Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
19<br />
Mungu Mtakatifu, Mweza Mtakatifu, Msiye kufa Mtakatifu,<br />
utuhurumie. (Mara tatu)<br />
Utukufu Kwa Baba. .. Sasa na siku. .. Utatu Mtakatifu kamili utuhurumie, Bwana<br />
utusamehe zambi zetu. Rabi utuondolee makosa yetu, Mtakatifu utukaribie ukatuponye<br />
magonjwa yetu. Bwana hurumia, Bwana hurumua, Bwana hurumia.<br />
Utukufu kwa Baba. .. Sasa na siku. ..<br />
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, mapenzi yako<br />
yatimizwe hapa duniani kama mbinguni, utupe leo chakula chetu cha kila siku,<br />
utusamehe makosa yetu kama sisi vilevile nasi tunawasamehe waliotukosea, tena<br />
tusishindwe na vishawishi, lakini utuokoe na yule mwovu.<br />
Apolitikion ya hii siku ao ya Siku Kuu. Kisha Utukufu.. . Sasa na siku zote.. .<br />
Theotokion.<br />
Kwa maombezi ya Wapadri wetu Watakatifu, ee Bwana Yesu Kristu, utuhurumie<br />
na utuokoe. Amina.<br />
Apodipnon Kidogo ni Sala ya Kanisa, somo yake linamaliza siku yetu.<br />
Inafanyika usiku; kisha chakula cha usiku. Ndio maana inaitwa Apo-dipnon, nikusema<br />
kisha dipnon, kisha chakula cha usiku.<br />
Tena tuko na na Apodipnon ingine ile tunaita «Apodipnon mukubwa» hii tunaisoma<br />
wakati wa Kwarezima Mkubwa. Hii Ibada ya Apodipnon Mukubwa inafanyika mu<br />
Kanisa saa ya Mangaribi mu Kazi moja, mu kazi mbili, mu kazi mbili, mu kazi tatu na<br />
mu kazi ine.<br />
APODIPNO KIDOGO<br />
(Sala ya usiku mbele ya Kulala)<br />
Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amina. Utukufu kwako, ee<br />
Mungu wetu, utukufu kwako.<br />
Mfalme wa mbinguni, wewe mfariji, Roho wa ukweli, uliye mahali popote na<br />
kuvijaza vitu vyote, hazina ya mema, tena Mupaji wa uzima, uje ukae kwetu, na<br />
kutusafisha kwa kila aibu, okoa roho zetu, wewe mwema. Amina.