You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
26<br />
APOLITIKIA NA THEOTOKIA ZA UFUFUO WA BWANA<br />
YESU KRISTU<br />
Elezo: Kila Juma tunaanza Ibada yote toka Ibada ya Muposho Mangaribi. Kila<br />
Juma tunageuza sauti. Sauti yote ni Mnane. Kwa kila sauti kuwa wimbo wa Ufufuo na<br />
Theotokion na wimbo wa Ipakoi mbalimbali. Ni vizuri sana kama waaminifu wetu wanafunza<br />
bila kitabu kusema na kuimba Apolitikia ya Ufufuo wa Bwana Yesu Kristu. Sauti ya kwanza.<br />
APOLITIKION<br />
Sauti ya kwanza<br />
Wakati jiwe lilitiliwa muhuri na wayuda, na wakati Waaskari walichunga mwili<br />
wako wasio doa, ulifufuka siku ya tatu ee Mwokozi, uliupatia ulimwengu uzima. Kwa hii<br />
ezi mbingu ilipaza sauti kwa wewe mpaji wa uzima; utukufu kwa ufufuo wako, ee Kristu,<br />
utukufu kwa ufalme wako, utukufu kwa shuruli yako ya ulimwengu, wewe peke<br />
Mpenda-Wanadamu.<br />
THEOTOKION<br />
Wakati Gabrieli alisema kwako Bikira, Salamu, kwa sauti; Rabi wa wote alichukua<br />
mwili, ndani yako safina takatifu, sawa mwenye haki Daudi alivyosema. Ulionekana<br />
kuwa munene sana kuliko mbingu, kwa sababu ulichukuwa Muumba wako. Utukufu kwa<br />
yule alikaa ndani yako; utukufu kwa huyu alitoka kwako; utukufu kwa huyu alitupatia<br />
uhuru juu ya uzazi wako.<br />
IPAKOI<br />
Toba ya Munyanganyi ikashurtisha Paradizo, maombolezo ya Wabebaji manukato<br />
ya katangaza furaha: Ee Kristu Mungu wetu, ulifufuka kwa kuleta ku dunia neema<br />
kubwa.<br />
APOLITIKION<br />
Sauti ya pili<br />
Wakati ulishuka ku mauti, uzima usiyo kufa, hapo uliregeza kuzimu, kwa unara wa<br />
umungu wako; na wakati ulifufua wafu waliyolala kuzimuni, ezi zote za mbinguni<br />
zilipaza sauti; Mpaji wa uzima Kristu, ee Mungu wetu, utukufu kwako.