19.03.2015 Views

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

06KITABU YA SALA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

17<br />

Zaburi I42<br />

Kwa sauti yangu ninalilia Bwana; kwa sauti yangu ninasihi Bwana.<br />

Ninamwanga mashitaki yangu mbele yake; ninamwonyesha taabu yangu.<br />

Wakati nilipozima roho, umejua njia yangu.<br />

Katika njia ninapokwenda wamenifichia mutego.<br />

Utazame kwa mukono wa kuume, uone, kwa maana hakuna mutu anayenijua:<br />

Makimbilio yamenipotea; hakuna mutu anayekumbuka nafsi yangu.<br />

Nikalia kwako, ee Bwana; Ninasema: wewe ni kimbilio langu, sehemu yangu<br />

katika inchi yao waliohai.<br />

Usikilize kilio changu; kwa maana nimeshushwa chini sana:<br />

Uniponyeshe nao wanaonifuata; kwa maana wao wana nguvu kuliko mimi<br />

Toa nafsi yangu katika kifungo, ili nishukuru jina lako.<br />

Wenye haki watanizunguka; kwa kuwa wewe utanitendea kwa ukarimu.<br />

Zaburi I3O Kuomba usamehe.<br />

Toka vilindini nimekulilia, ee Bwana. Bwana, sikia sauti yangu.<br />

Masikio yako yasikilize sauti ya kusihi kwangu.<br />

Kama wewe Bwana, ukihesabu maovu, ee Bwana, nani atakayesimama? Lakini<br />

usamehe pamoja nawe, ili uogopwe.<br />

Ninangojea Bwana, nafsi yangu inangoja, na ninatarajia neno lake.<br />

Nafsi yangu inangoja Bwana, kuliko walinzi wanaongoja asubuhi; ndiyo, walinzi<br />

wanaongoja asubui. Ee Israeli, utarajie Bwana.<br />

Maana pamoja na Bwana ni rehema, na pamoja naye ukombozi mwingi. Naye<br />

atakomboa Israeli na maovu yake yote.<br />

Zaburi 117<br />

Musifu Bwana, ninyi mataifa yote; mumutolee sifa, ninyi watu wote.<br />

Maana rehema yake kwetu ni kubwa; na kweli ya Bwana inakaa milele. Musifu<br />

Bwana.<br />

Utukufu kwa Baba, na kwa Mwana, na kwa Roho Mtakatifu, sasa na siku zote hata<br />

milele na milele.<br />

Kisha kusoma ile zaburi tunaimba hii sala:<br />

Mwangaza upole (ilaron) ya sifa mtakatifu, ya Baba Musiye kufa wa mbinguni,<br />

mtakatifu na heri, ee Yesu Kristo, kufika kuingia kwa jua, kuangalia mwangaza wa<br />

mangaribi; tunasifu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu Mungu mmoja, uko kweli wakati<br />

wote. Kukuimbia kwa ma sauti nzuri, ee Mwana wa Mungu, chemchem ya uzima,<br />

ulimwengu utaita sifa yako.<br />

Kisha tunaimba Prokimenon ya kila siku ya Juma:<br />

Siku ya Mungu Mangaribi. Sauti ya Mnane.<br />

Tazama ninyi munaobariki Bwana, ninyi watumishi wote wa Bwana<br />

(Mara tatu)

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!