You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
85<br />
WIMBO INGINE<br />
Sauti ya sita<br />
Utuhurumie, ee Bwana, utuhurumie; Kwa kuwa sisi watu wenye zambi, hakuna<br />
tena yoyote kukutolea, ila ombi hii tunatoa kwako, uliye Rabi, utuhurumie.<br />
Utukufu kwa Baba na kwa Mwana.. .<br />
Ee Bwana, utuhurumie kwa kuwa tunatengemea kwako. Utukaribie sana wala<br />
kuzikumbuka zambi zetu, lakini hata sasa utwangalie kama mwenye huruma, ukatuokoe<br />
na madui zetu. Wewe, u Mungu wetu, tena sisi ni watu wako, sisi wote ni viumbe vya<br />
mikono yako na jina lako tunaliita.<br />
Sasa na siku zote.. . THEOTOKION<br />
Utufungulie lango wa huruma yako, ee Mzazi Mungu Mbarikiwa.<br />
Tunayokutumainia wewe, hatutaanguka. Kwako tutaepuka mateso, kwa kuwa wewe ni<br />
wokovu wa amini wa wa Kristu.<br />
Bwana hurumia (Mara makumi Ine).<br />
Utukufu kwa Baba.. . Sasa na siku zote.. . Uliye wa tamani.. .<br />
Mungu, Rabi, Baba Mwenyezi; Mwokozi, Mwana wa pekee, Yesu Kristu na Roho<br />
Mtakatifu, umungu moja, nguvu moja, unihurumie; wakati wa mwisho uniokoe mimi<br />
mukosefu wako, kwani umetukuzwa milele na milele. Amin.<br />
Njooni tumwinamie na tumusujudu Mungu Mfalme wetu.<br />
Njooni tumwinamie Kristu aliye Mfalme wetu.<br />
Njooni tumwinamie yeye Kristu aliye Mfalme na Mungu wetu.<br />
ZABURI 69 (70).<br />
Ee Mungu, uniokoe; unisaidie mbio, ee Bwana. Wapate haya na kufazaishwa<br />
wanaotafuta nafsi yangu; warudishwe nyuma na kuzarauliwa wanaofurahi kwa kuumia<br />
kwangu. Warudishwe nyuma kwa ajili ya haya yao wanaosema: Ewe, ewe. Wote<br />
wanaokutafuta washangilie na kukufurahia; nao wanaopenda wokovu wako waseme<br />
daima: Mungu atukuzwe. Lakini mimi ni masikini na mwenye hitaji unisaidie mbio, ee<br />
Mungu; wewe ni musaidia wangu na mwokozi wangu; ee Bwana, usikawie.<br />
ZABURI 142 (143)<br />
Sikia maombi yangu, ee Bwana, usikilize kusihi kwangu; katika uaminifu wako<br />
unijibu, katika haki yako. Usihukumu mutumishi wako; maana machoni mwako hakuna<br />
mutu aliye hai atahesabiwa haki. Maana adui amefuata nafsi yangu; amepiga uzima<br />
wangu chini hata udongo. Amenikalisha katika pahali pa giza, kama wale waliokufa<br />
zamani. Kwa hivi roho yangu imezimia ndani yangu; Moyo wangu ndani yangu ni ukiwa.<br />
Ninakumbuka siku za kale; ninafikili matendo yako yote; ninawaza kazi ya mikono yako.<br />
Ninakunyoshea mikono yangu; nafsi yangu inaona kiu kwa wewe, kama inchi<br />
inayochoka. Fanya mbio kwa kunijibu, ee Bwana; roho yangu inazimia; usinifichie uso<br />
wako; nisiwe kama wao wanaoshuka shimoni. Unifanye kusikia wema wako asubui; kwa<br />
maana ninakutumainia wewe; unijulishe njia nitakayoikwenda; kwa maana<br />
ninakunyanyulia nafsi yangu. Uniponyeshe, ee Bwana, na adui zangu, ninakukimbilia<br />
unifiche. Unifundishe kufanya mapenzi yako; kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu;<br />
Roho yako ni mwema; uniongoze katika inchi ya haki. Unipatize uzima, ee Bwana, kwa<br />
ajili ya jina lako; kwa haki yako utoe nafsi yangu katika taabu. Na kwa wema wako