya kristu tunafunga sana.<br />
2. Juma ya Diakenisimos. Ni Juma kisha Ufufuo wa Bwana Yesu; inaanza siku ya<br />
Ufufuo wa Kristu mpaka siku ya Bwana ya Mtume Thomas.<br />
3. Tangu siku ya Bwana ya Pentikosti mpaka siku ya Bwana ya Watakatifu wote.<br />
4. Juma tatu za wakati wa Triode: Juma ya kwanza ni makumbusho ya Mtoza-<br />
Kodi na Mfarisayo; tunakula vyakula vyote kila siku. Juma ya mbili ni makumbusho ya<br />
Mwana Mpotevu; tunakula vyakula vyote. Mu Kazi Tatu na mu Kazi Tano tunafunga,<br />
hatukule mafuta.<br />
Juma ya Tatu ni makumbusho ya Jivini (Tirofagi); tunakula yote, lakini hapana<br />
nyama. Tumekuisha kula nyama mpaka JUma ya Apokreo. Tokea hii Juma mpaka Juma<br />
ya Jivini hatukule nyama, lakini tunakula chakula ingine yote.<br />
Kama tulivyosema, kifingo cha mu Kazi tatu na mu kazi tano ni cha mwaka<br />
mzima, nikusema haipaswe kula chakula na mafuta. Lakini kama tuko na shangilio<br />
kubwa mu hii masiku tutakula ao samaki, ao paka mafuta na vinyo.<br />
Tunakula samaki wakati wa siku Kuu za mashangilio ya Mzazi-Mungu na ya<br />
Yoane Nabii Mtangulizi na Mbatizaji. Makumbusho ya Watakatifu wengine<br />
tunashangilia na mafuta na vinyo.<br />
Tena tunakula samaki mu Kazi Tatu kwa Siku Kuu katikati ya Pentikosti, na mu<br />
Kazi Tatu ya Sindikizo ya Ufufuo wa Bwana Yesu Kristu, siku moja mbele ya Siku Kuu<br />
ya kupenda kwake Bwana Yesu Kristu mbinguni.<br />
Kisha tutaonyesha vizuri kila mwezi siku gani tutafunga na chakula gani tutakula.<br />
MWEZI <strong>YA</strong> JANUARI.<br />
Tarehe 6: Ni Epifania ya Kristu. Tunakula yote.<br />
Tarehe 7: Baraza ya Yoane Mtangulizi. Tunakula samaki.<br />
11 Makumbusho ya Mt. Theodosios. Tunakula mafuta na vinyo.<br />
16. Usujudu ya monyororo ya Mtume Petro. Tunakula mafuta na vinyo.<br />
17. Ya Mtakatifu Antonios. Tunakula mafuta na vinyo.<br />
18. Ya Watakatifu Athanasios na Kirillos. Mafuta na vinyo.<br />
20. Ya Mtakatifu Efthimios mukubwa. Mafuta na vinyo.<br />
22 Ya Mutume Timotheos na Mushahindi Anastasios ya Persia. Mafuta na vinyo.<br />
25 Ya Mtakatifu Askofu Grigorie mutheologo. Mafuta na vinyo.<br />
27. Kuhamisha Mifupa ya Mt. Yoane Krisostomo. Mafuta na vinyo.<br />
30. Makumbusho ya Maaskofu Wakubwa tatu, Basile Mkuu, Grigorie na Yoane<br />
Krisostome. Mafuta na vinyo.<br />
MWEZI <strong>YA</strong> FEBRUARI<br />
2. Mapokeleo ya Bwana Yesu Kristu mikononi mwa Mt. Simeoni. Tunakula<br />
samaki.<br />
8. Mtakatifu Mshahidi askari Mkubwa Theodoros. Mafuta na vinyo.<br />
10. Mt. Haralambos Askofu na Shahindi. Mafuta na vinyo.<br />
11. Mtakatifu Askofu Vlasios. Mafuta na vinyo.<br />
17. Mt. shahindi Theodoros wa Tironi. Mafuta na vinyo.<br />
24. Kupata Kichwa cha Mt. Yoane Mutangulizi. Mafuta na vinyo.