You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>SALA</strong> <strong>YA</strong> CHAKULA<br />
14<br />
Chakula cha asubui<br />
1. Mbele ya chakula<br />
Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu. Sasa na siku zote hata<br />
milele na milele. Amina. Bwana hurumia (mara tatu). Rabi mtakatifu barikia:<br />
Ee Bwana Yesu Kristu, bariki chakula na kinywaji cha watumishi wako, kwani<br />
wewe peke yako ni Mtakatifu daima, sasa na siku zote hata milele. Amina.<br />
Kama hakuna padri tunasema paka sala ya padri bila kubariki.<br />
Kisha chakula cha asubui tunasema ivi:<br />
Kwa maombezi ya Wapadri wetu Watakatifu.. .<br />
Chakula cha katikati ya muchana (midi)<br />
Mbele ya chakula<br />
Baba yetu.. . Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote.. . Bwana hurumia<br />
(mara tatu). Ee Rabi mtakatifu barikia.<br />
Padri: Ee Bwana Yesu Kristu, bariki chakula na kinywaji.. .<br />
Kisha hii chakula tunasema:<br />
Ee Kristu Mungu wetu, tunakushukuru kwa maana ulitushibisha na vitu nyako vya<br />
inchi; usikatae kutupatia na ufalme wako wa mbinguni, lakini kama ulivyokuwa katikati<br />
ya wafwasi wako kwa kuwapa amani, vile, ee Mwokozi, kuja pia na kwa sisi na utuokoe.<br />
Amina.<br />
Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote.. . Bwana hurumia<br />
(mara tatu). Ee Rabi mtakatifu barikia:<br />
Padri: Ee Kristu Mungu wetu, bariki mabaki ya hii chakula iliyo mezani, uiongeze<br />
kwa hii nyumba na kwa dunia yote, wewe ni Mungu Mwema, Mrahimu na Mpenda<br />
Wanadamu. Kwa maombezi ya Wapadri wetu.. . .<br />
Kama hakuna padri, kisha Bwana hurumia (mara tatu), tunasema:<br />
Kwa maombezi.. .<br />
Chakula cha mangaribi<br />
Mbele ya chakula<br />
Maskini watakula na kushiba, wenye kumutafuta Bwana watamusifu na mioyo yao<br />
iishi kwa milele. Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote.. . Bwana hurumia