You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
42<br />
KONTAKION. Sauti ya Mnane.<br />
Kwako, jemadari kunilinda nina deni<br />
kukushukuru kwa wokovu na kushinda wangu.<br />
Mimi muji wako, ee Mzazi Mungu.<br />
Tena kwa mamlaka yako si kushindwa,<br />
na hatari kila namna niepuwe kukuimba,<br />
kwa kelele kuu: Salamu, Bibi-Arusi, usiyeolewa.<br />
FUNGU 1<br />
I K O S 1<br />
Alitumwa toka mbinguni Malaika Mkuu kumwambia Mzazi-Mungu: Salamu.<br />
Yeye alipokuona wewe, ee Bwana, ukipata mwili mara ileile kwa sauti yake ya bilamwili,<br />
alistaajabu, akasimama na akasema na sauti kubwa.<br />
Salamu, kwa kuwa unaangaza wokovu wetu,<br />
Salamu, kwa kuwa katika wewe uovu uliondolewa,<br />
Salamu, uliyemusimamisha tena Adamu aliyeanguka,<br />
Salamu, uliyemwoka Eva halii tena.<br />
Salamu, ndiwe mlima kutofikika kwa mawazo ya wanadamu;<br />
Salamu, ndiwe bahari isiyoweza kufumbuliwa hata kwa macho ya Malaika,<br />
Salamu, kwa kuwa wewe ni kiti cha ezi na makao ya Mfalme,<br />
Salamu, kwa kuwa unamubeba Muumba wako.<br />
Salamu, ndiwe nyota iliyoonyesha Jua, Salamu, ndiwe tumbo Mungu alimojifanya<br />
mtu,<br />
Salamu, kwani katika wewe kiumbe kinapata upya;<br />
Salamu, kwani kwako Muumba anakuwa mtoto.<br />
Salamu, Bibi-Arusi usiyeolewa.<br />
I K O S 2<br />
Bikira Mtakatifu alipojua hali ya ubikira wake akamujibu Malaika Gabrieli na<br />
uhodari: Neno lako ni la ajabu rohoni mwangu, namna gani unasema nitachukua mimba,<br />
maana sijui mume?<br />
Alliluya.<br />
I K O S 3<br />
Kwa kufahamu fumbo isiyo julikana, Bikira akamuelekea Mtumishi na akauliza<br />
namna gani anaweza kuzaliwa Mwana tumboni mwake. Malaika mwenye kujaa na<br />
heshima akamuambia na furaha: Salamu, maana umefumbuliwa shauri iliyo siri, Salamu,