You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
17<br />
Zaburi I42<br />
Kwa sauti yangu ninalilia Bwana; kwa sauti yangu ninasihi Bwana.<br />
Ninamwanga mashitaki yangu mbele yake; ninamwonyesha taabu yangu.<br />
Wakati nilipozima roho, umejua njia yangu.<br />
Katika njia ninapokwenda wamenifichia mutego.<br />
Utazame kwa mukono wa kuume, uone, kwa maana hakuna mutu anayenijua:<br />
Makimbilio yamenipotea; hakuna mutu anayekumbuka nafsi yangu.<br />
Nikalia kwako, ee Bwana; Ninasema: wewe ni kimbilio langu, sehemu yangu<br />
katika inchi yao waliohai.<br />
Usikilize kilio changu; kwa maana nimeshushwa chini sana:<br />
Uniponyeshe nao wanaonifuata; kwa maana wao wana nguvu kuliko mimi<br />
Toa nafsi yangu katika kifungo, ili nishukuru jina lako.<br />
Wenye haki watanizunguka; kwa kuwa wewe utanitendea kwa ukarimu.<br />
Zaburi I3O Kuomba usamehe.<br />
Toka vilindini nimekulilia, ee Bwana. Bwana, sikia sauti yangu.<br />
Masikio yako yasikilize sauti ya kusihi kwangu.<br />
Kama wewe Bwana, ukihesabu maovu, ee Bwana, nani atakayesimama? Lakini<br />
usamehe pamoja nawe, ili uogopwe.<br />
Ninangojea Bwana, nafsi yangu inangoja, na ninatarajia neno lake.<br />
Nafsi yangu inangoja Bwana, kuliko walinzi wanaongoja asubuhi; ndiyo, walinzi<br />
wanaongoja asubui. Ee Israeli, utarajie Bwana.<br />
Maana pamoja na Bwana ni rehema, na pamoja naye ukombozi mwingi. Naye<br />
atakomboa Israeli na maovu yake yote.<br />
Zaburi 117<br />
Musifu Bwana, ninyi mataifa yote; mumutolee sifa, ninyi watu wote.<br />
Maana rehema yake kwetu ni kubwa; na kweli ya Bwana inakaa milele. Musifu<br />
Bwana.<br />
Utukufu kwa Baba, na kwa Mwana, na kwa Roho Mtakatifu, sasa na siku zote hata<br />
milele na milele.<br />
Kisha kusoma ile zaburi tunaimba hii sala:<br />
Mwangaza upole (ilaron) ya sifa mtakatifu, ya Baba Musiye kufa wa mbinguni,<br />
mtakatifu na heri, ee Yesu Kristo, kufika kuingia kwa jua, kuangalia mwangaza wa<br />
mangaribi; tunasifu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu Mungu mmoja, uko kweli wakati<br />
wote. Kukuimbia kwa ma sauti nzuri, ee Mwana wa Mungu, chemchem ya uzima,<br />
ulimwengu utaita sifa yako.<br />
Kisha tunaimba Prokimenon ya kila siku ya Juma:<br />
Siku ya Mungu Mangaribi. Sauti ya Mnane.<br />
Tazama ninyi munaobariki Bwana, ninyi watumishi wote wa Bwana<br />
(Mara tatu)